Halmashauri ya Jiji la Dodoma Yatoa Mafunzo ya Malisho ya Mifugo
Na. Rehema Kiyumbi, DODOMA Afisa Mifugo katika Halmashauri ya Jiji la Dodoma Leonia Msuya ameendelea kutoa elimu kwa wakulima na wafugaji namna ya kulisha na kutunza mifugo yao kwa maendeleo ya kiuchumi. Aliyasema hayo wakati akiwa katika vipando vya Halmashauri ya Jiji la Dodoma katika maadhimisho ya kimataifa Nanenane. ’’Tumejiandaa kutoa elimu na kuonesha maonesho ya malisho ambayo ni chakula cha mifugo kwa sababu yamepanuka sana wananchi na wahamiaji wamekuwa wengi ambapo kusababisha malisho kupungua. Kwa mwaka huu tumeandaa vipando vitatu ambavyo ni malisho ya mikunde, nyasi na magugu (sumu) ambapo huchanganywa ili ng’ombe kupata virutubisho ambavyo ni protini, mafuta na wanga kama sisi binadamu,” alisema Msuya. Alisema kuwa aina ya malisho ambayo ni sumu huchangia kutoa elimu kwa wakulima na ni moja ya kutunza mazingira. ’’Sumu ni aina ya malisho kama mihogo na nyanya tumefanya makusudi ili mkulima na mfugaji kuweza kuyaondoa kwenye shamba lake. Pia, mkulima na mfugaji ...