Mradi wa Maji ya Mvua uliofadhiliwa na TASAF wasaidia wanafunzi Shule ya Msingi Ipala

Na. Emanuel Charles, IPALA

 

Mwenyekiti wa Kamati ya TASAF Taifa, Peter Ilomo ameupongeza uongozi wa Kata ya Ipala kwa kuendelea kutunza miradi iliyofadhiliwa na Mfuko wa Maendeleo ya Jamii (TASAF) ukiwemo mradi wa ukusanyaji maji ya mvua unaopatikana katika Shule ya Sekondari Ipala wenye lengo la kuondoa adha ya upatikanaji wa maji kwa wanafunzi shuleni hapo.

 



Akizungumza katika ziara ya kukagua miradi iliyotekelezwa na TASAF, Ilomo alisema kuwa lengo la kwenda kukagua mradi huo ni kuangalia kama unafanya kazi na kusaidia wanafunzi kama ilivyokusudiwa. “Tunashukuru mradi ulianza 2022 na kumalizika 2023, kwakuwa tayari mradi umeshakamilika na jamii inayozunguka mradi huu kwa maana ya wanafunzi na waalimu wananufaika tunasema asante sana. Lengo lakuja hapa ni kukagua kama mradi unafanya kazi kwasababu mara nyingi miradi unaweza kukamilika lakini usifanye kazi, nipongeze uongozi wa hapa Ipala, ninyi mmekuwa wa tofauti” alisema Ilomo.

 

Pia aliongeza kwa kusema kuwa uongozi wa Kata ya Ipala unapaswa kuendelea kufuatilia kwa ukaribu changamoto za wanufaika wa TASAF na kuwasaidia kutatua changamoto zao. “Kama kuna mnufaika ana changamoto awasilishe ili aweze kutatuliwa. Lakini pia viongozi fuatilieni kwa makini kwasababu kuna baadhi ya wazee hawasemi. Tumebakiza miezi tisa ili kumaliza mwaka, miezi hii si mingi. Hivyo, basi fedha mtakazo zipata katika kipindi hiki cha miezi tisa zitumike vizuri” aliongeza Ilomo.

 

Nae mmoja wa wanufaika wa TASAF, Christina Fande aliipongeza Serikali ya Jamhuri ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania inayoongozwa na Rais, Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuleta mpango huo kwasababu umeweza kumsaidia kununua ng’ombe wa kulimia, jembe la kulimia pamoja na ujenzi wa nyumba ya kuishi. “Katika mpango huu wa kunusuru watu masikini nilianza kupokea shilingi 40,000 ambayo nilikuwa naiwekeza sehemu na baadae nikaweza kununua ng’ombe wa kulima, jembe la kulimia pamoja na ujenzi wa nyumba yenye vyumba vitatu na sebule. Nawaasa wenzangu ambao ni wanufaika wa TASAF, watumie vizuri fedha wanazopata ili kuweza kufanya maendeleo” alisema Fande.







MWISHO

Comments

Popular Posts

Agenda ya Lishe yaongeza Ari ya usomaji S/M Dodoma Makulu

RC Senyamule azipongeza Club za Jogging Dodoma

Usafi wa Mazingira Kipaumbele Kata ya Chamwino