Posts

Mil. 838 zakopeshwa wanawake, vijana na wenye ulemavu Jiji la Dodoma

Image
Na. Dennis Gondwe, DODOMA Halmashauri ya Jiji la Dodoma imetoa mikopo ya shilingi 838,775,212 kwa vikundi 54 katika kipindi cha Mwaka wa Fedha 2024/2025 hadi kufikia Oktoba 2025/2026 kwa lengo la kuviongezea mtaji wa kutekeleza shughuli za kujikwamua kiuchumi. Kauli hiyo ilitolewa na Mkurugenzi wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Dkt. Frederick Sagamiko alipokuwa akiwasilisha taarifa ya utendaji kazi kwa kipindi cha kuanzia Mwezi Juni hadi Oktoba, 2025 katika mkutano wa kwanza wa halmashauri baada ya Uchaguzi Mkuu wa Rais, Wabunge na Madiwani. Alisema kuwa vikundi 17 vya wanawake vilikopeshwa shilingi 274,334,000, vikundi 26 vya vijana vilikopeshwa shilingi 460,041,212 na watu wenye ulemavu vikundi 11 vilikopeshwa shilingi 104,400,000. Akiongelea uchangiaji wa michango ya asilimia 10, alisema kuwa mwaka 2024/2025 halmashauri ilitenga shilingi 4,032,510,000, kwa mwezi Juni, 2024/2025, jumla ya shilingi 373,778,597.12 zimechangiwa katika mfuko. “Mwaka 2025/2026 halmashauri imetenga b...

Madiwani watakiwa kuifanya Dodoma kuwa kinara ukusanyaji mapato

Image
Na. Dennis Gondwe, DODOMA MKUU wa Wilaya ya Dodoma, Alhaj Jabir Shekimweri amelitaka Baraza la Madiwani kuendelea kuifanya Halmashauri ya Jiji la Dodoma kuwa kinara katika utekelezaji wa miradi ya maendeleo kupitia mapato ya ndani ili kuwaletea wananchi maendeleo na kuboresha maisha yao. Kauli hiyo aliitoa alipokuwa akiwasalimia madiwani katika mkutano wa kwanza wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma uliofanyika katika ukumbi wa halmashauri jijini hapa. Alhaj Shekimweri alisema “katika mapato ya ndani mmekuwa vinara katika kutekeleza miradi mizuri   ya maendeleo. Tumeona miradi ya hoteli, mradi wa Soko la wazi la Machinga, miradi ya ujenzi wa barabara, mfano ile ya Nala kuelekea hospitali ya jiji na miradi mingine mingi. Nendeni mkawe vinara wa kutekeleza miradi ya maendeleo. Ninayasema haya kwa kumuenzi Rais, Dkt. Samia Suluhu Hassan kwamba mnapochukua madaraka yale mema yaliyoanzishwa na wenzenu msiyaweke kando, ambayo hayajakamilika mkayakamilishe, yanayoendelea mkayakalishe huku ...

Madiwani Jiji la Dodoma watakiwa kuwa walezi

Image
Na. Dennis Gondwe, DODOMA MADIWANI wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma wametakiwa kutumia nafasi yao na kuwa walezi kwa maafisa watendaji katika kata zao na kuwasimamia ili kuwaletea maendeleo wananchi. Rai hiyo ilitolewa na Mkuu wa Wilaya ya Dodoma, Alhaj Jabir Shekimweri alipokuwa akiongea na madiwani katika mkutano wa kwanza wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma baada ya Uchaguzi Mkuu wa Rais, Wabunge na Madiwani wa tarehe 29 Oktoba, 2025. “Waheshimiwa Madiwani, nataka niwaombe sana mkawalee maafisa watendaji wenu kwenye ngazi ya kata. Mstahiki Meya, ninasema hapa kwa kuwaangukia na kuwaomba, mkawe walezi, ninyi ndiyo wenyeviti wa kamati za maendeleo kwenye kata, mkono wako wa kulia ni katibu, ambae ni Afisa Mtendaji wa Kata. Watendaji hawa inawezekana wakawa na madhaifu ya hapa na pale, nenda ukawe mlezi, nenda ukawe mzazi, yeye pamoja na wataalam wengine ngazi ya kata. Wasaidieni wafanye majukumu yao sawasawa ili wewe upate matokeo na kuwaletea wananchi maendeleo. Mimi, nitakusifu san...

