Na. Dennis Gondwe, MSALATO WANANCHI wa Kata ya Msalato iliyopo Halmashauri ya Jiji la Dodoma wamemshukuru Rais wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuwajengea shule mpya na kuwapunguzia wanafunzi kutembea umbali mrefu kufuata elimu. Afisa Mtendaji Kata ya Msalato, Devotha Selufara akimuelezea Rais, Dkt. Samia Suluhu Hassan alichoifanyia Kata ya Msalato Shukrani hizo zilitolewa na Afisa Mtendaji Kata ya Msalato, Devotha Selufara alipokuwa akiwatambulisha wataalam wa kata yake katika Shule ya Msingi Chikole kwa mgeni rasmi Mwenyekiti wa Umoja wa Wanawake wa Tanzania (UWT) Mkoa wa Dodoma. Selufara alisema “Shule ya Msingi Chikole ina wanafunzi 790 ilianza mwaka jana mwezi Julai. Baada ya kumaliza ujenzi ulioanza mwezi Aprili, 2023 kwa fedha ya mama Samia Suluhu Hassan aliyotupatia shilingi 318,800,000 kwa ajili ya ujenzi wa shule mpya ya msingi Chikole, ambapo tulijenga madarasa tisa, matundu 16 ya vyoo, jengo la utawala moja, tumefanikiwa kujenga madarasa ya chekechea ya mfano...
Na. Mwandishi Wetu, Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dkt. Doto Biteko, amehitimisha Kongamano la Nne la Kitaifa la Ufuatiliaji, Tathmini na Kujifunza lililofanyika jijini Mwanza akiweka mkazo kuwa mfumo wa ufuatiliaji na tathmini ni nyenzo muhimu katika kuhakikisha kuwa kila taasisi inatimiza wajibu wake kwa ufanisi na hivyo kufikisha huduma bora kwa wananchi. Kutokana na hilo, Dkt. Biteko amewataka Wataalam wa Ufuatiliaji na Tathmini nchini kufanya kazi kwa uaminifu na uadilifu bila kuogopa kuchukiwa kwani taifa linawategemea ili kuweza kutoa huduma bora kwa wananchi. “Hakuna mtu au taasisi inayoweza kufanikisha majukumu yake bila kufanya tathmini, ninyi ndio mnaoweza kutambua changamoto mapema na kuzitafutia suluhisho kabla hazijawa kubwa, taasisi yoyote inayokosa mfumo huu inafanana na timu inayoingia uwanjani bila refa..” alisema Dkt. Biteko. Alitoa mfano kuwa katika sekta ya umeme, kabla ya kupeleka huduma hiyo eneo lolote lazima tathmni ifanyike ili kuepuka kurudia...
Na. Dennis Gondwe, KIKUYU KUSINI MAMIA ya wananchi wa Kata ya Kikuyu Kusini wamejitokeza wa wingi kuupokea Mwenge wa Uhuru ulipowasili katika Shule ya Sekondari Wella kuzindua mradi wa ujenzi wa vyumba viwili vya madarasa wenye thamani ya shilingi 42,800,000 fedha kutoka mapato ya ndani ya halmashauri. Akiongelea wingi huo wa wananchi, Afisa Mtendaji Kata ya Kikuyu Kusini, Violet Oswald alisema kuwa muitikio wa wananchi kujitokeza kwa wingi utekelezaji wa misingi ya Mwenge wa Uhuru ya kuwaleta watu pamoja kwa upendo na kusisitiza umoja na mshikamano. “Wingi huu wa wananchi wa Kata ya Kikuyu Kusini ni utekelezaji wa kaulimbiu ya Mwenge wa Uhuru Mwaka 2026 isemayo ‘Tanzania ni yetu sote, tushikamane kwa pamoja kuleta maendeleo’. Hivyo, wananchi wamejitokeza kwa wingi kuupokea Mwenge wao na kushuhudia unavyozindua madarasa yao yaliyojengwa kwa fedha zao” alisema Oswald. Akisoma taarifa ya mradi wa ujenzi wa vyumba viwili vya madarasa katika Shule ya Sekondari Wella kwa Kiongozi wa Mbi...
Comments
Post a Comment