Mkurugenzi wa Jiji awatakia Heri ya Mwaka Mpya 2025 Wafanyakazi

Na. Dennis Gondwe, DODOMA

MKURUGENZI wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Dkt. Frederick Sagamiko amewatakia heri ya mwaka mpya 2025 wafanyakazi wote katika Bonanza kubwa michezo katika uwanja wa Jamhuri Dodoma.



Akifungua bonanza hilo lililoandaliwa na Halmashauri ya Jiji la Dodoma kwa ajili ya kuwakutanisha wafanyakazi na kuuaga mwaka 2024 na kuukaribisha mwaka 2025, Mkurugenzi wa Jiji alisema kuwa michezo inalenga kuwakutanisha wafanyakazi na kuwakumbusha kuwa ni wamoja na wanatakiwa kufanya kazi kwa upendo na kushirikiana.

Akiongelea umuhimu wa michezo katika kujenga urafiki na umoja alisema kuwa hilo halina mjadala. “Karibu sana katika uwanja wa Jamhuri. Tumekutana hapa taasisi zaidi ya moja katika uwanja huu lakini wote lengo letu ni moja la michezo kwa afya zetu. Ushauri wangu Dodoma Jiji wenye ratiba wakutane na Ofisi ya Rais, Ikulu ‘kuharmonise’ ratiba ili tuona tutakavyoshirikiano pamoja. Heri ya Mwaka mpya 2025” alisema Dkt. Sagamiko.

Kwa upande wake Mwl. Sylvia Madeje kutoka shule ya Sekondari Chinangali alimpongeza mkurugenzi wa jiji na timu yake kwa kuandaa bonanza hilo kubwa la michezo kwa wafanyakazi. “Michezo inadumisha ushirikiano kwa wafanyakazi, kuongeza ufanisi kwa sababu pamoja na michezo tunabadilishana mawazo na kuimarisha ari ya utendaji wa kazi” alisema Madeje.




Bonanza kubwa la michezo la wafanyakazi wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma lilitanguliwa na mbio za polepole (jogging) zilizoanzia Ofisi kuu ya Jiji zikiongozwa na Mkurugenzi wa Jiji la Dodoma kuelekea uwanja wa michezo wa Jamhuri kuanzia saa 12.30 alfajiri.




=30=

Comments

Popular Posts

Wananchi Makutupora wafunguka changamoto ya Maji, Umeme na Shule kwa Mkuu wa Mkoa

Waziri Mchengerwa apongeza usimamizi wa miradi jijini Dodoma

Mkataba ujenzi Uwanja wa Mpira wa Miguu wasainiwa Dodoma