Huduma bora ni msingi wa kazi Kanda Namba Tatu

Na. Mwandishi Wetu, KIZOTA

Kanda Namba Tatu yaonesha kiwango bora cha huduma kwa wateja kwa kuendelea kufanya vizuri katika kutoa huduma zinazogusa matarajio ya wananchi wakati wa maadhimisho ya Wiki ya Huduma kwa Mteja.


Kauli hiyo ilitolewa na Meneja wa Kanda Namba Tatu ya utoaji huduma katika Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Fanuel Lawrence alipokuwa akiongelea Wiki ya Huduma kwa Mteja katika kanda hiyo. Alisema kuwa huduma bora ni wajibu wa kila mtumishi wa umma na njia ya kuj

enga imani na uaminifu wa wananchi kwa serikali yao. “Huduma bora ni msingi wa kazi yetu, tunapaswa kuwa na mbinu mpya, kuwa na adabu, na kujitolea ili wananchi wapate huduma stahiki” alisema Lawrence. Aidha, aliwakaribisha wananchi na wafanyabiashara katika ofisi ya Kanda Namba Tatu zilizopo katika pamoja na Ofisi ya Afisa Mtendaji Kata ya Kizota kupata huduma zote muhimu. Aliongeza kuwa ofisi hizo zimesogezwa karibu na wananchi ili kuwapunguzia kero ya kufuata huduma mbali na makazi na shughuli zao.

Nae, Afisa Biashara wa Kanda Namba Tatu, Steven Maufi alibainisha kuwa Wiki ya Huduma kwa Mteja ni fursa ya kuhudumia wananchi kwa namna ya tofauti ili kupata maoni na ushauri kutoka kwao ya namna ya kuboresha huduma zaidi. “Mbinu zetu za kutoa huduma bora za kiwango cha juu zinategemea pia maoni ya wateja. Lengo kuu ni kuhakikisha wananchi wanapata huduma bora na kwa haraka na serikali inapata kile kinacjostahili kwa wakati” alisema.

Kwa upande wake, Mfanyabiashara kutoka Kata ya Nala, Salehe Hamisi alitoa pongezi kwa kanda hiyo kutoa huduma nzuri. “Mabadiliko ni makubwa sana, sasa hivi ndugu mwandishi, tunahudumiwa vizuri sana. Hata lugha wanayotumia ni nzuri tofauti na kipindi cha nyuma, unamkuta mtumishi kwenye meza ya huduma, anakuhudumia kama ni vita. Sasa hivi wanatupokea vizuri na wanahakikisha unaondoka umepata kile umekifuata na ukiwa umeridhika” alisema.

Maadhimisho ya Wiki ya Huduma kwa Mteja yanayofikia kilele tarehe 10 Oktoba, 2025 yakilenga kuimarisha uhusiano mzuri kati ya taasisi na wanufaika wa huduma.

Comments

Popular Posts

Kanda Namba Mbili yaendelea kutoa huduma bora kwa wananchi

Kanda Namba Mbili yang'ara kwa huduma bora kwa wateja

JIJI LA DODOMA KUPELEKA MIL 50 ZAHANATI YA KIKUYU