Mbunge Mavunde akabidhi Kompyuta kwa Kata 41 za Jiji la Dodoma
Na. Nancy Kivuyo, VIWANDANI
Watendaji
wa Kata 41 za Halmashauri ya Jiji la Dodoma wapokea Kompyuta na Printa kwa
ajili ya kurahisisha na kuboresha utendaji kazi wenye ufanisi za kuwahudumia
wananchi.
Vifaa hivyo, viligawiwa katika hafla ya Ugawaji Kompyuta na Printa kwa Shule za Sekondari za Serikali na Watendaji wa Kata jijini Dodoma, iliyofanyika katika Shule ya Sekondari Viwandani.
Nae, Afisa Mtendaji wa Kata ya Hazina, Tunu Mahmoud, alisema kuwa ameguswa na tukio la kipekee la mbunge kuwapa kompyuta za kisasa kwa kwaajili ya utendaji kazi unaoendana na ukuaji wa teknolojia. “Mimi kama mkazi wa Dodoma, suala la elimu lilikuwa nyuma lakini kwa mbunge wetu na waziri, ameona kipaumbele chake ni elimu. Hivyo, nimefarijika na nafurahi sana kwasababu tunaona mabadiliko makubwa katika sekta ya elimu kwa mchango wake” alisema Mahmoud.
MWISHO
Comments
Post a Comment