Wafanyabiashara wa Soko Kuu la Majengo Dodoma watarajia makubwa Mradi wa TACTIC
Na. Halima Majidi, DODOMA
Wafanyabiashara wa Soko Kuu la Majengo
Jiji la Dodoma, wameishukuru serikali
kwa kuona umuhimu wa kukarabati miundombinu ya Soko hilo na kuomba kuharakishwa uboreshaji wa soko ili waweze
kuendelea na majukumu yao, kwa sababu
soko hilo ndio soko mama la chakula.
Akizungumza katika hafla ya Utiaji Saini
Mikataba ya Ujenzi wa Miradi ya TACTIC uliofanyika katika Bustani ya Chinangali
Park, Mfanyabiashara wa Soko Kuu la Majengo, Rhoda Boyi, alipongeza juhudi
za Halmashauri ya Jiji la Dodoma kwa
kuwashirikisha katika hatua zote za
mradi "Tunatarajia kuwa sauti zetu zitasikilizwa na kuzingatiwa ili
kuhakikisha kuwa maboresho haya yanakidhi mahitaji yetu na kuboresha mazingira
ya biashara" alisema Boyi.
Kwa upande wake Mohammedi,
alifafanua changamoto watakazokumbana nazo katika kipindi chote cha ukarabati wa jengo
hilo, ni pamoja na; kupoteza wateja, kuharibika kwa bidhaa kutokana na kuhamishwa katika sehemu zao za biashara pamoja na
upungufu wa chakula kwasababu Majengo ni Soko linalotumika kama ghala kubwa
la chakula Dodoma" watu walikuwa
wanaweka "stock" watu walikuwa wanaleta bidhaa kwa wingi hivyo watapunguza,
mteja amezoea akitoka Chaduru, UDOM na Mipango anaenda moja kwa moja Majengo hivyo, kuhama sehemu moja kwenda nyingine kunatuathiri
sana " alisema Mohammed.
Nae, Kaimu Katibu wa Soko Kuu la Majengo,
Emanuel Samwel, alisema kuwa wapo tayari na
wamepokea maboresho ya Soko hilo,
na wameomba serikali kutoenda kinyume na makubaliano ya
kwenye vikao mbalimbali vilivyokuwa
vikiendelea.
Hata hivyo, Samwel alisema kuwa Soko la
Majengo limejengwa mwaka 1993 nakuanza kutumika mwaka 1996 likiwa na
wafanyabiashara 400, hivyo ni uhakika kuwa miundombinu ya Soko kwa sasa
imechakaa, kupitia mkataba huu utaenda kuleta mabadiliko makubwa, "soko
letu sisi ni soko mama, lina muda mrefi na kwa sasa lina watu 3200 -4000. Hivyo, ukiangalia idadi
na muda soko lilipoanzishwa kiuhalisia tunashukuru serikali kwa kuona ukarabati
huo" alisema Samwel.
Sambamba na hayo, uongozi huo uliahidi kutunza miundombinu ya
Soko hilo pindi tu utakapokamilika kwa kuhakikisha wanawaelimisha
wafanyabiashara wenzao kuhusu utunzaji wa miundombinu na kuimarisha usafi wa
mazingira ya soko kwa ujumla kwa lengo la kuendelea kulipa thamani na hadhi
Soko Kuu la Majengo.
Kwa upande wake Waziri wa Nchi, Ofisi ya
Rais – Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa, (TAMISEMI) Mohamed Mchengerwa
(Mb), aliwahakikishia wafanyabiashara na wananchi kwa ujumla kuwa serikali
imejipanga kuhakikisha miradi inatekelezwa kwa ufanisi na kwa wakati.
"Tunaelewa changamoto mnazokabiliana nazo, na kupitia mradi huu, tunalenga
kuboresha mazingira ya wafanyabiashara wanaojihusisha na shughuli mbalimbali
ili kuinua uchumi wa nchi kwa ujumla "alisema Mchengerwa.
Mchengerwa aliwataka viongozi wa ngazi zote wakiwemo Wakurugenzi, Wakala wa Barabara Mijini na
Vijijini( TARURA) na Tawala za mikoa na
Serikali za Mitaa (TAMISEMI) kusimamia kwa weledi utekelezaji wa miradi hiyo
kwa sababu imegharimu kiasi kikubwa cha
fedha na pia imewalenga Watanzani "miradi hii
inathamani kubwa, thamani ya miradi ni
zaidi ya tirioni 1.1, ambapo mradi huu
unaenda kuboresha miundombinu ya miji 45, niwaombe kwa pamoja muende mkasimamie
miradi hii ambayo Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu
Hassan amewakusudia watanzania"
alisema Mchengerwa.
Mradi wa uboreshaji wa Soko Kuu la Majengo
unajumla ya Mita za mraba 9,273, ambapo utajumuisha maboresho ya mpangilio,
mfumo wa umeme, mfumo wa maji na mzunguko wa hewa, wenye jumla ya makusanyo ya
mapato milioni 204.7 na unatarajiwa kukamilika ndani ya miezi 12.
MWISHO
Comments
Post a Comment