Posts

Agenda ya Lishe yaongeza Ari ya usomaji S/M Dodoma Makulu

Image
Na. Abdul Iddi, DODOMA MAKULU Shule ya Msingi Dodoma Makulu imeshukuru agenda ya Rais, Dkt. Samia Suluhu Hassan ya lishe shuleni kwa sababu inawaongezea ari ya kusoma na kupata matokeo yanayokusudiwa. Shukrani hiyo ilitolewa na Mwalimu wa Lishe, Rehema Kalinga alipokuwa akiongea na waandishi wa Habari waliotembelea shule ya msingi Dodoma makulu kujionea hali ya lishe kwa wanafunzi shuleni hapo. Alisema kuwa shule yake inazingatia ajenda ya Lishe kwa kuwapa wanafunzi wote kuanzi awali mpaka darasa la Saba uji. Darasa la Nne na la Saba kupata chakula cha mchana. ā€œToka ajenda hii kuanza kutekelezwa, tumeanza kuona matokeo Chanya. Kwanza kwakupunguza utoro, pia watoto darasani wanafundishikaā€ alisema Mwl. Kalinga. Aidha, alitoa pongezi kwa wazazi kwa kusikiliza ajenda ya Lishe na kuitekeleza bila kusuasua kwasababu waliweza kutoa mchango kwa kiasi walicho kubaliana na kamati ya wazazi wa shule hiyo. ā€œMuitikio ni mkubwa kwasababu watoto wote katika Shule ya Dodoma Makulu wanapata uji ...

Kata ya Ipala ipo mstari wa mbele katika Michezo

Image
Na. Nancy Kivuyo, IPALA Hamasa ya serikali katika michezo nchini ni kichocheo cha wananchi wa Kata ya Ipala kupenda kushiriki michezo ya aina mbalimbali kwa ajili ya kujenga na kuboresha afya zao ili waweze kushiriki katika shughuli za maendeleo. Diwani wa Kata ya Ipala, George Magawa Kauli hiyo ilitolewa na Diwani wa Kata ya Ipala, George Magawa alipokuwa akiongea na waandishi wa habari kuhusu nafasi ya michezo katika Kata ya Ipala walipotembelea kata hiyo. Diwani Magawa alisema kuwa serikali imekuwa inafanya hamasa kubwa katika michezo hali iliyopelekea kata yao kuwa na mwamko mkubwa katika kushiriki mashindano mbalimbali yanayoandaliwa katani hapo. ā€œKwakweli, mambo ya michezo tunaenda nayo vizuri, kila mwaka tunafanya mashindano yanayoitwa ā€˜Magawa Cupā€™ ambayo diwani ndiye mimi na kwa kushirikiana na mheshimiwa mbunge tuna ā€˜Mavunde Cupā€™, tunaandaa mashindano hayo ili kuwasogeza wananchi karibu zaidi na michezo. Wakati mwingine tunaunganisha michezo na kampeni za kijamii za serika...

Umeme wa REA chachu ya viwanda vidogo vidogo Kata ya Ipala

Image
Na. John Masanja, IPALA Awamu ya kwanza ya umeme wa Wakala wa Nishati Vijijini (REA) umechochea shughuli za maendeleo na kuinua uchumi wa wananchi katika Kata ya Ipala, Halmashauri ya Jiji la Dodoma. Kauli hiyo ilitolewa na Diwani wa Kata ya Ipala, George Magawa wakati akizungumza na waandishi wa habari waliofanya ā€˜media tourā€™ kutembelea miradi ya maendeleo iliyotekelezwa na serikali katika kata hiyo kuanzia mwaka 2021 hadi 2025. Alisema kuwa serikali ya awamu ya sita imepeleka huduma ya umeme katika Kata ya Ipala. ā€œKata yetu imefikiwa na awamu ya kwanza ambayo ina faida nyingi sana. Wananchi wanafanya shughuli mbalimbali zinazojumuisha matumizi ya umeme kwa kiwango kikubwa na naamini kwa siku za usoni hapa kwetu kutakuwa mtaa wa viwanda vya aina tofautiā€ alisema Magawa. Nae mkazi wa Kata ya Ipala, Mathias Masita aliishukuru serikali kwa kuwapelekea umeme kwasababu maisha yao yamebadilika na wanafanya shughuli zinazohusisha umeme kwa kiwango kikubwa. ā€œMradi wa REA umetunufaisha s...

