CCM yawataka wanachama kushiriki uchaguzi ujao

Na. Valeria Adam, DODOMA

Kuelekea katika uchaguzi wa serikali za mitaa mwaka 2024 Mlezi wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Mkoa wa Dodoma, Dkt. Philip Mpango amehizima wanachama wa CCM kujitokeza kwa wingi na kushiriki ili kuhakikisha ushindi katika chama chao.




Kauli hiyo aliitoa katika hafla ya kumpokea iliyoandaliwa na Chama Cha Mapinduzi na kufanyika katika ukumbi wa mikutano wa Jakaya Kikwete jijini Dodoma.

Dkt. Mpango ambae ni Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, alisema kuwa ni muhimu kwa wanachama wa CCM kujitokeza na kujiandikisha kwenye daftari la kudumu la wapiga kura. Uchaguzi ni muhimu na lazima kwa kila mwananchi kushiriki aliongeza kuwa utekelezaji wa Ilani ya Uchaguzi ya CCM ni jambo la msingi kwa mafanikio ya watanzania na chama hicho, aliongeza.

“Tarehe 27 Novemba, mwaka huu tutafanya uchaguzi wa serikali za mitaa na mwaka ujao tutafanya uchaguzi mkuu. Ili kukipa chama chetu ushindi katika chaguzi hizi ni lazima tujipange ili kuhakikisha tunapata ushindi kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, wabunge, madiwani na viongozi wote katika ngazi za serikali za mitaa.

Lakini pia kwa kutekeleza ipasavyo Ilani ya Uchaguzi ya CCM ya mwaka 2020 na kutoa hamasa ya kutosha kwa wanachama wenzetu ili wajitokeze kujiandikisha kwenye daftari la kudumu la wapiga kura na kushiriki michakato yote ya taifa. Haitoshi tu kujiandikisha ni lazima kushiriki uchaguzi” alisema Dkt. Mpango.

Katika kuimarisha uchumi wa CCM, alihimiza kwa viongozi wa chama kuwa waadilifu katika kusimamia miradi na mapato ya chama. “Viongozi msimamie miradi na mapato ya chama kwa uadilifu pamoja na kuhakikisha mali zote za CCM zinatumika kwa manufaa ya chama ili kuimalisha uchumi wa chama chetu na kuepuka kuathiri uendeshaji wa shughuli za chama” alisema Dkt. Mpango.

MWISHO

Comments

Popular Posts

Wananchi Makutupora wafunguka changamoto ya Maji, Umeme na Shule kwa Mkuu wa Mkoa

Waziri Mchengerwa apongeza usimamizi wa miradi jijini Dodoma

Mkataba ujenzi Uwanja wa Mpira wa Miguu wasainiwa Dodoma