WAZIRI SILAA APANIA KUMALIZA MIGOGORO YA ARDHI JIJI LA DODOMA

 Na. Mwandishi wetu, DODOMA

Waziri Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Jerry Silaa amesema Wizara yake itahakikisha kero zote za migogoro ya ardhi zinakwisha katika Jijini la Dodoma ikiwa ni hatua muhimu ya utekelezaji   rasmi maagizo ya Rais, Dkt. Samia Suluhu Hassan.

Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Jerry Silaa akimsikiliza mwananchi katika Kliniki ya Ardhi Kata kwa Kata inayoendelea jijini Dodoma


Akiongea na wananchi waliofika katika Kliniki ya Ardhi Waziri Silaa alisema kuwa lengo la kuweka kambi katika Ofisi ya Kamshina Msaidizi wa Ardhi wa Jiji la Dodoma ni kuhakikisha wanawahudumia wananchi ipasavyo.

Waziri Silaa aliwaaambia wananchi waliofika kupata huduma katika kliniki hiyo kuwa atakuwa akifanya nao mazungumzo kila baada ya kumaliza ratiba ya bunge ili kujionea mwenyewe kero zinazowakabili wananchi hao.

Mwananchi Foime Yohana alitoa dukuduku lake kwa Waziri Silaa baada ya kuwa na kero ya muda mrefu ya kuvamiwa na kuchukuliwa eneo lake nakuomba Waziri huyo kusaidia ili aweze kupata haki yake.

Akiongea na vyombo vya habari wakati zoezi la kuhudumia wananchi likiendelea Katibu Mkuu wa Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Mhandisi Anthony Sanga alisema kuwa Kliniki ya Ardhi inayoendelea kwa wiki mbili jijini Dodoma, itakuwa mwarobaini wa changamoto nyingi za ardhi zinazowakabili wananchi wengi wa jiji hilo.

Mhandisi Sanga alisema kuwa baada ya kupokea maagizo ya Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi tayari ameanza kuyafanyia kazi yeye pamoja na watendaji wa Ardhi ikiwa ni kutatua changamoto za Ardhi zinazowakabili wananchi pamoja na ugawaji wa hatimiliki za Ardhi.

Katika hatua nyingine, Katibu Mkuu alisema kuwa Jiji la Dodoma ndio lenye changamoto nyingi za mgogoro ya Ardhi na wizara  imejipanga kikamilifu kwa kupiga kambi ya wiki mbili ili kuhakikisha changamoto zote za Ardhi Mkoa wa Dodoma zinapatiwa ufumbuzi kwa wakati ili wananchi wapate haki zao.

Katibu Mkuu wa Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Mhandisi Anthony Sanga (wa kwanza kushoto) akikabidhi Hati


“Kliniki ya Ardhi kwa sasa iko Dodoma na niendelevu kwa mikoa yote, pia Wizara inakusudia kuweka mifumo rahisi ya kutoa huduma kwa wananchi ikiwemo kufunga kamera katika ofisi za utoaji huduma ili kuepuka mianya ya ukiukwaji wa sheria” alisema Mhandisi Sanga.

Katika hatua nyingine Katibu Mkuu huyo alibainisha kuwa mchakato wa kuanzisha kwa Program tumishi yaani Ardhi App ili kurahisha wananchi kupata huduma popote pale nchini kwa njia ya mtandao ikiwemo huduma ya ulipaji wa pango ya Ardhi.




MWISHO

Comments

Popular Posts

Miundombinu ni nyenzo ya maendeleo ya Jiji la Dodoma

JIJI LA DODOMA KUPELEKA MIL 50 ZAHANATI YA KIKUYU

Umeme wa REA chachu ya viwanda vidogo vidogo Kata ya Ipala