Madiwani Jiji la Dodoma watakiwa kutoa tamko la rasilimali na madeni

Image
                                              Na. Dennis Gondwe, DODOMA SEKRETARIETI ya Maadili ya Viongozi wa Umma imewataka madiwani wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma kutoa tamko la rasilimali na madeni kwa mujibu wa sheria. Kauli hiyo ilitolewa na Katibu Msaidizi Kanda ya Kati, Ofisi ya Rais, Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma, Jasmin Bakari wakati akiwaongoza kutoa tamko la kimaandishi la ahadi ya uadilifu kwa viongozi wa umma katika ukumbi wa mikutano wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma. “Niwapongeze kwa kufanikiwa kuchaguliwa kuwa madiwani, ni mategemeo yetu mtatekeleza majukumu yenu kwa viwango vya juu vya maadili, na mviishi viapo vyenu. Niwakumbushe madiwani na viongozi wote waliopo hapa kutoa tamko la rasilimali na madeni, tunawakumbusha kuingia kwenye mfumo kwa wale wapya kuna sehemu ya kujisajili. Kwa wale waliokuwa baraza lililopita wataingia kwa aka...

Jiji la Dodoma lakusanya 104% Mapato ya ndani 2024/2025

Image
Na. Dennis Gondwe, DODOMA HALMASHAURI ya Jiji la Dodoma ilikusanya shilingi 65,042,215,034 sawa na asilimia 104 ya lengo la mwaka la mapato ya ndani kwa Mwaka wa Fedha 2024/ 2025. Kauli hiyo ilitolewa na Mkurugenzi wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Dkt. Frederick Sagamiko alipokuwa akiwasilisha taarifa ya utendaji kazi kwa kipindi cha kuanzia Mwezi Juni hadi Oktoba, 2025 katika mkutano wa kwanza wa halmashauri baada ya uchaguzi mkuu wa Rais, Watunge na Madiwani. Alisema kuwa baada ya kuvunjwa kwa Baraza la Madiwani Mwaka 2025/2026 Menejimenti ya Halmashauri ya Jiji la Dodoma iliendelea na jukumu la kukamilisha ukusanyaji wa mapato kwa kipindi cha mwaka 2024/2025. “Kwa Mwaka huo wa fedha, halmashauri ilikusudia kukusanya shilingi 143,164,202,949.46 na hadi kufikia tarehe 30 Juni, 2025, ukusanyaji wa mapato ya ndani ulikuwa shilingi 65,042,215,034 sawa na asilimia 104 ya lengo la mwaka na kufanya ukusanyaji wa mapato yote ya halmashauri kuwa shilingi 152,269,204,654 sawa na asilimi...

Diwani Alimwoni Chaula, achaguliwa Meya Jiji la Dodoma

Image
Na. Dennis Gondwe, DODOMA Baraza la Madiwani la Halmashauri ya Jiji la Dodoma katika mkutano wake wa kwanza limemchangua Alimwoni Simon Chaula, Diwani wa Kata ya Makutupora kuwa Mstahiki Meya wa Jiji hilo kwa kupata kura za ndiyo 57 sawa na asilimia 100 ya kura zote zilizopigwa. Akitangaza matokeo ya kura zilizopigwa, Mwenyekiti wa Mkutano wa Halmashauri, Sakina Mbugi alitangaza kuwa Diwani Alimwoni Chaula alipata kura 57 kati ya kura 57 zilizopigwa na wajumbe. “Niwapongeze wajumbe wote halali mlioshiriki kupiga kura kwa nafasi ya Mstahiki Meya na Naibu Meya. Naomba kutanga za matokeo kama ifuatavyo. Nafasi ya Mstahiki Meya, kura 57 zilipigwa, hakuna kura ambayo haikupigwa. Kura zote 57 ni kura za ndiyo. Kwa matokeo hayo, ninamtangaza rasmi Mheshimiwa Alimwoni Chaula kuwa Mstahiki Meya wa Jiji la Dodoma. Nafasi ya Naibu Meya, jumla kura zilizopigwa 55 kati ya kura 57. Wajumbe wawili hawakupiga kura. Kura za ndiyo ni zote 55. Hivyo, ninatangaza rasmi kuwa Mheshimiwa Bakari Fundikira a...

DC Shekimweri asisitiza semina elekezi kwa madiwani Dodoma

Image
Na. Dennis Gondwe, DODOMA MKUU wa Wilaya ya Dodoma, Alhaj Jabir Shekimweri amesema kuwa semina elekezi kwa madiwani wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma ni muhimu ili kuwapa maarifa na kufanya uendeshaji wa mikutano ya halmashauri kuwa ya viwango kwa mujibu wa kanuni zilizopo. Kauli hiyo aliitoa alipokuwa akiwasalimia madiwani katika mkutano wa kwanza wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma baada ya Uchanguzi Mkuu wa Rais, Wabunge na Madiwani wa tarehe 29 Oktoba, 2025. “Ninawapongeza kwa dhati Mstahiki Meya, Chaula na Naibu Meya, Fundikira kwa kuchaguliwa kwa kura nyingi na baraza hili. Ninyi bado ni vijana, kwa hiyo baraza hili lina sura ya viongozi wa vijana. Ukiangalia waheshimiwa madiwani wengi pia ni vijana, hapo peke yake ni fursa lakini pia ni changamoto msipoangalia vizuri. Nami niungane na mtoa hoja wa kwanza, kwamba yakaandaliwa mafunzo na kupata semina elekezi ili msheheni maarifa, uelewa wa taratibu za vikao, lakini kanuni za kudumu za Baraza la Madiwani. Kwa sababu katika mkutano...

