DC Shekimweri awakaribisha wananchi kushiriki maonesho ya Nanenane

Na. Tutindaga Nkwindi, DODOMA

Mkuu wa Wilaya ya Dodoma, Alhaj Jabir Shekimweri ametoa pongezi kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kufanya maboresho ya miundombinu katika viwanja vya maonesho ya Siku ya Wakulima Duniani.


Hayo aliyasema wakati alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari na kuwakaribisha wananchi wote wa Jiji la Dododma na vionga vyake katika maonesho ya Siku ya Wakulima Duniani yanayohusu tasnia ya uvuvi, kilimo na mifugo yatakayofanyika katika viwanja vya Nanenane vilivyopo Kata ya Nzuguni, jijini Dodoma.

Alisema kuwa kwa maonesho ya wakulima duniani kwa mwaka 2025 katika Jiji la Dodoma yamekuwa na mabadiliko ya hali ya juu. “Kupitia maelekezo ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan alitaka mahema yajengwe ya kisasa na ya kudumu. Hivyo, maagizo hayo tumetekeza kwa kiasi kikubwa. Pia kwa upande wa barabara tumeweka miundombinu mizuri ya barabara ili kuepusha vumbi. Hivyo, kwa wale watakaokuja katika viwanja vya maonesho hawatapata vumbi kwa kuwa miundombinu imeboreshwa” alisema Alhaj Shekimweri.

Pia aliongeza kwa kusema kuwa maonesho hayo yatakuwa ya kimataifa, kutakuwa na nchi nane kutoka ukanda wa Afrika zitakazohudhuria na kufanya maonesho katika Jiji la Dodoma. “Kumekuwa na muamko mkubwa hususani katika taasisi na wadau wa kilimo, mifugo na uvuvi ambapo wadau wa kilimo zaidi ya 640 wamejisajili kuhudhuria. Hivyo, kwa maonesho ya mwaka huu yatakuwa yamefana sana kutokana na ongezeko kubwa wadau watakaohudhuria kutoka nchi mbalimbali” alisema Alhaj Shekimweri.

Aidha, mkuu huyo wa Wilaya ya Dodoma aliwakaribisha wananchi wote wanaohitaji kujifunza mambo mbalimbali kuhudhuria katika maonesho hayo kwasababu ni bure, yatakayoanza tarehe 01.08.2025 na kufunguliwa na Makamu wa Rais, Dkt. Phillip Mpango na kufungwa tarehe 08.08.2025 na Rais, Dkt. Samia Suluhu Hassan.

 

Comments

Popular Posts

Mfumo wa Ufuatiliaji na Tathmini ni nyenzo ya utendaji kazi serikalini – Dkt. Biteko

JIJI LA DODOMA KUPELEKA MIL 50 ZAHANATI YA KIKUYU

WENZA WA VIONGOZI WASHAURIWA KUANZISHA BUSTANI ZA NYUMBANI