DC Dodoma awapongeza wahitimu mafunzo ya stakabadhi

Na. Veronica Elias,

Mkuu wa Wilaya ya Dodoma, Alhaj Jabir Shekimweri amewapongeza wakufunzi wa semina ya usimamizi wa mafunzo ya stakabadhi kutoka wizarani na washiriki waliohitimu mafunzo hayo na kusema kuwa ni mafunzo muhimu.


Akizungumza na waandishi wa habari Shekimweri alisema kuwa mafunzo hayo yanaumuhimu kwa wakulima na wafanyabiashara kwasababu yanawawezesha kuona faida ya kile wanachokifanya pamoja na kupata mabalozi wengine kwaajili ya kwenda kutoa elimu kwa wakulima.

Alisema kuwa kutakuwa na mfumo rasmi wa kuratibu tasnia ya mazao mchanganyiko ilikusudi mkulima alindwe na anufaike na jasho lake kupitia nguvu na gharama alizopoteza kwenye uwekezaji huo Pamoja na wafanyabiashara kupata haki yao ya msingi kutokana na matarajio yao waliokusudia. “Najisikia furaha sana kufika katika semina hii kwasababu moja ya maoni yangu binafsi, mfumo wa stakabadhi wakati fulani unakutana na wapinzani kwa sababu ni kitu kipya ambacho hawakijui kwa muda huo. Hivyo, asilimia kubwa ya watu kukataa hayo mabadiliko ni maumbile ya kibinadamu. Moja ya ufumbuzi wa watu ambao wanapinga mfumo huu ni kutoa elimu na uhamasishaji wa mfumo wenyewe ambao ni meneja, watu wa rekodi, wasimamizi na watu wanaotunza kwenye maghala. Hapo wakipata mafunzo hata wakulima wanaokuja wanaweza kuwaelimisha na wanunuzi pia kwa namna moja ama nyingine” alisema Alhaj Shekimweri.

Mmoja wa washiriki wa mafunzo hayo, Zainabu Shomari alieleza kuhusiana na jinsi alivyonufaika na mafunzo na vitu vipya ambavyo amejifunza kupitia fursa hiyo. “Sipo kwenye kampuni ya aina yeyote bali nimekuja kwenye mafunzo kama mtu binafsi na katika msimu wa mafunzo 2025-2026 kitu kipya ambacho nimejifunza ni uingizaji wa ‘data’ kieletroniki. Pia na sheria ambazo zimewekwa zimetiliwa sana mkazo na ndizo zinatumika kurekebisha makosa maana kipindi cha nyuma watu walikuwa wanafanya makosa kwa makusudi. Wakulima watarajie mambo mazuri kupitia mazao yao na wakae wakijua yapo salama hata wanapokuwa wanatumia kuyapeleka ghalani” alisema Shomari.

 

 

Comments

Popular Posts

Mfumo wa Ufuatiliaji na Tathmini ni nyenzo ya utendaji kazi serikalini – Dkt. Biteko

JIJI LA DODOMA KUPELEKA MIL 50 ZAHANATI YA KIKUYU

WENZA WA VIONGOZI WASHAURIWA KUANZISHA BUSTANI ZA NYUMBANI