Na. Nancy Kivuyo, DODOMA Katibu Tawala Mkoa wa Singida, ametembelea banda la Halmashauri ya Jiji la Dodoma na kuelezwa shughuli zinazotolewa katika banda hilo kwa upande wa Divisheni ya Kilimo Mjini. Alielezwa kuwa Kilimo Mjini kinahusiana na kilimo cha kisasa kinachojikita katika mbogamboga na matunda kutokana na ufinyu wa maeneo ya mjini wanapoishi wakulima. Afisa Kilimo katika Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Athumani Mpanda alieleza kuwa wakulima wanapaswa kutumia maeneo yao madogo waliyonayo kwaajili ya bustani kiroba. “Hizi bustani kiroba tunazitumia kupanda mbogamboga ambazo familia itatumia na hii ni kwasababu kama una kiroba cha kustawisha maua ambayo huyatumii ni vizuri kutumia kuotesha mboga mboga ambazo zitajumuisha lishe na kupendezesha mazingira yetu” alisema Mpanda. Aliongeza kuwa elimu ya bustani za majumbani imeendelea kutolewa katika taasisi nyingi za serikali pamoja na shule za msingi na sekondari. “Tumeanzisha elimu hii kwa lengo la kuhakikisha wakulima na wale ...
Na. Veronica John, DODOMA Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, Rosemary Senyamule awapongeza wafugaji kwa kujitokeza kwa wingi katika shindano la Paredi ya Mifugo Kitaifa 2025 ambalo hufanyika kila mwaka kuanzia tarehe 1-8 Agosti. Akizungumza na wafugaji, Senyamule alisema kuwa ameshuhudia mabadiliko na maboresho makubwa katika shughuli za mifugo ambapo hapo awali ilifanyika kikanda na sasa yameenda kimataifa. Alisema kuwa mashindano hayo kufanyika sehemu nyingi duniani yakiwa na lengo la kutambua mchango na juhudi za wafugaji katika kuchangia maendeleo ya taifa na ya mtu mmoja mmoja. “Maonesho haya huongeza ari kwa wananchi katika kuinua hadhi ya uzalishaji na tija kwa kutumia teknolojia mpya zilizoboreshwa katika shughuli za ufugaji ili kukidhi mahitaji ya soko. Na nimearifiwa kuwa maonesho na mashindano haya yaliasisiwa na Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete, Rais Mstaafu wa Awamu ya Nne wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania mwaka 2010 katika siku ya kilele cha sherehe za maonesho ya Nanenane Dodoma” a...
Na. Mwandishi wetu, DODOMA Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan amewataka wananchi, Wizara na Taasisi zinazohusika na sekta za kilimo, mifugo na uvuvi kutumia kikamilifu miundombinu, teknolojia na mitaji iliyowekezwa na Serikali ili kuongeza tija na ushindani wa Taifa katika masoko ya ndani na nje. Akizungumza katika kilele cha Maonesho na Sherehe za wakulima, wafugaji na wavuvi (Nanenane) zilizofanyika kitaifa katika Viwanja vya Nzuguni, Rais Dkt. Samia amesema miradi ya umwagiliaji iliyokamilika na inayoendelea kutekelezwa inapaswa kusimamiwa kwa viwango bora ili kuongeza eneo la kilimo cha umwagiliaji na kukuza tija ya mavuno. Alieleza kuwa Serikali ya Awamu ya Sita imeongeza bajeti ya kilimo ili kugharamia ujenzi na ukarabati wa skimu za umwagiliaji, mabwawa na visima, pamoja na kuanzisha mashamba makubwa ya pamoja, huku upatikanaji wa mbegu bora na mbolea ya kisasa ukiimarika kupitia ruzuku na kuanzishwa kwa viwanda vya uzalishaji, hatua iliyo...
Comments
Post a Comment