Kamba wanaume Ofisi ya Rais Ikulu yaiburuza kwa taabu Ofisi ya Rais Jiji la Dodoma

Na. Dennis Gondwe, DODOMA

Timu ya Kuvuta Kamba wanaume kutoka Ofisi ya Rais Ikulu imeiburuza kwa taabu sana Timu ya Kuvuta Kamba wanaume ya Ofisi ya Rais Jiji la Dodoma kwa mivuto miwili mtawalia katika Bonanza la michezo.




Katika mchezo uliochezwa kwenye Uwanja wa Jamhuri jijini hapa, timu zote zilionesha kukamiana kutokana na kuwa chini ya mwavuli mmoja ambao ni Ofisi ya Rais.

Aidha, mwamuzi wa mchezo huo alilazimika mara kadhaa kutumia filimbi yake kuzikumbusha timu zote mbili kanuni za mchezo huo wa kiuvuta kamba. Mchazo ulianza kwa nguvu na kila upande ulionesha unaweza ibuka mshindi.

Ofisi ya Rais Ikulu iliibuka kidedea kwa kuiburuza kwa taabu sana Ofisi ya Rais Jiji la Dodoma kwa mivuto miwili bila majibu.

Halmashauri ya Jiji la Dodoma iliandaa Bonanza la michezo mbalimbali la wafanyakazi kwa lengo la kuwakutanisha na kufurahia kuuaga mwaka 2024 na kuukaribisha mwaka 2025 katika Uwanja wa Jamhuri Dodoma.

MWISHO

Comments

Popular Posts

Wananchi Makutupora wafunguka changamoto ya Maji, Umeme na Shule kwa Mkuu wa Mkoa

Waziri Mchengerwa apongeza usimamizi wa miradi jijini Dodoma

Mkataba ujenzi Uwanja wa Mpira wa Miguu wasainiwa Dodoma