Posts

Madiwani Jiji la Dodoma wasisitizwa kufanya kazi kwa weledi na ushirikiano

Image
Na. Mwandishi Wetu, DODOMA Madiwani wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma wapongezwa kwa kuaminiwa na wananchi na kutakiwa kufanya kazi kwa uwajibikaji, ushirikiano na weledi wa hali ya juu. Hayo aliyasema Mkuu wa Wilaya ya Dodoma, Alhaji. Jabir Shekimweri wakati wa mkutano wa kwanza wa Baraza la Madiwani wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma uliofanyika katika ukumbi wa halmashauri. Alisema kuwa anawataka madiwani kuimarisha uwazi na uwajibikaji katika utendaji wao, kusikiliza kero za wananchi na kuhakikisha kuwa mipango ya maendeleo inalenga kuleta manufaa kwa jamii nzima. “Dodoma kama makao makuu ya nchi inahitaji uongozi thabiti, wa mfano na wenye matokeo. Ni wajibu wenu kuhakikisha jiji linaendelea kuwa kioo cha maendeleo kwa taifa hasa kwa kuibua miradi yenye tija kwa wananchi na kuwapa kipaumbele zaidi wananchi kwa kusikiliza kero zao” alisema Shekimweri. Aidha, alisisitiza umuhimu wa madiwani kushirikiana na watendaji wa halmashauri katika kutekeleza miradi ya maendeleo, kuboresh...

Kihaga: Fanyeni matangazo ili kuwafikia wananchi wa maeneo mbalimbali

Image
Na. Mwandishi Wetu, Dodoma Maafisa Maendeleo ya Jamii kutoka Halmashauri ya Jiji la Dodoma wametakiwa kuongeza juhudi katika kutoa elimu kwa wananchi kuhusu fursa z a mikopo isiyokuwa na riba inayotolewa na h almashauri ili kuhakikisha wananchi wanaifahamu na kunufaika nayo. Hayo aliyasema Mkurugenzi Idara ya Serikali za Mitaa, Angelista Kihaga, wakati akitoa semina kwa Maafisa Maendeleo ya Jamii kuhusu mikopo ya asilimia 10 inayotolewa na halmashauri katika ukumbi wa Dodoma Sekondari. Alisema kuwa kuna baadhi ya wananchi bado hawana uelewa wa kutosha kuhusu uwepo wa mikopo hiyo, jambo linalochangia kutokuitumia ipasavyo. “Ni muhimu maafisa Maendeleo ya Jamii m katoa elimu kwa ukaribu zaidi. Wananchi wengi bado hawana uelewa kuwa mikopo hii ipo na haina riba. Tukitoa elimu ya kutosha tutasaidia makundi mbalimbali hasa wanawake, vijana na watu wenye ulemavu kunufaika na fursa hii” alisema Kihaga. Aidha, alisisitiza umuhimu wa kutumia matangazo na vipindi mbalimbali kwenye vyomb...

Maafisa Maendeleo ya Jamii wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma wameshiriki kongamano la Maafisa Maendeleo ya Jamii Mkoa wa Dodoma kwa siku mbili likiwa na lengo la kukumbushana majukumu ya kazi, kupitia sera mpya zilizoandaliwa na Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum na kutoka na mpango kazi mpya wa kutekeleza katika maeneo yao ya kazi.

Image
  Maafisa Maendeleo ya Jamii wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma wameshiriki kongamano la Maafisa Maendeleo ya Jamii Mkoa wa Dodoma kwa siku mbili likiwa na lengo la kukumbushana majukumu ya kazi, kupitia sera mpya zilizoandaliwa na Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum na kutoka na mpango kazi mpya wa kutekeleza katika maeneo yao ya kazi.

Maafisa Mazingira Kanda Namba Sita waanza ziara ya kutoa elimu ya usafi wa mazingira sambamba na uhamasishaji wananchi kuchangia ada ya uzoaji taka.

Image
  Maafisa Mazingira Kanda Namba Sita waanza ziara ya kutoa elimu ya usafi wa mazingira sambamba na uhamasishaji wananchi kuchangia ada ya uzoaji taka. ‎ ‎Watumishi Kanda Namba Sita waanza mkakati wa kuhakikisha kata zinazounda kanda hiyo usafi wa mazingira unaimarika. ‎ ‎Akizungumza katika kikao kilichofanyika baina ya watumishi wa Kanda na viongozi wa Mtaa wa Mbwanga, Afisa Afya Kanda Namba Sita, Zainab Iddi alisema kuwa kuishi kwenye mazingira safi ni haki na wajibu wa kila mwananchi ‎ ‎Alisema kuwa usafi wa mazingira husaidia afya kuwa imara na salama. "Mtaa wa Mbwanga ni mojawapo wa mitaa ambayo tunataka wananchi waimarike katika suala la usafi wa mazingira. Katika suala la kiafya hairuhusiwi kutunza taka kwa mda mrefu au kuzichoma kwasababu kuna baadhi ya kemikali zinaweza kuleta madhara kwa binadamu" alisema Iddi ‎ ‎Aidha aliongeza kuwa wananchi wanatakiwa kufuata sheria na taratibu zilizowekwa na Serikali. ‎ ‎Akisoma sheria za usafi wa mazingira Afisa Mazingir...