Usipange kukosa kukimbia na Mbunge wako

Image
 

Serikali yatoa fedha kujenga Kituo cha Jemolojia ili kuongea thamani ya Madini

Image
Na. Janeth Raphael MichuziTv -Dodoma Katibu Mkuu Wizara ya Madini, Mhandisi Yahya Samamba amesema kuwa katika kuhakikisha Madini yanaongezewa thamani kabla ya kupelekwa nje ya nchi, Serikali imetoa fedha nyingi na kujenga Kituo kikubwa cha Jemolojia ili kuwa na kituo bora, chenye mashine bora na wataalam bora nchi nzima ili kuhakikisha Madini hasa ya vito yanaongezewa thamani hapa nchini kwa viwango vinavyohitajika kabla ya kusafirisha kwenda nje. Mhandisi Samamba aliyasema hayo jijini Dodoma katika hafla fupi ya utiaji saini wa makubaliano kati ya Kampuni Sun Set kutoka Tailand na Taasisi ya Jemolojia Tanzania iliyoko chini ya Wizara ya Madini. Alisema kuwa watahakikisha kwamba wanaweka utaratibu wa namna ambavyo makubaliano hayo yatatekelezwa ili pande zote mbili waweze kunufaika na makubaliano hayo. ā€œKupitia Kituo chetu chetu cha TGC, Mheshimiwa Rais ameweka fedha nyingi, tumejenga jengo kubwa kabisa ambacho ni kituo kikubwa Afrika Mashariki na Afrika kwa ujumla ambapo lengo...

Waziri Mavunde asisitiza miradi mikubwa ya madini iliyopewa leseni kuanza kazi haraka

Image
Na. Mwandishi Wetu, DODOMA Waziri wa Madini, Anthony Mavunde, ameagiza miradi mikubwa na ya kati ya Madini ambayo tayari imekwishapewa leseni kuanza utekelezaji wake mara moja ili kuchochea ukuaji wa sekta na kuleta manufaa kwa taifa na kutimiza azma ya serikali kutoa leseni hizo. Waziri wa Madini, Anthony Mavunde Aliyasema jijini Dodoma wakati akizungumza katika mkutano maalum na Chemba ya Migodi Tanzania (TCM) kwa lengo kujadili masuala mbalimbali yanayohusu sekta ya Madini ili kuboresha uendelezaji na usimamizi wa shughuli za uchimbaji na biashara ya Madini kwa manufaa ya sekta na taifa kwa ujumla. Waziri Mavunde alisema serikali inataka kuhakikisha kuwa miradi yote ya uchimbaji Madini iliyopangwa kuanza inaanza mara moja bila kucheleweshwa, na kuwa serikali kwa upande wake imejitahidi kurahisisha taratibu kwa wawekezaji na sasa ni wakati wa sekta binafsi kuchukua hatua kwa upande wao. ā€œSerikali imefanya kazi yake, tumeondoa vikwazo vingi na kurahisisha utaratibu. Sasa ni juku...

Shule shikizi Ipala, mkombozi kwa wanafunzi wanaotembea umbali mrefu

Image
Na. John Masanja, IPALA Diwani wa Kata ya Ipala, George Magawa, aishukuru serikali ya awamu ya sita inayoongozwa na Rais, Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuboresha miundombinu ya elimu msingi katika kata hiyo kwa kujenga shule shikizi ili kutengeneza mazingira rafiki kwa wanafunzi wenye umri mdogo kupata elimu bora. Diwani wa Kata ya Ipala, George Magawa Aliyasema hayo wakati akizungumza na waandishi wa habari waliofanya ā€˜media tourā€™ kutembelea miradi ya maendeleo iliyotekelezwa na serikali katika Kata ya Ipala kuanzia mwaka 2021 hadi 2025. Diwani Magawa alisema kuwa katika miaka minne ya uongozi wa serikali ya awamu ya sita, elimu katika Kata ya Ipala imekuwa kwa kasi. ā€œSerikali yetu tukufu imetuletea elimu hadi kwenye kata yetu. Tuna shule shiziki mbili zimeanzishwa kwa lengo la kusaidia wanafunzi wadogo wanaotembea umbali mrefu karibu kilomita tano kufuata elimu. Sasa hivi uwepo wa madarasa haya matatu nafuu imekuwa kubwa sana kwa kuwapunguzia watoto wadogo kutembea umbari mrefuā€ ...

