Shule ya Sekondari Kikuyu yapongeza ajenda ya Lishe
Na. Abdul Juma, KIKUYU KASKAZINI
Halmashauri ya Jiji la Dodoma imekuwa mstari wa mbele
kuunga mkono juhudi za serikali za kuhakikisha chakula na lishe linapatikana
katika Shule ya Sekondari Kikuyu na kuwawezesha wanafunzi kusoma wakiwa
wameshiba.
Kauli hiyo ilitolewa na Mkuu wa Shule ya Sekondari Kikuyu, Mwl. Gasper Mmary alipokuwa akiongelea hali ya upatikanaji wa chakula na lishe shuleni hapo yakiwa ni mafanikio ya serikali kwa miaka minne ya serikali.
Alisema kuwa Halmashauri ya Jiji la
Dodoma imewezesha upatikanaji wa unga zaidi Kilogramu 650 ili kusaidia
wanafunzi waliopo shuleni hapo kupata chakula shuleni. “Tunaushukuru mpango huu
wa kuboresha chakula na lishe kwa wanafunzi wote wa shule za msingi na
sekondari. Katika mpango huu, halmashauri imetusaidia kupata unga zaidi ya Kilogramu
650 ili kuwezesha wanafunzi wote kupata chakula. Suala hili lina mchango mkubwa
katika kuwafanya wanafunzi kusoma kwa bidii ili kuweza kupata ufaulu mzuri
katika masomo yao” alisema Mwl. Mmary.
Aidha, Mwalimu wa Taaluma, Mwl. Mwajuma Kidela alipongeza
na kuishukuru serikali kwa kuwezesha suala la chakula na lishe kupatikana
shuleni hapo kwasababu limekuwa chachu ya wanafunzi kusoma kwa bidii. Alisema
kuwa chakula na lishe shuleni hapo imepunguza utoro wa wanafunzi kwa kiwango
kikubwa. “Tunaipongeza serikali yetu ya awamu ya sita inayoongozwa na Rais, Dkt.
Samia Suluhu Hassan kwa kutimiza suala la chakula na lishe shuleni kwasababu jambo
hilo katika shule yetu limetuletea manufaa makubwa kwa wanafunzi wetu. Mpango
huu umeongeza ufahulu wa hali ya juu ukilinganisha na hapo awali wanafunzi wetu
walipokuwa hawapati chakula shuleni” alisema Mwl. Kidela.
Nae mwanafunzi wa Kidato cha Nne, Ratifa Mohamed aliishukuru
serikali kwa kuwawezesha kupata chakula na lishe wanapokuwa shuleni kwa lengo
la kuongeza ufanisi katika masomo yao hasa yale ya jioni. “Tunaishukuru serikali
kwa kutuwezesha kupata chakula na lishe tunapokuwa shuleni. Suala hili
linatusaidia sisi wanafunzi kuwa na ufanisi katika masomo yetu ya jioni, tunakuwa
na nguvu ya kutosha katika kujisomea. Vilevile, kutoa mchango na ushirikiano
katika masuala mbalimbali yanayohusu taaluma, jambo linalosaida kufanya vizuri
katika masomo yetu" alishukuru Mohamed.
Chakula na lishe kwa wanafunzi wa shule za sekondari na
msingi ni chachu ya ufanisi na ufaulu jambo linaloboresha elimu katika Jiji la
Dodoma.
MWISHO
Comments
Post a Comment