Shekimweri awaita mashabiki wa Dodoma Jiji FC, Ally Hassan Mwinyi

Na. Nancy Kivuyo, DODOMA

Mkuu wa Wilaya ya Dodoma, Jabir Shekimweri ameitakia kila la kheri timu ya Dodoma Jiji FC katika mchezo wao ujao dhidi ya Tabora United FC, utakaopigwa katika dimba la Ally Hassan Mwinyi mjini Tabora.


Mkuu wa Wilaya ya Dodoma, Jabir Shekimweri akielezea jambo


Alizungumza hayo wakati akitoa salamu katika Mkutano wa Baraza la Madiwani uliofanyika katika ukumbi wa mikutano wa halmashauri.

“Licha ya changamoto timu yetu iliyopitia, timu imeweza kufanya vizuri katika michezo miwili mtawalia. Timu hii ni fahari ya nchi ikiiwakilisha makao makuu ya nchi. Hivyo, tunawatakia kila la kheri katika mchezo wao dhidi ya Tabora United FC watakaocheza ijumaa. Tunawasisitiza wadau na wana Dodoma kwenda kuipa nguvu timu yetu ili matokeo yawe mazuri” alisema Shekimweri.

Naye, Elice Kitendya alisema “kwakua mimi ni mdau mkubwa wa timu yetu ya Dodoma Jiji, nina matumaini makubwa na timu yetu, mashabiki tunawahimiza wenye nafasi ya kwenda Tabora tujumuike pamoja kwenda kuisapoti timu yetu ili wapate morali ya kutosha. Niseme tu kwamba, ninaamini watafanya vizuri ili kuendeleza ushindi ambao tumeuanza”.

Timu ya Dodoma Jiji FC itaondoka kesho kuelekea mkoani Tabora kwaajili ya mechi yao dhidi ya Tabora United FC, mchezo utakaopigwa katika dimba la Ally Hassan Mwinyi siku ya Ijumaa majira ya saa nane mchana, katika mechi ya mzunguko wa kwanza Dodoma Jiji FC iliibuka kidedea kwa ushindi wa jumla ya mabao 3-0. Katika michezo mitatu ya mwisho ya ligi Dodoma Jiji FC imekusanya alama saba kibindoni.

MWISHO

Comments

Popular Posts

Mbunge Mavunde akabidhi Kompyuta kwa Kata 41 za Jiji la Dodoma

Wafanyabiashara wa Soko Kuu la Majengo Dodoma watarajia makubwa Mradi wa TACTIC

Mkataba ujenzi Uwanja wa Mpira wa Miguu wasainiwa Dodoma