Wanafunzi Chamwino wahimizwa kula mboga za majani

Na. Dennis Gondwe, CHAMWINO

WANAFUNZI wa Shule ya Msingi Chamwino wametakiwa kula kwa wingi mboga za majani ili kuwa na lishe bora itakayowasaidia kusanya vizuri katika masomo yao.

Afisa Lishe kutoka Kituo cha Afya Makole, Ezeleda Mongo (mwenye tisheti nyeupe) akiwafundisha wanafunzi jinsi ya kusia mbegu


Kauli hiyo ilitolewa na Afisa Lishe kutoka Kituo cha Afya Makole, Ezeleda Mongo alipokuwa akiongea na wanafunzi, walimu na wadau wa lishe katika tukio za kusia mbegu za mboga za majani katika Shule ya Msingi Chamwino.

Nimefurahi kujumuika nanyi katika hili zoezi la kuhamasisha mazoezi na zoezi la upandaji wa mbogamboga. Ninashauri sana jamii itumie mbogamboga na matunda zaidi kwa ajili ya kuhamasisha afya. Magonjwa yasiyo ambukiza yanaweza kutibika kwa njia ya chakula hususani mbogamboga na matunda” alisema Mongo.

Aidha, aliwashauri wanafunzi kuwa wanakula mbogamboga kwa wingi. “Wito wangu hata kwa watoto wa shule wanapokuwa wanaendelea kukua wale mbogamboga za majani kwa wingi. Ndio maana leo tumekuja kuonesha upandaji wa mbogamboga ili ziwe zinapatiokana kwa wingi katika shule zetu. Hii itatusaidia kupata watoto wenye uelewa mzuri na wenye afya njema” alisema Mongo.

Kwa upande wake Joseph Malolela kutoka Chama cha Baiskeli Mkoa wa Dodoma alisema kuwa waliamua kuendesha baiskeli kwa ajili ya kujikinga na magonjwa yasiyo ya kuambukiza hususani zoezi la uhamasishaji lishe bora. “Wadogo zetu nawaomba sana mjitahidi kufanya mazoezi ya kuendesha baiskeli yanaimarisha afya. Mnaniona mimi nilivyo, hii yote ni sababu ya baiskeli, baiskeli inajenga afya inakuwa safi na inakusaidia kujikinga na magonjwa yasiyo ya kuambukiza. Baiskeli inasaidia kuimarisha akili na mwili” alisema Malolela.



Zoezi la kusia mbegu za mboga katika Shule ya Msingi Chamwino lilitanguliwa na mbio za baiskeli zilizolenga kuhamaisha afya bora dhidi ya magonjwa yasiyo ya kuambuza na kuchochea masuala ya lishe bora kwa jamii.



MWISHO

 

 

Comments

Popular Posts

Wananchi Makutupora wafunguka changamoto ya Maji, Umeme na Shule kwa Mkuu wa Mkoa

Waziri Mchengerwa apongeza usimamizi wa miradi jijini Dodoma

Mkataba ujenzi Uwanja wa Mpira wa Miguu wasainiwa Dodoma