Kanda Namba Mbili yaendelea kutoa huduma bora kwa wananchi

Na. Tutindaga Nkwindi, NZUGUNI

Kanda Namba Mbili inayohudumia kata tano za Nzuguni, Ipagala, Ihumwa, Mtumba na Kikombo imeendelea kutoa huduma bora kwa wananchi, ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kuhakikisha kila mkazi wa kanda hiyo anapata huduma kwa wakati na kwa kiwango kinachostahili.


Akizungumza na waandishi wa habari Meneja wa Kanda hiyo, Abeid Msangi alisema kuwa kanda imejipanga vizuri katika kusimamia utoaji wa huduma kwa kuzingatia maadili ya utumishi wa umma, ubunifu na uwajibikaji.

Tunaendelea kuhakikisha wananchi wanapata huduma kwa haraka na kwa ubora. Tumeweka mifumo ya ufuatiliaji wa maombi ya wananchi na kuboresha mawasiliano kati ya ofisi na jamii ili kuongeza ufanisi alisema Msangi.

Aidha, alieleza kuwa maafisa walioko katika kanda hiyo wamekuwa wakipatiwa mafunzo ya mara kwa mara kuhusu utoaji wa huduma kwa wateja na matumizi ya teknolojia katika kushughulikia maombi ya wananchi, hatua ambayo imepunguza changamoto za ucheleweshaji wa huduma.



Vilevile, alisisitiza kuwa ubunifu na uwajibikaji ndiyo nguzo kuu zinazoiongoza kanda hiyo katika kutoa huduma bora, huku akiwataka watumishi kuendelea kujituma kwa bidii ili kufikia matarajio ya wananchi.

Kwa upande wake Anna James, mkazi wa Kata ya Ipagala aliipongeza Kanda Namba Mbili kwa huduma zake bora na upokeaji mzuri kwa wananchi wanaofika kupata huduma.

Nimekuwa nikifika ofisini mara kadhaa, na kwa kweli huduma zimeboreshwa sana. Watumishi wanatupokea vizuri, wanatoa maelezo kwa heshima na wanashughulikia changamoto zetu kwa wakati alisema James.

Kanda Namba Mbili imeendelea kuwa mfano wa kuigwa katika utoaji wa huduma bora kwa wananchi, ikiakisi dhamira ya Halmashauri ya Jiji la Dodoma ya kujenga utamaduni wa uwajibikaji, ubunifu na huduma zenye ubora kwa jamii.

Comments

Popular Posts

Agenda ya Lishe yaongeza Ari ya usomaji S/M Dodoma Makulu

Miaka minne ya Dkt. Samia, Kizota yanufaika mikopo ya asilimia 10

Halmashauri ya Jiji la Dodoma Kuhudumia Majimbo Mawili ya Uchaguzi