Maafisa kutoka Kanda Namba Nne wakípima bango kwaajili ya kutathmini kodi ya bango kwa mujibu Sheria ndogo ya Ada na Ushuru wa Mabango na Matangazo ya Mwaka 2017.

Image
  Maafisa kutoka Kanda Namba Nne wakípima bango kwaajili ya kutathmini kodi ya bango kwa mujibu Sheria ndogo ya Ada na Ushuru wa Mabango na Matangazo ya Mwaka 2017. Sambamba na hilo wanaendelea kutoa elimu ya ulipaji kodi kwa wananchi wanaowatembelea ili kuhakikisha halmashauri inakusanya mapato stahiki

Timu ya Menejimenti ya Halmashauri ya Jiji la Dodoma imefanya ziara katika Kanda Namba Tatu ya kukagua miradi ya maendeleo.

Image
  Timu ya Menejimenti ya Halmashauri ya Jiji la Dodoma imefanya ziara katika Kanda Namba Tatu ya kukagua miradi ya maendeleo. Miradi iliyotembelewa ni Shule ya Msingi Mahungu na Kituo cha Afya Kizota.

Timu ya Menejimenti ya Halmashauri ya Jiji la Dodoma imefanya ziara ya kukagua miradi ya maendeleo Kanda Namba Mbili ambapo wakati wa ukaguzi walisisitiza ubora, thamani ya fedha na kasi ya utekelezaji kwa manufaa ya wananchi.

Image
  Timu ya Menejimenti ya Halmashauri ya Jiji la Dodoma imefanya ziara ya kukagua miradi ya maendeleo Kanda Namba Mbili ambapo wakati wa ukaguzi walisisitiza ubora, thamani ya fedha na kasi ya utekelezaji kwa manufaa ya wananchi.

Timu ya Menejimenti ya Halmashauri ya Jiji la Dodoma imefanya ziara katika Kanda Namba Moja kukagua miradi ya maendeleo. Mradi uliotembelewa ni Shule ya Msingi Kaloleni wenye thamani ya shilingi 151,000,000 ambapo mradi huo upo katika utekelezaji

Image
  Timu ya Menejimenti ya Halmashauri ya Jiji la Dodoma imefanya ziara katika Kanda Namba Moja kukagua miradi ya maendeleo. Mradi uliotembelewa ni Shule ya Msingi Kaloleni wenye thamani ya shilingi 151,000,000 ambapo mradi huo upo katika utekelezaji

Maafisa kutoka Kanda Namba Nne wamefanya ziara katika Migahawa mikubwa kwa lengo la kukagua Leseni za Biashara na pia ulipaji wa Kodi ya Huduma yaani Service Levy huku wakiendelea kutoa elimu juu ya umuhimu wa kulipa kodi kwa wakati

Image
  Maafisa kutoka Kanda Namba Nne wamefanya ziara katika Migahawa mikubwa kwa lengo la kukagua Leseni za Biashara na pia ulipaji wa Kodi ya Huduma yaani Service Levy huku wakiendelea kutoa elimu juu ya umuhimu wa kulipa kodi kwa wakati

"Lakini kwenye uwezeshaji Wananchi kiuchumi tunapoliangalia kundi la Maendeleo ya Jamii,tunaona kuwa ni watu ambao wanatakiwa kuona mabadiliko ya kijamii kwa ujumla ya kiuchumi yanatokea kutokana na kazi zao".

Image
  "Lakini kwenye uwezeshaji Wananchi kiuchumi tunapoliangalia kundi la Maendeleo ya Jamii,tunaona kuwa ni watu ambao wanatakiwa kuona mabadiliko ya kijamii kwa ujumla ya kiuchumi yanatokea kutokana na kazi zao". Ni maneno ya Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, Mhe. Rosemary Senyamule wakati akifungua kikao kazi cha siku 2 cha Maafisa Maendeleo ya jamii kutoka Halmashauri zote za Mkoa wa Dodoma.