Na. Mwandishi wetu, Dodoma Wakazi wa Mtaa wa Mbwanga katika Kata ya Mnadani wanatarajia kunufaika na usafiri rahisi, kuimarika kwa shughuli za biashara na kuongezeka kwa fursa za maendeleo kufuatia ufunguzi wa barabara za mtaa katika uboreshaji wa miundombinu kwa ajili ya maisha bora ya wananchi. Akizungumza wakati wa hafla ya ufunguzi wa barabara hiyo, iliyofanyika katika moja ya barabara hizo, Diwani wa Kata ya Mnadani, Mugendi Kerenge alisema kuwa uboreshaji wa miundombinu ya barabara ni nguzo muhimu ya maendeleo kwa kuwa unarahisisha usafirishaji wa watu na bidhaa, kuchochea biashara na kuongeza upatikanaji wa huduma za kijamii. “Kukamilika kwa barabara zaidi ya kilomita 14 zimefunguliwa hii ni hatua muhimu katika safari ya maendeleo ya Kata ya Manadani. Itaondoa changamoto zilizokuwa zikiwakabili wananchi, hasa wakati wa mvua, na kufungua fursa zaidi za kiuchumi kwa wakazi wa Mbwanga na maeneo jirani. Natoa shukrani kwa Mkurugenzi wa Jiji la Dodoma kwa kutuwezesha kufani...
Watumishi wa Timu ya Halmasahuri ya Jiji la Dodoma inayoshiriki Mashindano ya SHIMISEMITA 2026 jijini Mbeya wanaendelea na kujifua katika mazoezi makali kwa ajili ya mashindano ya ngoma na kwaya, mazoezi yanayoendelea katika viwanja vya Shule ya Sekondari Dodoma. Mashindano ya SHIMISEMITA ya Mwaka 2026 yanaongozwa na kaulimbiu isemayo “Tupo Tayari kwa AFCON 2027”.
Na. Mwandishi wetu, DODOMA Uongozi wa Kanda Namba Tatu umefanya kikao na wamiliki wa vituo vya malezi ya watoto (Daycare) vinavyopatikana ndani ya kanda hiyo kwa lengo la kuimarisha utoaji wa huduma za malezi na maendeleo ya watoto. Akizungumza katika kikao hicho kilihofanyika katika Ofisi ua Kanda, Meneja wa Kanda Namba Tatu, CPA. Christina Changwala aliwataka wamiliki wa vituo hivyo kuhakikisha wanatoa malezi yanayozingatia maadili, mila na tamaduni za kitanzania ili kujenga kizazi chenye maadili mema na chenye mchango chanya katika maendeleo ya taifa. Aidha, aliwahimiza wamiliki wa vituo hivyo kuhakikisha wanakamilisha usajili wa vituo vyao ili vitambulike rasmi na viweze kuingizwa katika mifumo ya serikali ili kurahisisha usimamizi na utoaji wa huduma kwa mujibu wa sheria na taratibu. Wamiliki hao pia walikumbushwa umuhimu wa kutimiza wajibu wa kulipa kodi na tozo mbalimbali zinazotozwa na Halmashauri ya Jiji la Dodoma pamoja na mamlaka nyingine husika, kwa wakati kwa k...
Comments
Post a Comment