Mil. 838 zakopeshwa wanawake, vijana na wenye ulemavu Jiji la Dodoma
Na. Dennis Gondwe, DODOMA Halmashauri ya Jiji la Dodoma imetoa mikopo ya shilingi 838,775,212 kwa vikundi 54 katika kipindi cha Mwaka wa Fedha 2024/2025 hadi kufikia Oktoba 2025/2026 kwa lengo la kuviongezea mtaji wa kutekeleza shughuli za kujikwamua kiuchumi. Kauli hiyo ilitolewa na Mkurugenzi wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Dkt. Frederick Sagamiko alipokuwa akiwasilisha taarifa ya utendaji kazi kwa kipindi cha kuanzia Mwezi Juni hadi Oktoba, 2025 katika mkutano wa kwanza wa halmashauri baada ya Uchaguzi Mkuu wa Rais, Wabunge na Madiwani. Alisema kuwa vikundi 17 vya wanawake vilikopeshwa shilingi 274,334,000, vikundi 26 vya vijana vilikopeshwa shilingi 460,041,212 na watu wenye ulemavu vikundi 11 vilikopeshwa shilingi 104,400,000. Akiongelea uchangiaji wa michango ya asilimia 10, alisema kuwa mwaka 2024/2025 halmashauri ilitenga shilingi 4,032,510,000, kwa mwezi Juni, 2024/2025, jumla ya shilingi 373,778,597.12 zimechangiwa katika mfuko. “Mwaka 2025/2026 halmashauri imetenga b...