Baraza la Madiwani Jiji la Dodoma lapokea taarifa ya ufungaji hesabu mwaka 2023/2024

Na. Jackline Patrick na Emmanuel Lucas, DODOMA

Mkutano maalum wa Baraza la Madiwani kwaajili ya kujadili taarifa ya ufungaji hesabu za Halmashauri ya Jiji la Dodoma kwa mwaka wa fedha 2023/2024 umepokea, kujadili na kupitisha taarifa hiyo.


Diwani wa Kata ya Chang’ombe, Bakari Fundikira akichangia taarifa ya kufunga hesabu za halmashauri


Mkutano huo ulifanyika leo tarehe 29 Agosti, 2024 katika ukumbi wa mikutano wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma.

Wakati akichangia taarifa hiyo, Diwani wa Kata ya Chang’ombe, Bakari Fundikira alisema kuwa taarifa hiyo imeandaliwa vizuri. “Mstahiki Meya, kwanza tumeipokea taarifa na niipongeze timu ya wataalamu kwa kuandaa na kuwasilisha hii taarifa. Lakini la pili, Mstahiki Meya taarifa hii imetupa dira ya mwaka huu wa fedha kwenye yale mapungufu yaliyojionesha kwenye taarifa hii katika utekelezaji wa shughuli zetu za halmashauri, tukayafanyie kazi ili taarifa ya mwaka unaokuja basi haya mapungufu yaweze kupunguzwa kwa kiasi kikubwa. Taarifa hii itupe dira ya utekelezaji wa shughuli za halmashauri katika kuhakikisha tunaweka mambo sawa. Hata Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali atakapokuja, haya mambo mengine tuwe tumeshayatatua” alisema Diwani Fundikira.

Mkutano maalum wa Baraza la Madiwani kwa ajili ya kupokea na kujadili ufungaji wa hesabu za Halmashauri ya Jiji la Dodoma kuishia tarehe 30 Juni 2024, ulihudhuriwa na madiwani, viongozi wa CCM, Kamati ya Usalama ya Wilaya, wakuu wa taasisi, wakuu wa divisheni na vitengo na waandishi wa habari.

MWISHO


Comments

Popular Posts

Wananchi Makutupora wafunguka changamoto ya Maji, Umeme na Shule kwa Mkuu wa Mkoa

Waziri Mchengerwa apongeza usimamizi wa miradi jijini Dodoma

Mkataba ujenzi Uwanja wa Mpira wa Miguu wasainiwa Dodoma