Wanafuzi Dodoma Sec watakiwa kusoma kwa bidii

Na. Dennis Gondwe, DODOMA

WANAFUNZI wa Shule ya Sekondari Dodoma wametakiwa kusoma kwa bidii na kutumia mfumo wa teknolojia ya ufundishaji mubashara kwa manufaa yao na vizazi vijavyo.

Mkurugenzi wa Idara ya Elimu Msingi na Maandalizi kutoka Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Zanzibar, Fatma Ramadhani alipokuwa akiongea na wanafunzi wa Shule ya Sekondari Dodoma


Kauli hiyo ilitolewa na Mkurugenzi wa Idara ya Elimu Msingi na Maandalizi kutoka Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Zanzibar, Fatma Ramadhani alipokuwa akiongea na wanafunzi wa Shule ya Sekondari Dodoma walipotembelea shule hiyo kwa ajili kujifunza juu ya mfumo wa ufundishaji mubashara unavyofanya kazi.

Ramadhani alisema kuwa mfumo wa ufundishaji mubashara unawarahisishia walimu kufundisha kwa wepesi na wanafunzi kuelewa zaidi kwa sababu wanakuwa wakisikiliza na kuona. “Hivyo, ni jukumu lenu sasa wanafunzi kuweza kuhakikisha mnaitumia vizuri teknolojia hii si kwa maisha yenu pekee, bali kwa vizazi vijavyo. Kwasababu leo ni mwanafunzi lakini ni dada kwenye familia, baadae utabadilika utakuwa mama kwenye familia yako na pia mtendaji kazi katika jamii yako. Kwa hiyo, jamii inakusubiri ukaitumikie. Je, utaweza kuitumikia kama haukuelimika? Ili uelimike lazima ufuatilie haya unayofundishwa kwa makini” alisema Ramadhani.

Wakati huohuo, Mkurugenzi wa Idara ya Sekondari Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Zanzibar, Asya Issa alisema kuwa serikali inawekeza ili wanafunzi waweze kutimiza ndoto zao katika masomo. “Kwa niaba ya wenzangu kwenye msafara wetu, tunapenda kuwashukuru uongozi wa Sule ya Sekondari Dodoma kwa mapokezi na kazi nzuri mnayoifanya. Kwa wanafunzi, wanafunzi mnaona serikali inavyohangaika na walimu wanavyohangaika kwa ajili yenu ili msome vizuri na kufikia ndoto zenu. Hakikisheni mnatendea haki juhudi hizi kwa kusoma kwa bidii na kufikia malengo yanayotarajiwa na serikali na malengo yenu binafsi” alisema Issa.

Mkurugenzi wa Idara ya Sekondari Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Zanzibar, Asya Issa akitoa neno


Shule ya Sekondari Dodoma ni moja ya vituo vilivyochaguliwa na kufungwa mfumo unaowezesha ufundishaji mubashara ambao mwalimu anaweza kuwa shuleni hapo akafundisha wanafunzi wa shule nyingine wakimuona na kuweza kuuliza maswali na kujibiwa.




MWISHO

 

 

Comments

Popular Posts

Wananchi Makutupora wafunguka changamoto ya Maji, Umeme na Shule kwa Mkuu wa Mkoa

Waziri Mchengerwa apongeza usimamizi wa miradi jijini Dodoma

Mkataba ujenzi Uwanja wa Mpira wa Miguu wasainiwa Dodoma