Diwani Fundikila awataka wananchi kuendeleza amani kuelekea Uchaguzi wa Serikali za Mitaa

Na. Emmanuel Lucas, CHANG’OMBE

Diwani wa Kata ya Chang`ombe, Bakari Fundikira amewataka wananchi kuendelea kutunza amani, upendo na mshikamano hasa katika kipindi hiki kuelekea uchaguzi wa Serikali za mitaa 2024 Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) Mohammed Mchengerwa kutoa tamko la uchaguzi wa serikali za mitaa.


Diwani wa Kata ya Chang`ombe, Bakari Fundikira akisisitiza jambo


Kauli hiyo aliitoa kwa waandishi wa Habari baada ya kikao na viongozi wa Soko la Mavunde kilichofanyika katika ukumbi wa mikutano wa Ofisi ya Kata ya Chang'ombe iliyopo Halmashauri ya Jiji la Dodoma.

Diwani Fundikira alisema “kuelekea uchaguzi wa serikali za mitaa, Waziri mwenye dhamana Mheshimiwa Mohammed Mchengerwa ameshatoa tarehe ya uchaguzi ambayo itakuwa tarehe 27 Novemba, 2024. Rai yangu kwa wananchi wa Kata ya Chang`ombe na wananchi wengine, itakapofika wakati wa uandaaji wa daftari la wapiga kura cha kwanza tujitokeze wananchi wote wenye sifa tujiandikishe ili tuwe na sifa ya kuchagua na kuchaguliwa”.

 

“Kimsingi kwenye suala la ulinzi katika uchaguzi wa serikali za mitaa, sisi katika kata kutakuwa na ulinzi na usalama wa kutosha kwasababu kuna Polisi Kata, tunakamati ya ulinzi ya kata lakini pia tunazidi kutoa elimu kwenye ngazi za mitaa kuhusiana na suala la kutunza amani, upendo na mshikamano” aliongeza Fundikira.

MWISHO

Comments

Popular Posts

Wananchi Makutupora wafunguka changamoto ya Maji, Umeme na Shule kwa Mkuu wa Mkoa

Waziri Mchengerwa apongeza usimamizi wa miradi jijini Dodoma

Mkataba ujenzi Uwanja wa Mpira wa Miguu wasainiwa Dodoma