Nyumba ya mtumishi kuchangia huduma masaa 24 Zahanati ya Ipala

Image
Na. Nancy Kivuyo, IPALA Mradi wa ujenzi wa nyumba ya mtumishi katika Zahanati ya Ipala uliogharimu kiasi cha shilingi 55,000,000, umeleta maboresho katika utoaji wa huduma ya afya katika kata hiyo. Nyumba ya Mtumishi Zahanati ya Ipala Hayo yalielezwa na Muuguzi kutoka Zahanati ya Ipala, Tumain Sanga alipokuwa akiwaelezea waandishi wa habari waliofanya ā€˜media tourā€™ kutembelea miradi ya maendeleo iliyotekelezwa na serikali katika kata hiyo kuanzia mwaka 2021 hadi 2025. Alisema kuwa anatoa pongezi kwa serikali kuwajengea nyumba hiyo ili kurahisisha utoaji wa huduma za afya katika kata hiyo. ā€œTunaipongeza serikali kutujengea nyumba ya mtumishi, uwepo wa nyumba hii imeturahisishia kutendaji wa kazi mzuri. Laiti tungekuwa mbali tungeshindwa kuwahudumia wananchi vizuri na kwa wakati, lakini sasa wagonjwa wanaweza kuja muda wowote na wakatukuta na tukawahudumia kwa masaa 24. Tunaishukuru sana serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania inayoongozwa na Rais, Dkt. Samia Suluhu Hassan, tuna...

Wananchi wa Mtaa wa Mwaja, Jiji la Dodoma washiriki kufanya usafi wa mazingira wa Jumamosi ya mwisho wa Mwezi, Machi, 2025

Image
Leo tarehe 29.03.2025, wananchi wa Mtaa wa Mwaja, Kata ya Chamwino, Halmashauri ya Jiji la Dodoma wameshiriki zoezi la usafi wa Mazingira wa kila Jumamosi ya mwisho wa mwezi kwa lengo la kuweza mazingira safi kwa ajili ya afya zao. Usafi huo uliongozwa na Mwenyekiti wa Mtaa wa Mwaja, Athumani Makuka ambaye aliambatana na Afisa Mtendaji wa Mtaa, Mwanaasha Mani. Zoezi hilo la usafi lilifanyika katika mtaro unaopita pembezoni mwa Shule ya Msingi Chinangali ambao umehusisha kuzibua mtaro wenye urefu wa mita 100 sambamba na kutoa taka ngumu kama makopo na mifuko kwenye mtaro huo ili kuruhusu maji yaliyotuwama kwa sababu ya mvua kutiririka pasina kizuizi chochote.

Ukarabati tanki la Maji Kata ya Ipala waleta neema kwa wananchi

Image
Na. John Masanja, IPALA Ukarabati mradi wa tanki la maji la Lita 90,000 katika Kata ya Ipala, waleta ahueni kwa wananchi na kuwapunguzia adha ya kutembea umbali mrefu kufuata maji kwa matumizi mbalimbali. Akizungumza na waandishi wa habari waliofanya ā€˜media tourā€™ kutembelea miradi ya maendeleo iliyotekelezwa na serikali katika Kata ya Ipala kuanzia mwaka 2021 hadi 2025, Diwani George Magawa aliishukuru serikali kwa kutoa fedha shilingi 43,406,300 kwaajili ya ukarabati wa tanki la mradi mkubwa wa Maji Ipala. ā€œWananchi sasa wanapata maji safi na salama. Kwahiyo, tunaishukuru serikali, tunamshukuru sana mbunge wetu na wataalam mbalimbali. Kata imechimba visima vinne kwaajili ya kupata maji safi na kupunguzia wananchi adha ya kutumia maji yasiyo salama. Hivi visima vinapunguza adha ya kwenda umbali mrefu kufuata maji ambayo mara nyingi siyo salama. Hivyo, wananchi wa kata yetu tatizo hili la uhaba wa maji limepungua sanaā€ alisema Magawa. Kwa upande wake Mwenyekiti wa Bodi ya Maji Hombo...