Sepesha Rushwa, Acha Rushwa ya Ngono

Na. Coletha Charles, DODOMA

Mkuu wa Wilaya ya Kongwa, Mayeka Simion Mayeka ametoa wito kwa vijana wa Wilaya ya Dodoma kushiriki kikamilifu katika mapambano dhidi ya rushwa kwa kujihusisha na kampeni mbalimbali za kuleta tija na mabadiliko katika nchi kwa sababu ni nguzo ya taifa na mchango muhimu katika kufanikisha ndoto za maendeleo.

 





Mayeka alisema hayo wakati akisoma hotuba kwa niaba ya Mgeni Rasmi, Patrobas Katambi, Naibu Waziri, Ofisi ya Waziri Mkuu (Kazi, Vijana,  Ajira na wenye Ulemavu) kwenye kilele cha mbio ndefu na fupi za Taasisi ya Anti-Corruption Voices Foundation yenye kauli mbiu ya Badili tabia Shepesha Rushwa  katika shule ya msingi makole.

 

Alisema kuwa kupitia mbio hizo wamepeleka ujumbe kwa jamii kama nguzo ya maendeleo na kutoa pongezi kwa Ant-Corruption Voices Foundation kwa juhudi za kuimalisha maadili na uwajibikaji kwa sababu ni mfano bora kwa taasisi zisizo za kiserikali kwa kushirikiana na Serikali kuimalisha maendeleo ya jamii. “Mbio za Sepesha Rushwa Marathon ni mfano wa ubunifu na jinsi michezo inaweza kuwa jukwaa la kuhamasisha jamii kuhusu maadili, uwazi na uwajibikaji, tukio hili siyotu linanatufundisha umuhimu wa kuzingatia afya zetu, bali linatufundisha mshikamano wa kitaifa zidi ya changamoto zinazotukabili, mbio hizi zinaweza kuwa chachu ya mabadiliko chanya na kuibua mijadala mbalimbali muhimu kama mapambano zidi ya rushwa ya ngono na kuhamasisha uwajibikaji katika sekta zote za maisha” alisema Mayeka.

 

Mayeka aliongeza kwa kusema kuwa Tanzania imeshika nafasi ya Pili Ukanda wa Afrika Mashariki katika mapambano ya Rushwa ikitanguliwa na nchi ya Rwanda, “Ripoti mbalimbali zinaonyesha rushwa ya ngono ni changamoto kwa wanawake na vijana madhara ya rushwa ya ngono kazini ni pamoja na kutoa ajira  kwa wanawake, kupandishwa cheo, nyongeza za mishahara, kupewa siku za kupumzika na wanawake wengi wanafanya rushwa ya ngono kwa kutishiwa kupoteza kazi zao, madhara mengine ya rushwa ya ngono ni kuchochea maambukizi ya VVU na UKIMWI na inafanyika katika mazingira yasiyo salama na kuongeza magonjwa ya zinaa” alisema.

 


Naye, Mkuu wa Wilaya ya Dodoma, Alhaj Jabir Shekimweri alisema wananchi wanalo jukumu la kuzuia na kukemea rushwa ya ngono, mapambano zidi ya madawa ya kulevya Ukimwi na mmonyoko wa maadili kwa vitendo kulingana na maslahi ya Taifa na ukubwa wa tatizo hili katika jamii kuongezeka hasa kwa vijana na wanawake. “Viongozi Anti-Corruption Voices Foundation ninawahakikishia ushirikiano na ulezi, tumewapatia ofisi tunawawezesha kwa vitu mbalimbali, kadili tulivyo jaliwa na mwenyezi mungu tuendelee kuwaunga mkono lakini pia kuwaunganisha na wadau wengine ili kusudi mapambano haya dhidi ya rushwa yaweze kuleta matokea katika nchi yetu, ofisi ya mkuu wa wilaya na wadau wengine tutaendelea kutoa msukumo katika mapambano haya, mnafahamu sisi tunamipango mingi ya kupambana na rushwa tuna midahalo ya wanafunzi na wanavyuo pia tunazungumzia na UKIMWI, mmonyoko wa maadili na mapambano dhidi ya madawa ya kulevya” alisema Alhaj Shekimweri.

 

Kwa upande wake, Balozi wa kupinga Rushwa Shule za Msingi anayesoma Darasa la Nne, Genesnai Katawa, alisema kuwa rushwa inamuumiza kila mtu ambapo tumekimbia katika mbio za Sepesha Rushwa Marathon kuwahamasisha wananchi kutojihusisha na rushwa kwa kufanya mambo yasiyo ya haki. “Rais wetu mpendwa Dkt. Samia Suluhu Hassan anahakikisha Tanzania inakuwa nchi yenye haki na usawa, kila mtu anapinga rushwa kwa nguvu sana pia anatufundisha kuwa waaminifu na kufanya kazi kwa bidii na lakini pia tuungane kama Taifa, tukimbie kwa matumaini  katika haki na kuna baadhi ya madhala ya rushwa katika nchi yetu ni Pamoja na watu kukosa haki zao, kuhamasisha uhalifu ili kupambana ni kuhamasisha taasisi mbalimbali zina kemea’’ alisema Katawa.

 


Sepesha Rushwa Marathon ni Kauli mbiu ya Taasisi ya Ant-Corruption Voices Foundation yenye ujumbe wa Acha Rushwa ya Ngono, imekuwa ikifanya mbio hizi kwa mda wa miaka mitatu tangu 2022, kwa lengo la kupinga rushwa ya ngono kazini, shuleni na vyuoni.

MWISHO

Comments

Popular Posts

Wananchi Makutupora wafunguka changamoto ya Maji, Umeme na Shule kwa Mkuu wa Mkoa

Waziri Mchengerwa apongeza usimamizi wa miradi jijini Dodoma

Mkataba ujenzi Uwanja wa Mpira wa Miguu wasainiwa Dodoma