Na. Mwandishi Wetu, Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dkt. Doto Biteko, amehitimisha Kongamano la Nne la Kitaifa la Ufuatiliaji, Tathmini na Kujifunza lililofanyika jijini Mwanza akiweka mkazo kuwa mfumo wa ufuatiliaji na tathmini ni nyenzo muhimu katika kuhakikisha kuwa kila taasisi inatimiza wajibu wake kwa ufanisi na hivyo kufikisha huduma bora kwa wananchi. Kutokana na hilo, Dkt. Biteko amewataka Wataalam wa Ufuatiliaji na Tathmini nchini kufanya kazi kwa uaminifu na uadilifu bila kuogopa kuchukiwa kwani taifa linawategemea ili kuweza kutoa huduma bora kwa wananchi. “Hakuna mtu au taasisi inayoweza kufanikisha majukumu yake bila kufanya tathmini, ninyi ndio mnaoweza kutambua changamoto mapema na kuzitafutia suluhisho kabla hazijawa kubwa, taasisi yoyote inayokosa mfumo huu inafanana na timu inayoingia uwanjani bila refa..” alisema Dkt. Biteko. Alitoa mfano kuwa katika sekta ya umeme, kabla ya kupeleka huduma hiyo eneo lolote lazima tathmni ifanyike ili kuepuka kurudia...
Na. Dennis Gondwe, KIKUYU KASKAZINI SERIKALI kupeleka shilingi milioni 50 kukamilisha jengo la wodi ya wazazi katika Zahanati ya Kikuyu iliyopo Halmashauri ya Jiji la Dodoma kwa lengo la kuwafikishia huduma za afya wananchi. Mbunge Anthony Mavunde Kauli hiyo ilitolewa Mbunge wa Jimbo la Dodoma mjini, Anthony Mavunde alipokuwa akiongea na mamia ya wananchi wa Kata ya Kikuyu Kaskazini waliojitokeza kushiriki zoezi la usafi wa mazingira na upandaji miti kuzunguka Zahanati ya Kikuyu. Mavunde alisema “Mheshimiwa Mkuu wa Wilaya ya Dodoma jengo unaloliona kushoto kwako ni jitihada zangu mimi na diwani wa hapa. Habari njema ni kwamba kabla ya Jumatano wiki ijayo tunaingiza shilingi milioni 50 ambazo zitakwenda kukamilisha jengo hilo. Na nategemea mwezi Oktoba mwaka huu kina mama wataanza kuhudumiwa katika wodi ya wazazi”. Akiongelea historia ya jengo hilo, alisema kuwa mwaka 2020 aliwaahidi wananchi wa kata hiyo kujengewa wodi ya wazazi. “Nilikuja hapa nikiwa na Diwani Mwansasu nikakut...
Na. Dennis Gondwe, NZUGUNI WENZA wa viongozi katika Halmashauri ya Jiji la Dodoma wameshauriwa kuanzisha bustani za nyumbani ili kusaidia familia zao na wageni wanaowatembelea. Afisa Kilimo katika Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Lucy Kway Kauli hiyo ilitolewa na Afisa Kilimo katika Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Lucy Kway alipokuwa akiongelea umuhimu wa bustani za nyumbani kwa wenza wa viongozi wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma alipokuwa akihamasisha kilimo cha bustani hizo kwenye Banda la Jiji la Dodoma katika viwanja vya Nanenane Nzuguni. Kway alisema “nichukue nafasi hii kuwashauri wenza wa viongozi katika Halmashauri ya Jiji la Dodoma kulima bustani za nyumbani kwa ajili ya kusaidia familia zao na wageni wanaowatembelea. Hii ni muhimu kwa sababu wenza wa viongozi ni mfano wa kuigwa katika jamii hivyo ni rahisi kwa watu kuiga mfano mzuri kutoka kwa wenza wa viongozi hapa Halmashauri ya Jiji la Dodoma”. Akiongelea kilimo hicho kwa wananchi na watumishi wanaohamia Makao Makuu Do...
Comments
Post a Comment