TAMISEMI yakusanya Shilingi Trilioni 1.11

OR-TAMISEMI

WAZIRI wa Nchi, Ofisi ya Rais-TAMISEMI, Mohamed Mchengerwa amesema hadi kufikia Machi, 2025 shilingi trilioni 1.11 zimekusanywa sawa na asilimia 93.15 ya lengo la kukusanya shilingi trilioni 1.60 kwa Mwaka 2024/25.


Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais-TAMISEMI, Mohamed Mchengerwa


Akiwasilisha bungeni makadirio ya mapato na matumizi ya Ofisi hiyo kwa Mwaka 2025/26, Waziri Mchengerwa alisema kuwa kati ya fedha hizo shilingi trilioni 61.21 ni kodi ya majengo, shilingi trilioni 1.04 ni mapato ya ndani ya mamlaka za serikali za mitaa.

Pia, alisema kuwa shilingi bilioni 16.23 ni mapato ya ndani ya taasisi na shilingi milioni 201.60 ni maduhuli ya mikoa.

Alifafanua kuwa makusanyo hayo yalitokana na ada za wanachuo, tozo, ukusanyaji wa madeni, mauzo ya bidhaa mbalimbali na ushuru unaotozwa na mamlaka za serikali za mitaa kulingana na Sheria ya Fedha za Serikali za Mitaa, Sura 290.

Mchengerwa alisema kuwa kwa kipindi hicho, TAMISEMI ilipanga kutumia shilingi bilioni 541.27 za mapato ya ndani ya halmashauri kwa ajili ya kuchangia utekelezaji wa shughuli za maendeleo. Hadi kufikia Machi, 2025 shilingi bilioni 312.30 sawa na asilimia 57.70 zilitolewa.

Alielezea kuwa baadhi ya miradi iliyotekelezwa kwa kipindi hicho ni ujenzi wa miundombinu ya elimu, afya, ujenzi wa barabara, machinjio, minada nyumba za walimu na watumishi wa afya, hospitali, vituo vya afya, zahanati, vituo vya polisi, ununuzi wa magreda.

Chanzo: www.tamisemi.go.tz

Comments

Popular Posts

Mfumo wa Ufuatiliaji na Tathmini ni nyenzo ya utendaji kazi serikalini – Dkt. Biteko

JIJI LA DODOMA KUPELEKA MIL 50 ZAHANATI YA KIKUYU

WENZA WA VIONGOZI WASHAURIWA KUANZISHA BUSTANI ZA NYUMBANI