Mnadani wakumbushwa kuchukua tahadhari ya athari za mvua

 Na. Dennis Gondwe, MNADANI

WANANCHI wa Mtaa wa Mnadani wametakiwa kuchukua tahadhari ya athari inayoweza kusababishwa na mvua kwa kuhakikisha mazingira yanakuwa safi na mitaro ya kupitisha maji ya mvua haijaziba ili kuepusha mafuriko kwenye makazi ya watu.



Mwenyekiti wa Serikali ya Mtaa wa Mnadani, Hema Wawa alipokuwa akiongea na wananchi wa Mtaa wa mnadani


Tahadhari hiyo ilitolewa na Mwenyekiti wa Serikali ya Mtaa wa Mnadani, Hema Wawa alipokuwa akiwahutubia mamia ya wananchi wa Mtaa wa Mnadani katika mkutano wa hadhara uliofanyika katika mtaa huo.

Wawa alisema “tupo katika kipindi cha mvua, katika kipindi hiki milipuko ya magonjwa mbalimbali huwa inatokea. Ni vizuri tujitahadhari na mazingira ambayo ni hatarishi. Kama tulivyojadili suala la usafi wa mazingira linagusa kila mmoja wetu. Hivyo, tuchukue tahadhari kadri inavyohitajika. Kipindi hiki kuna watu kuharibiwa nyumba zao na vitu vyao kutokana na maji ya mvua. Tuhakikishe mitaro ya kupitishia maji ni safi na haijaziba. Toeni taarifa na sisi tutazifikisha sehemu husika, tukifanya hivyo, tutakuwa tumejijali wenyewe na kunusuru maisha ya ndugu zetu. Toeni taarifa sahihi na sisi tutafikisha taarika kwenye eneo husika, serikali ya mama Samia Suluhu Hassan ni sikivu na inachukua hatua”.

MWISHO


Comments

Popular Posts

Wananchi Makutupora wafunguka changamoto ya Maji, Umeme na Shule kwa Mkuu wa Mkoa

Waziri Mchengerwa apongeza usimamizi wa miradi jijini Dodoma

Mkataba ujenzi Uwanja wa Mpira wa Miguu wasainiwa Dodoma