Posts

Halmashauri ya Jiji la Dodoma yashiriki maadhimisho ya Wiki ya Utumishi wa Umma

Image
Na. Nancy Kivuyo, DODOMA Halmashauri ya Jiji la Dodoma inashiriki maadhimisho ya Kitaifa ya Wiki ya Utumishi wa Umma, yanayojumuisha Taasisi za Serikali, Bunge na Mahakama, katika uwanja wa Chinangali Park jijini Dodoma. Maadhimisho hayo yanalenga kuonesha uwajibikaji wa taasisi katika utoaji wa huduma kwa wananchi pamoja na kutoa elimu mbalimbali. Hayo yalisemwa na Afisa Utumishi, Patrick Bashemela alipokuwa akitoa utambulisho wa huduma zinazopatikana katika banda la halmashauri. “Maadhimisho ya Wiki ya Utumishi wa Umma yanatupa fursa nzuri ya kuonesha namna huduma zetu zinawafikia wananchi, banda letu linatoa huduma ya ukataji wa leseni ya biashara, elimu ya matumizi ya mfumo wa Tausi, elimu ya juu ya mikopo ya asilimia 10 na huduma ya uuzaji viwanja. Huduma zote muhimu zinazotolewa halmashauri, zitapatikana hapa kwa siku zote za maadhimisho” alisema Bashemela. Alimalizia kwa kuwakaribisha watumishi wote na wananchi kutembelea banda la halmashauri ili kupata elimu ya huduma mba...

Mexime awaonya mastaa Dodoma Jiji FC, aitaja nafasi ya tano

Image
Na. Mussa Richard, DODOMA. Kocha Mkuu wa Klabu ya Soka ya Dodoma Jiji FC, Mecky Mexime amewataka wachezaji wa timu hiyo kuzingatia yale waliyojifunza kwenye uwanja wa mazoezi ili kuhakikisha wanashinda mchezo dhidi ya Singida Black Stars na waweze kutimiza malengo waliyojiwekea kwa msimu huu. Mexime aliyasema hayo wakati wa mkutano na waandishi wa habari kuelekea mchezo huo ambapo walima zabibu wa Dodoma Jiji FC watavaana na kikosi cha Singida Black Stars ikiwa ni duru ya lala salama ya Ligi Kuu ya NBC Tanzania Bara, mchezo unaotarajiwa kuvurumishwa majira ya saa 10 kamili jioni katika uwanja wa Jamhuri Dodoma. “Tumejiandaa kuhakikisha tunafanya vizuri kwenye mchezo huu ili tuweze kusogea nafasi za juu zaidi kwasababu nafasi ya tano bado iko wazi kwa yeyote atakayechanga karata zake vizuri ataweza kuishika. Sisi Dodoma Jiji FC mipango yetu ni kufika nafasi ya tano, kikubwa ni wachezaji kuzingatia kile tulichojifunza kwenye uwanja wa mazoezi na kuja kukionesha uwanjani” alisema Mexi...

Jiji la Dodoma lafikisha 93% ya ukusanyaji Mapato

Image
Na. Dennis Gondwe, DODOMA MKUU wa Mkoa wa Dodoma, Rosemary Senyamule ameipongeza Halmashauri ya Jiji la Dodoma kwa kufikia asilimia 93 ya makusanyo ya mapato ya ndani hadi kufikia tarehe 31 Mei, 2025 na kusema kuwa ukusanyaji huo unatoa matumaini ya kufikia lengo ifikapo mwisho wa mwaka wa fedha. Pongezi hizo alizitoa katika mkutano maalum wa Baraza la Madiwani la Halmashauri ya Jiji la Dodoma kwa ajili ya kupitia na kujadili taarifa ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) uliofanyika katika ukumbi wa mikutano wa halmashauri. Senyamule alisema kuwa kwa mujibu wa taarifa ya uchambuzi wa mapato ya mamlaka za serikali za mitaa kwa Mkoa wa Dodoma uliofanywa na wataalam wa ofisi yake hadi kufikia tarehe 31 Mei, 2025 Halmashauri ya Jiji la Dodoma ilikuwa imekusanya asilimia 93. “Hivyo, niendelee kusisitiza menejimenti ya halmashauri kuongeza nguvu ya ukusanyaji wa mapato ili kuhakikisha kuwa asilimia saba iliyobaki inakusanywa kabla ya tarehe 30 Juni, 2025. Wataalamu wangu ...

