Kanda Namba Mbili yang'ara kwa huduma bora kwa wateja
Na. Tutindaga Nkwindi DODOMA
Kanda Namba Mbili imeendelea kung’ara kwa kutoa huduma bora zenye tija kwa wananchi katika
maadhimisho ya Wiki ya Huduma kwa Mteja yanayoendelea katika ofisi ya kanda kwa
kushirikisha watumishi pamoja na wananchi kutoka maeneo mengi ya kata
zinazounda kanda hiyo.
Maadhimisho hayo ni ukumbusho wa kuimarisha mawasiliano kati ya watumishi na wananchi, sambamba na kujadili changamoto na mafanikio katika utoaji wa huduma kwa umma.
Kwa upande wake, Afisa Biashara wa Kanda Namba Mbili, Ruth Kingu alisema kuwa Wiki ya Huduma kwa Mteja ni fursa muhimu ya kupokea mrejesho kutoka kwa wananchi na kuboresha zaidi mifumo ya utoaji huduma. “Tunajifunza mengi kupitia maoni ya wateja. Lengo letu ni kuhakikisha kila mwananchi anapata huduma bora, haraka na kwa ufanisi” alisema Kingu.
Katika hatua nyingine, mkazi wa Kata ya Iyumbu, Lucas Moses alieleza kuwa mfumo wa utoaji huduma kupitia kanda umeboresha upatikanaji wa huduma kwa wananchi, kwasababu wanahudumiwa karibu na makazi yao jambo lililopunguza muda na gharama. “Kupitia mfumo wa kanda, tunapata huduma karibu na haraka zaidi. Tunashauri maboresho zaidi kwenye miundombinu” alisema Moses.
Comments
Post a Comment