WAJUMBE WA KAMATI YA FEDHA JIJI LA DODOMA WATAKIWA KUJIHOJI

Na. Dennis Gondwe, DODOMA

WAJUMBE wa Kamati ya Fedha na Utawala ya Halmashauri ya Jiji la Dodoma wametakiwa kuhoji utendaji kazi wa halmashauri na kutoa ushauri utakaoifanya halmshauri hiyo kusonga mbele.

Mwenyekiti wa Mkutano wa Mwaka wa Baraza la Madiwani, Prof. Davis Mwamfupe


Kauli hiyo ilitolewa na Mwenyekiti wa Mkutano wa Mwaka wa Baraza la Madiwani, Prof. Davis Mwamfupe baada ya kuunda Kamati ya Fedha na Utawala katika mkutano wa wazi uliofanyika katika Ukumbi wa Halmashauri ya Jiji.

Prof. Mwamfupe ambae ni Mstahiki Meya alisema kuwa Kamati ya Fedha na Utawala kwa mujibu wa kanuni itaongozwa na Mstahiki Meya. Wajumbe wake ni Mbunge Anthony Mavunde, Naibu Meya Asma Karama, Joan Mazanda, Daud Mkhandi, Jumanne Ngede, Bakari Fundikila, Ased Ndajilo, Grace Milinga, Neema Mwaluko na Elis Kitendya.

“Yeyote aliyepangwa katika kamati hii atangulie kuamini kwamba ni imani yangu kwake, kwamba anaweza kufanya hivyo kuliko vinginevyo kwamba huyu alikuwa anataka hizi kamati siyo baraza la uwakilishi ambapo kila jimbo lazima liwe na mtu. Ndiyo maana wakati mwingine tumepewa vipaji mbalimbali. Kwangu naongozwa na ukweli kwamba nataka tuhoji. Sisi ni wasimamizi nataka tuwe na uwezo wa kuhoji na kushauri vizuri” alisema Prof. Mwamfupe.

MWISHO.

Comments

Popular Posts

Wananchi Makutupora wafunguka changamoto ya Maji, Umeme na Shule kwa Mkuu wa Mkoa

Waziri Mchengerwa apongeza usimamizi wa miradi jijini Dodoma

Mkataba ujenzi Uwanja wa Mpira wa Miguu wasainiwa Dodoma