RC Senyamule aipongeza Halmashauri ya Jiji la Dodoma kupata Hati safi

Image
Na. Dennis Gondwe, DODOMA MKOA wa Dodoma umeipongeza Halmashauri ya Jiji la Dodoma kwa kupata hati safi ya ukaguzi wa hesabu za serikali kwa hesabu zinazoishia tarehe 30 Juni, 2025. Pongezi hizo zilitolewa na Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, Rosemary Senyamule katika mkutano maalum wa Baraza la Madiwani kwa ajili ya kupitia na kujadili taarifa ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) uliofanyika katika ukumbi wa mikutano wa halmashauri. “Mheshimiwa Naibu Meya, naomba nitumie nafasi hii kuipongeza Halmashauri ya Jiji la Dodoma kwa kupata hati safi ya ukaguzi wa hesabu za serikali kwa hesabu zinazoishia tarehe 30 Juni, 2025. Hati safi hii ya ukaguzi inaifanya halmashauri kuendelea kupata hati safi tangu mwaka 2017/2018 hadi sasa. Kitendo hiki kinaipa heshima kubwa halmashauri na mkoa kwa kazi kubwa mnayoendelea kuifanya. Mafanikio haya makubwa yanatokana na ushirikiano wenu mkubwa waheshimiwa madiwani, watendaji wa jiji na viongozi mbalimbali. Hivyo, nawasihi kuendelea kudumish...

Prof. Kabudi atoa salam za pongezi kwa wataalam walioshiri kutengeneza Sheria ya Mazingira

Image
Na. Nancy Kivuyo, Dodoma Waziri wa Habari, Sanaa, Michezo na Utamaduni, Prof. Palamagamba Kabudi amewasihi viongozi wenye mamlaka ya kusimamia Sheria ya Mazingira ngazi zote kuziweka katika utekelezaji ili utunzaji wa mazingira ufanikiwe kwa asilimia zote. Aliyasema hayo wakati akitoa salamu katika maadhimisho ya Siku ya Mazingira Duniani kitaifa yaliyofanyika jijini Dodoma katika ukumbi wa Jakaya Kikwete. Prof. Kabudi alisema kuwa utunzaji wa mazingira ni jambo mtambuka wananchi wote wanapaswa kulifahamu. Aliomba pia kuwatambua wataalam waliohusika katika utengenezwaji wa Sheria ya Mazingira. “Mheshimiwa Makamu wa Rais, na viongozi mliopo hapa, mimi pamoja na wataalam wa sheria tulishiriki mchakato wa kuandaa Sheria ya Mazingira ambao ulikua na safari ndefu, lakini tunashukuru tulifanikiwa kwa kiwango kikubwa na leo tupo hapa. Nawapongeza sana japokuwa kuna wenzetu kwa isivyo bahati wametangulia mbele za haki” alisema Prof. Kabudi. Aliongeza kuwa baada ya kuandaa sheria ile kish...

Dkt. Mpango ahimiza elimu kwa jamii juu ya utunzaji wa Mazingira

Image
Na. Nancy kivuyo, DODOMA Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Philip Mpango atoa rai kwa tasnia ya habari, taasisi na wananchi wote kushirikiana kutoa elimu kwa jamii juu ya utunzaji wa mazingira ili kupunguza madhara yatokanayo na uharibifu wa mazingira. Aliyasema hayo akiwa mgeni rasmi katika maadhimisho ya Siku ya Mazingira Duniani kitaifa yaliyofanyika jijini Dodoma katika ukumbi wa Jakaya Kikwete. Dkt. Mpango alisema kuwa suala la usimamizi wa mazingira ni la kipaumbele katika maendeleo ya nchi. “Waheshimiwa viongozi mliopo hapa, chanzo kikubwa cha uharibifu wa mazingira ni tabia ya watu na pia mabadiliko ya tabia nchi. Yote haya hasara yake kidunia ni makubwa sana, takriban dola bilioni 300-600 kila mwaka zinapotea. Kwa mantiki hiyo ili kupata mazingira safi lazima wote tuwajibike” alisema Dkt. Mpango. Aliongeza kuwa nchi yetu inapambana kuhakikisha kwamba kwa miaka ijayo taka za pastiki zitokomezwe kwa kiwango kikubwa. Taka hizi za plastiki zinatelekezwa...

Shilingi Milioni 473 kutekeleza Mradi wa Ufungaji CCTV Kamera Jiji la Dodoma

Image
Na. Josephina Kayugwa, DODOMA Halmashauri ya Jiji la Dodoma imesani mkataba na Kampuni ya Wisjane Smart Systems kwaajili ya ufungaji wa kamera za usalama barabarani (CCTV) unaogharimu shilingi 473,000,000 ikiwa ni mradi utakaotekelezwa kwa kipindi cha miezi mitatu. Akitoa taarifa ya mradi, Mkuu wa Kitengo cha Teknolojia ya Habari na Mawasiliano (TEHAMA) Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Joseph Fungo alisema kuwa mradi huo utakwenda kuimarisha ulinzi na usalama katika Jiji la Dodoma kwasababu kamera hizo zitafanya kazi masaa 24. “Mradi huu wa gharama ya shilingi 473,000,000 utahusisha ufungaji wa kamera kwenye barabara zinazoinga njia kuu lakini pia hapo baadae utakuja kuimarishwa zaidi kwa kuongeza sehemu nyingine za kuweka kamera lengo ni kupata picha zote za vyombo vya usafiri vitakavyokuwa vikiingia na kutoka katika Jiji la Dodoma” alisema Fungo. Aliongeza kuwa wana mpango wa kuunganisha mfumo huo na taasisi nyingine ili kuimarisha ulinzi na usalama. “Mfumo huu baada ya muda tuta...

