RAIS, DKT. SAMIA ATOA FIDIA YA BILIONI 4.5 KWA WAKAZI DODOMA
Na. Queen Peter, DODOMA
WAZIRI wa Ardhi,
Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Jerry Silaa amesema wananchi takribani 496 wa Jiji
la Dodoma watapatiwa fidia ya kiasi cha Tsh. Bil. 4.5 ambazo tayari zimetolewa
na Rais, Dkt. Rais, Dkt. Samia Suluhu ili
kulipa wananchi waliotwaliwa maeneo yao kwa ajili ya uendelezaji wa Jiji
hilo.
Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Jerry Silaa (kushoto) akiongea na Waziri wa Madini, Anthony Mavunde (kulia) katika Kliniki ya Ardhi jijini Dodoma |
Waziri Silaa alisema
hayo wakati wa zoezi la utatuzi wa migogoro ya Ardhi linaloendelea katika uwanja wa Ofisi ya Ardhi Mkoa wa Dodoma
alipofika hapo kwa lengo la kuongea na wananchi ikiwemo kukabidhi hati kwa
baadhi ya wananchi.
Waziri Silaa
ameongeza kuwa wananchi watakao lipwa fidia hiyo ni wale ambao viwanja vyao vilitwaliwa
kimakosa na kuzua malalamiko mengi hivyo hiyo ni hatua muhimu ya kutatua kero
ya muda mrefu kwa wananchi hao.
Aidha, aliwataka watumishi wa Wizara ya Ardhi,
Nyumba na Maendeleo ya Makazi na Ofisi ya Mkurugenzi wa Halmashauri ya Jiji la
Dodoma wanaoshiriki katika Kliniki ya Ardhi kuhakikisha wanatatua migogoro yote
ya Ardhi inayowakabili wananchi.
“Mheshimiwa Rais,
ameelekeza tutatue changamoto za Ardhi zinazowakabili wananchi hivyo, hii ni
kazi muhimu muifanye kwa uadilifu”. Alisema Waziri Silaa.
Kwa upande wake
Mbunge wa Jimbo la Dodoma mjini na Waziri wa Madini, Anthony Mavunde alitoa
pongezi kwa Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi na Jiji la Dodoma
kwa kutoa huduma nzuri kwa wananchi wa Dodoma.
Aidha Mavunde, alishauri
kuwa baada ya kufanikiwa kwa kliniki hiyo watumishi watoke ofisini na kutembelea
kata kwa kata kutatua migogoro ya Ardhi wakiwa uwandani.
Kliniki ya Ardhi
ilianza tarehe 4 na itaendelea hadi tarehe 20 Novemba, 2023 itahudumia kata
zote 41 za Halmashauri ya Jiji la Dodoma na kutatua migogoro ya Ardhi, kutoa
hati milki na elimu ya masuala ya sheria ya Ardhi.
MWISHO
Comments
Post a Comment