Mwenge wa Uhuru 2024 waweka jiwe la msingi Kituo cha vyombo vya habari cha Dodoma Media Group

 Na. Dennis Gondwe, MIYUJI

KIONGOZI wa mbio za Mwenge wa Uhuru kitaifa mwaka 2024 Godfrey Mnzava ameweka jiwe la msingi na kupongeza uwekezaji uliofanywa na Dodoma Media Group baada ya kutembelea na kukagua kituo cha vyombo vya habari cha Dodoma Media Group kilichojengwa eneo la Miyuji.

Kiongozi wa mbio za Mwenge wa Uhuru kitaifa mwaka 2024 Godfrey Mnzava baada ya kuweka jiwe la msingi kituo cha vyombo vya habari Dodoma Media Group


Mnzava baada ya kutembelea, kukagua na kujiridhisha na uwekezaji huo alipongeza na kusema kuwa ni uwekezaji mkubwa na mzuri. Alisema kuwa serikali ya awamu ya sita inayoongozwa na Rais, Dkt. Samia Suluhu Hassan imeweka mazingira mazuri kwa uwekezaji wa sekta binafsi nchini. Mazingira ya ufanyaji kazi kwa vyombo binafsi vya habari yameboreshwa katika kipindi chake, aliongeza. Aidha, aliweka jiwe la msingi mradi wa kituo cha vyombo vya Habari cha Dodoma Media Group.

Akiongelea gharama za mradi huo, meneja mkuu, Zania Miraji alisema kuwa hadi kukamilika utagharimu shilingi 1,000,000,000. Alisema kuwa hatua iliyofikiwa kiasi cha shilingi 700,000,000 kimetumika sawa na asilimia 70, akivitaja vyanzo vya fedha kuwa ni matangazo ya biashara, mkopo na mapato binafsi ya mkurugenzi.

Mradi wa kituo cha vyombo vya habari cha Dodoma Media Group ulianza kutekelezwa tarehe 1 Oktoba, 2018 ukitarajiwa kukamilika tarehe 31 Desemba, 2024, ukihusisha ujenzi wa majengo ya studio za redio, televisheni, samani na mifumo ya umeme na maji.



MWISHO

Comments

Popular Posts

Wananchi Makutupora wafunguka changamoto ya Maji, Umeme na Shule kwa Mkuu wa Mkoa

Waziri Mchengerwa apongeza usimamizi wa miradi jijini Dodoma

Mkataba ujenzi Uwanja wa Mpira wa Miguu wasainiwa Dodoma