WILAYA YA DODOMA IMEPANDA MITI 4,500,000 KAMPENI YA KIJANISHA DODOMA
Na. Dennis Gondwe, DODOMA
WILAYA Dodoma imefanikiwa kupanda miti 4,500,000
katika kampeni ya Dodoma ya kijani na utekelezaji wa ujumbe wa mbio za Mwenge
wa Uhuru mwaka 2023 unaosisitiza utunzaji wa Mazingira.
![]() |
Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru 2023 Abdalla Shaib Kaim akipanda mti kwenye mradi wa Maji safi nzuguni |
Akisoma risala ya utii kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano
wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan wakati wa mbio za Mwenge wa Uhuru Wilaya
ya Dodoma katika uwanja wa Shule ya Msingi Chamwino, Katibu Tawala Wilaya ya
Dodoma, Sakina Mbugi alisema kuwa Wilaya ya Dodoma ipo mstari wa mbele katika kutunza Mazingira. “Katika kutekeleza ujumbe wa Mwenge wa Uhuru wilaya imekuwa ikifanya jitihada mbalimbali katika
utunzaji wa Mazingira na kuokoa vyanzo vya Maji kwa ustawi wa viumbe hai na
uchumi wa Taifa. Katika kipindi cha miaka mitano ya Kampeni ya Dodoma ya Kijani Miti 4,500,000 imepandwa
katika maeneo mbalimbali pamoja na chanzo cha Maji Mzakwe. Aidha, wilaya imeweza kusambaza vifaa vya kuhifadhia taka
80 katika barabara na mitaa” alisema Mbugi.
Akiongelea
utekelezaji wa agizo la serikali la kupanda miti 1,500,000 alisema asilimia 81 ya
miti imepandwa. “Mheshimiwa Rais; Wilaya
ya Dodoma katika utekelezaji wa agizo
la serikali la kupanda miti 1,500,000
imefanikiwa kupanda miti 1,224,459 sawa na asilimia
81.6 kwa kushirikiana na
Halmashauri ya Jiji, Mfuko wa Misitu Tanzania, Wadau binafsi na Wakala wa
Huduma za Misitu Tanzania” alisema Mbugi.
Akiongelea
uzalishaji taka alisema kuwa Wilaya ya Dodoma inakadiriwa kuzalisha tani 391 za taka
ngumu kwa siku. “Kata za nje ya mji huzalisha tani 115 na kata za mjini huzalisha tani 276. Tani 180- 200
zinaondoshwa kwa siku sawa na asilimia 51.2. Wastani wa taka za plastiki tani tano hukusanywa
na kurejereshwa kwa siku kupitia vituo vidogo vya ukusanyaji na uchakataji wa
taka za plastiki. Wilaya ya Dodoma imeendelea kuhifadhi, kulinda na kuhamasisha
matumizi endelevu ya misitu na kufanya doria za mara kwa mara. Elimu juu ya
uhifadhi wa misitu na nishati mbadala inatolewa kwa wananchi” alisema Mbugi.
Mwenge
wa Uhuru mwaka 2023 unaongozwa na kaulimbiu isemayo “Tunza Mazingira, Okoa
vyanzo vya Maji kwa ustawi wa Viumbe Hai kwa Uchumi wa Taifa”
MWISHO
Comments
Post a Comment