Watumishi wa Kanda Namba Tatu watembelea Zahanati ya Soweto jijini Dodoma ambayo imekamilika na imeanza kufanya kazi. Zahanati hiyo inajumuisha jengo la huduma ya wagonjwa wa nje (OPD), chumba cha daktari, chumba cha kujifungulia wanawake, maabara na huduma ya mama, baba na mtoto. Uwepo wa zahanati hiyo ni kusogeza huduma karibu na wananchi ambao walikuwa wanatembea umbali mrefu kufuata huduma za afya katika Kituo cha Afya Zuzu au kwenda Hospitali ya Mkoa General
Na. Asteria Frank, DODOMA Gari la Darasa Tembezi kutoka Halmashauri ya Jiji Dodoma linalopakia abiria kwa lengo la kuelimisha kuhusu uandikishaji wa orodha ya wapiga kura kuelelea Uchaguzi wa Serikali za Mitaa linaendelea kuwafikia wananchi wengi katika maeneo mbalimbali ya halmashauri. Darasa Tembezi linapita kwenye kila kituo likipakia abiria na kuwapa elimu kisha linawashusha katika vituo vyao kwa kuhakikisha wameelewa zoezi la kujiandikisha katika orodha ya mpiga kura zoezi lililoanza tarehe 11-20 Oktoba, 2024 kuelekea Uchaguzi wa Serikali Mitaa. Muelimishaji na muhamasishaji wa Darasa Tembezi, Isabella Bruno aliwaeleza abira kuwa kuelekea Uchaguzi wa Serikali za Mitaa utakaofanyika tarehe 27 Novemba, 2024 na kusema kuwa mwananchi wanatakiwa kujiandikisha kwenye orodha ya wapiga kura katika vituo vilivyopo katika ofisi za mitaa, shule za msingi na sekondari, zahanati na vituo vya afya, maeneo ya wazi yenye mikusanyiko ya watu na majengo mengine ya taasisi za umma yaliyopo katik...
Comments
Post a Comment