Shule ya Sekondari ya Bil. 3.9 kujengwa Kata ya Chahwa

Image
Na. Emanuel Charles, CHAHWA Hafla ya kusaini Mkataba wa Ujenzi wa Shule ya Sekondari Chahwa wenye thamani ya shilingi bilioni 3.9 baina ya Mkurugenzi wa Jiji la Dodoma na Mkandarasi kutoka Gopa contractors Tanzanian Limited imefanyika katika Kata ya Chahwa ukilenga kusogeza huduma ya elimu karibu na wananchi. Mradi huo unatekelezwa kwa mapato ya ndani ya Halmashauri ya Jiji la Dodoma ukiwa ni ujenzi wa shule ya ghorofa nne yenye madarasa 12, maktaba pamoja na maabara nne, chumba cha TEHAMA na jengo la utawala na unatarajiwa kukamilika ndani ya mwaka mmoja. Akizungumza katika utiaji saini wa ujenzi wa shule hiyo Mbunge wa Jimbo la Dodoma Mjini, Anthony Mavunde alitoa pongezi kwa serikali kwa kuendelea kuboresha sekta ya elimu na kuleta miradi mikubwa katika maeneo ya nje ya Mji wa Dodoma. “Tunamshukuru sana Mheshimiwa Rais kwa mradi huu mkubwa kwasababu unaenda kuleta mapinduzi makubwa katika sekta ya elimu, ndugu zangu ni wakati sasa maeneo ya pembezoni mwa Jiji la Dodoma yanufaike...

Soko la Sabasaba kuongozwa kwa misingi ya uongozi bora

Image
Na. Nancy Kivuyo, DODOMA Kaimu Mkuu Divisheni ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Abdul Chacha amewaasa viongozi wa Soko la Sabasaba kuzingatia weledi katika kufanya kazi zao ili kuiishi dhana ya uongozi bora. Aliyasema hayo katika mafunzo waliyoandaa kwa viongozi wa Soko la Sabasaba yaliyofanyika katika Ukumbi wa Kituo kikuu cha Mabasi Dodoma. Alisema kuwa sifa mojawapo kubwa ya kiongozi bora ni yule mwenye kuzingatia katiba au muongozo wa ushirika ili aweze kutenda haki. “Kiongozi bora ni yule anayejua namna ya kutuimia katiba vizuri. Labda niulize hapa, Katiba ya ushirika ipo? Kama ipo, je ilitumika wakati ule matatizo yameanza kutokea? Jibu litakua hapana. Nipende kuwaambia kuwa, ukiijua vizuri katiba na miongozo, ni rahisi sana Kutenda haki kwasababu utatenda haki kwa kuzingatia taratibu na hakuna atakayelalamika kuwa ameonewa” alisema Chacha. Aliongeza kuwa zipo sifa zaidi ya 25 za kiongozi bora ambapo kila kiongozi wa soko la sabasaba anapaswa ...

Bima ya Taifa ya Afya yatoa huduma kieletroniki

Image
Na. Leah Mabalwe, DODOMA Maboresho ya huduma ya Bima ya Afya yamefanywa kwa kuzingatia ukuaji wa teknolojia ambapo wananchi wanaweza kujisajili kupata huduma za bima kupitia simu zao na vifaa vya kieletroniki vyenye ‘Internet’. Hayo yalisemwa na Afisa Wanachama Mwandamizi, Bima ya Afya Mkoa wa Dodoma, Bakary Hamdun katika Mkutano wa Baraza la Madiwani la Halmashauri ya Jiji la Dodoma lililofanyika katika ukumbi wa mikutano wa halmashauri wakati akiwasilisha sheria ya afya na kanuni zake. Alisema kuwa kila mwanachama anaetarajia kujiunga na Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF) anaweza kujihudumia kupitia simu ya mkononi “Mwanachama yeyote awe mtumishi au mwananchi wa kawaida anaweza kujisajili kupitia simu yake ya mkononi. Na anaweza kufanya hivyo bila kuwa na changamoto ya aina yoyote kwasababu huduma hii ni rahisi pia inafanyika kwa muda mfupi” alisema Hamdun. Kwa upande wake Mstahiki Meya wa Jiji la Dodoma, Prof. Davis Mwamfupe aliipongeza serikali kwa hatua kubwa ya uboresha...