M/Kiti CCM apewa kongole kuchagua safu makini ya madiwani

Image
Na. Dennis Gondwe, DODOMA MWENYEKITI wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Wilaya ya Dodoma amepongezwa kwa kupanga safu makini ya wagombea nafasi ya udiwani jambo lililowawezesha kushinda kwa kishindo katika Uchaguzi Mkuu wa Oktoba, 2025. Pongezi hizo zilitolewa na Mkuu wa Wilaya ya Dodoma, Alhaj Jabir Shekimweri alipotoa salamu katika mkutano wa kwanza wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma uliofanyika katika ukumbi wa halmashauri. Alhaj Shekimweri alisema “nichukue nafasi hii kuwapongeza waheshimiwa madiwani kwa kuchaguliwa kwa kishindo kuwa madiwani kwa kata zenu, ninyi mnatokana na CCM. Mstahiki Meya, nichukue nafasi hii kumpongeza Mwenyekiti, Charles Mamba kwa kuteua madiwani wazuri waliofanya kampeni zao kistaarabu na kuchaguliwa kwa kishindo kuunda Baraza la Madiwani la Jiji la Dodoma”. Aidha, aliwapongeza wabunge wa Jimbo la Dodoma Mjini na Mtumba kwa kuchaguliwa kuwa wabunge. “Mstahiki Meya, ulikuwa ni Uchaguzi wa Rais, Wabunge na Madiwani, nichukue nafasi hii kuwapongeza wabunge wetu...

Waziri Mkuu amtaka Mkandarasi kukamilisha Soko Kuu la Majengo kwa wakati

Image
Na. Nancy Kivuyo, DODOMA Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania , Dkt. Mwigulu Nchemba atembelea Soko Kuu la Majengo jijini Dodoma leo kwa ajili ya kukagua maendeleo ya ukarabati wa soko hilo na kutoa maagizo kwa m kandarasi anayekarabati soko hilo kuhakikisha kazi inakamilika kwa wakati na kwa ubora unaostahili. Katika ziara hiyo, Waziri Mkuu aliambatana na viongozi wa Mkoa wa Dodoma pamoja na Halmashauri ya Jiji la Dodoma ambapo alisomewa taarifa ya ukarabati wa miundombinu mbalimbali inayoboreshwa kama vile maeneo ya biashara, mitaro ya maji ya mvua, mifumo ya usalama na umeme. Baada ya taarifa hiyo , Waziri Mkuu alisema kuwa serikali imejipanga kuhakikisha soko linarejea katika matumizi haraka ili kuwezesha wananchi na wafanyabiashara kunufaika na miundombinu bora. “Mradi huu ni muhimu sana kwa wananchi wa Dodoma na lazima ukamilike kwa wakati na kwa kiwango bora. Mkandarasi hakikisha soko hili linakamilika kama ambavyo mkataba unasema. Nanyi jiji naelekeza kuwa soko l...

Kamati za kudumu zatakiwa kuchangia kasi utekelezaji miradi ya maendeleo

Image
Na. Dennis Gondwe, DODOMA Mstahiki Meya wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Alimwoni Chaula alimtangaza Mwenyekiti wa Kamati ya kudumu ya Maadili ya Halmashauri ya Jiji la Dodoma kuwa ni Omary Omary, Diwani wa Kata ya Makole, aliyepata kura zote tano kutoka kwa wajumbe wa kamati hiyo. Mwenyekiti wa Kamati ya Maadili ya Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Omary Omary (kushoto) ambae ni Diwani wa Kata ya Makole. Kulia ni Naibu Meya wa Jiji la Dodoma, Bakari Fundikira ambae pia ni Diwani wa Kata ya Chang'ombe Alisema kuwa kamati hiyo ina jumla ya wajumbe watano ambao ni Omary Omary (Diwani Kata ya Makole), Swalihina Athuman (Diwani Kata ya Viwandani), Charles Ngh’ambi (Diwani Kaya ya Mbalawala), Judith Mushi (Diwani Viti Maalum) na Mwamrisho Kasule (Diwani Viti Maalum). Mstahiki Meya aliwasoma wajumbe wa kamati nyingine kuwa ni Robert Njama, Diwani wa Kata ya Mkonze na Flora Liacho, Diwani wa Viti Maalum kuwa wajumbe wa Kamati ya Mfuko wa Jimbo la Dodoma Mjini. Wengine ni Elis Kitendya, ...