Afisa Elimu Jiji la Dodoma anunua jina la Rais Samia kwa Laki 5

Na. Dennis Gondwe, MIYUJI

MKUU wa Divisheni ya Elimu Sekondari Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Zainab Abdallah amefurahishwa na uwezo wa mwanafunzi mwenye mahitaji maalum, Angel Elias alipoandika jina la Rais, Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kutumia mdomo wake na kununua jina hilo kwa shilingi 500,000.

Mwanafunzi Angel Elias wa shule ya Msingi Hombolo Bwawani anayeandika kwa kutumia mdomo


Furaha hiyo aliionesha katika kikao cha wadau wa elimu wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma kilichoambatana na utoaji tuzo za kitaaluma na kufanyika katika Shule ya Msingi St. Gasper iliyopo Miyuji jijini hapa.

“Mheshimiwa Mwenyekiti kabla ya yote, ninaomba kwa ridhaa yako kama hautajari, hilo neno lililoandikwa na mtoto wangu Angel ‘I am so excited’. Nitalinunua kwa shilingi 500,000. Mheshimiwa Mkuu wa Wilaya ya Dodoma ni ukweli kwamba hata wale wanafunzi wasio na mahitaji maalum tunaowafundisha hawajifunzi haraka kama huyu anavyo fanya” alisisitiza Mwl. Abdallah.

Akiunga mkono tukio hilo, Mkuu wa Divisheni ya Elimu ya Awali na Msingi Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Mwl. Prisca Myalla alichangia shilingi 500,000. “Mheshimiwa Mwenyekiti tunakwenda sambamba katika kuinua elimu kwa watoto wetu wenye mahitaji maalum katika Halmashauri ya Jiji la Dodoma” alisema Mwl. Myalla.

Wachangiaji wengine katika kuunga mkono juhudi ni Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Dodoma iliyoahidi kuchangia shilingi 500,000 na Afisa Elimu Taaluma kutoka Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Dodoma aliahidi kuchangia shilingi 200,000.

Kwa upande wake, Mwl. Sarah Kapyela alimshukuru Mungu kwa kuwawezesha wadau kusogeza mbele gurudumu la elimu kwa mazingira yaliyopo katika kufundisha watoto wenye mahitaji maalum. “Watoto hawa tunawapa uangalifu sana kutokana na hali zao. Mfano huyu mtoto (Angel) kuna kitanda chake na godoro lake maalum, tunamuweka pale mbele anakuwa anaandika na tunamuelekeza ni namna gani aweze kumudu masomo yake. Tunachomshukuru Mungu zaidi huyu mtoto yupo darasa la tano amefaulu mtihani wake wa mwaka jana kuingia darasa la tano kwa kupata wastani daraja ‘B’, tunamshukuru Mungu, na wadau wetu wa elimu na serikali yetu kutusaidia kuinua hii elimu na kutupatia vifaa mbalimbali Mungu azidi kuwaongezea na kuwatia nguvu pale mnapotoa” alisema Mwl. Kapyela.

Alisema kuwa watoto wenye mahitaji maalum wanabidii sana darasani. “Hata wale wazazi wanaowaficha watoto wao wenye ulemavu tunawaomba wawalete watoto kwenye hiki kituo ambacho serikali imekitenga kwa ajili ya kuwahudumia. Na sisi tupo tunajitoa kwa moyo zaidi kuweza kutekeleza hili jukumu Mungu aendelee kuwatia nguvu nasisi kutukumbuka” alisema Mwl. Kapyela.

Mwl. Sarah Kapyela akuelezea umahili wa mwanafunzi Angel Elias darasani 

Mkuu wa Divisheni ya Elimu Sekondari Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Zainab Abdallah


MWISHO

Comments

Popular Posts

Wananchi Makutupora wafunguka changamoto ya Maji, Umeme na Shule kwa Mkuu wa Mkoa

Waziri Mchengerwa apongeza usimamizi wa miradi jijini Dodoma

Mkataba ujenzi Uwanja wa Mpira wa Miguu wasainiwa Dodoma