Na. Nancy Kivuyo, VIWANDANI Watendaji wa Kata 41 za Halmashauri ya Jiji la Dodoma wapokea Kompyuta na Printa kwa ajili ya kurahisisha na kuboresha utendaji kazi wenye ufanisi za kuwahudumia wananchi. Vifaa hivyo, viligawiwa katika hafla ya Ugawaji Kompyuta na Printa kwa Shule za Sekondari za Serikali na Watendaji wa Kata jijini Dodoma, iliyofanyika katika Shule ya Sekondari Viwandani. Akizungumza wakati wa ugawaji kompyuta hizo, Mbunge wa Jimbo la Dodoma Mjini, Anthony Mavunde, alisema kuwa anawapa kompyuta maafisa watendaji wa kata zote 41 kwaajili ya kuwasaidia kufanya kazi zao kidigitali zaidi. “Kompyuta na printa hizi natumaini zitachochea utendaji kazi ulio mzuri. Tuipongeze serikali chini ya uongozi wa Rais, Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa maboresho makubwa ya miundombinu kwenye sekta ya elimu jijini Dodoma ambapo kwa mwaka huu wa fedha zimetengwa shilingi bilioni 16” alisema Mavunde. Nae, Afisa Mtendaji wa Kata ya Hazina, Tunu Mahmoud, alisema kuwa ameguswa na tukio l...
Na. Halima Majidi, DODOMA Wafanyabiashara wa Soko Kuu la Majengo Jiji la Dodoma, wameishukuru serikali kwa kuona umuhimu wa kukarabati miundombinu ya Soko hilo na kuomba kuharakishwa uboreshaji wa soko ili waweze kuendelea na majukumu yao, kwa sababu soko hilo ndio soko mama la chakula. Akizungumza katika hafla ya Utiaji Saini Mikataba ya Ujenzi wa Miradi ya TACTIC uliofanyika katika Bustani ya Chinangali Park, Mfanyabiashara wa Soko Kuu la Majengo, Rhoda Boyi, alipongeza juhudi za Halmashauri ya Jiji la Dodoma kwa kuwashirikisha katika hatua zote za mradi "Tunatarajia kuwa sauti zetu zitasikilizwa na kuzingatiwa ili kuhakikisha kuwa maboresho haya yanakidhi mahitaji yetu na kuboresha mazingira ya biashara" alisema Boyi. Kwa upande wake Mohammedi, alifafanua changamoto watakazokumbana nazo katika kipindi chote cha ukarabati wa jengo hilo, ni pamoja na; kupoteza wateja, kuharibika kwa bidhaa kutokana na kuhamishw...
Na. Aisha Ibrahim, DODOMA Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Greyson Msigwa, amesema mradi wa ujenzi wa uwanja wa mpira wa miguu Dodoma, utakaoweza kubeba watu 32,000 ambao utagharimu kiasi cha shilingi bilioni 352 fedha za kitanzania, unatarajiwa kukamilika ndani ya miezi 24, chini ya serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Aliyasema hayo katika hafla ya utiaji saini mkataba wa ujenzi wa uwanja wa mpira wa miguu Dodoma, uliohusisha wizara hiyo na Kampuni ya Lemonta SPA, iliofanyika kiwanja cha Changamani, Kata ya Nzuguni, jijini Dodoma. Akizungumza kuhusu lengo la ujenzi wa uwanja huo, Msigwa alisema, mradi huo ni fursa kwa maendeleo ya michezo kwa wakazi wa Jiji la Dodoma kwasababu uwanja huo utatumika katika mashindano mbalimbali kitaifa na kimataifa ili kuhakikisha sekta ya michezo inazidi kukua. “Mradi huu ni fursa kwa maendeleo ya wakazi wa Dodoma lakini ni fursa kubwa kwa wanamichezo katika kukuza vipaji vyao, na sisi kama wizara tumejip...
Comments
Post a Comment