Serikali kuboresha viwanja vya maonesho ya Nanenane

Na. Moureen John, NANENANE

Waziri wa Kilimo, Hussein Bashe amesema serikali itaendelea kufanya maboresho katika viwanja vya maonesho ya Nanenane ikiwa ni mkakati wa kuchangia ukuaji wa uchumi nchini.


Waziri wa Kilimo, Hussein Bashe


Kauli hiyo aliitoa wakati wa uzinduzi maonesho ya kimataifa ya Nanenane kanda ya kati katika uwanja wa Nanenane Nzuguni jijini Dodoma.

Waziri Bashe alisema “Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan alitoa maelekezo mwaka jana jijini Mbeya kwamba serikali ianze kufanya mabadiliko ya ujenzi kwa viwanja vya maonesho ya Nanenane. Kiwanja cha kwanza ni Nzuguni, Dodoma na Mwakangale, Mbeya katika hali ya kawaida tungesema tumehairisha shughuli za Nanenane mpaka tumalize hali ya ujenzi lakini tukasema Nanenane itaendelea na ujenzi utaendelea kwa wakati mmoja. Ujenzi umeanza wa uwanja huu na ujenzi huo utakuwa ni wa awamu tatu mpaka utakapokamilika na awamu ya kwanza ndio imeanza na ilikuwa shughuli ya kuondoa watu waliokuwa wamevamia eneo hili tunawahukuru sana wao wenyewe kwa hiari yao walikubali kuondoka kwasababu wanaamini eneo hili ni mali ya serikali”, alisema Waziri Bashe.

“Serikali imeanza na ujenzi wa uzio, uwanja huu utakuwa na maeneo ya vipando, uwanja huu utakuwa na onesho la mifugo, uwanja huu utakuwa na maonesho ya shughuli za uzalishaji mwaka mzima. Lakini ndani ya uwanja huu kutakuwa na eneo la ‘conference facility’ na mikutano. Vilevile, kutakuwa na eneo la ‘incubation centre’ kwa ajili ya vijana wanaofanya teknolojia na hivi sasa shughuli za ujenzi zimeanza mpaka awamu zote zitakapokamilika. Serikali itatumia zaidi ya shilingi bilioni 40 kukamilisha miundombinu yote ya uwanja wa Nanenane Nzuguni Dodoma”, alisema Waziri Bashe.

Aidha, alimtaarifu Waziri Mkuu wa Tanzania aliyekuwa mgeni rasmi kuwa baada ya kukamilisha viwanja vya Nzuguni na Mwakangale wataenda hatua ya pili ambayo itahusisha viwanja vya Morogoro, Arusha, Lindi na Tabora.

Habari hii imehaririwa na Emmanuel Lucas kwa kushirikiana na Fadiga James

Comments

Popular Posts

Wananchi Makutupora wafunguka changamoto ya Maji, Umeme na Shule kwa Mkuu wa Mkoa

Waziri Mchengerwa apongeza usimamizi wa miradi jijini Dodoma

Mkataba ujenzi Uwanja wa Mpira wa Miguu wasainiwa Dodoma