Na. Abdul Iddi, DODOMA MAKULU Shule ya Msingi Dodoma Makulu imeshukuru agenda ya Rais, Dkt. Samia Suluhu Hassan ya lishe shuleni kwa sababu inawaongezea ari ya kusoma na kupata matokeo yanayokusudiwa. Shukrani hiyo ilitolewa na Mwalimu wa Lishe, Rehema Kalinga alipokuwa akiongea na waandishi wa Habari waliotembelea shule ya msingi Dodoma makulu kujionea hali ya lishe kwa wanafunzi shuleni hapo. Alisema kuwa shule yake inazingatia ajenda ya Lishe kwa kuwapa wanafunzi wote kuanzi awali mpaka darasa la Saba uji. Darasa la Nne na la Saba kupata chakula cha mchana. “Toka ajenda hii kuanza kutekelezwa, tumeanza kuona matokeo Chanya. Kwanza kwakupunguza utoro, pia watoto darasani wanafundishika” alisema Mwl. Kalinga. Aidha, alitoa pongezi kwa wazazi kwa kusikiliza ajenda ya Lishe na kuitekeleza bila kusuasua kwasababu waliweza kutoa mchango kwa kiasi walicho kubaliana na kamati ya wazazi wa shule hiyo. “Muitikio ni mkubwa kwasababu watoto wote katika Shule ya Dodoma Makulu wanapata uji ...
Na. Coletha Charles, KIZOTA Wananchi wa Kata ya Kizota, Halmashauri ya Jiji la Dodoma waeleza kunufaika na mikopo ya asilimia 10 inayotolewa na halmashauri kwa makundi ya wanawake, vijana, na watu wenye ulemavu, ikiwa ni hatua ya kuinua maisha yao kiuchumi na kuimarisha shughuli zao za ujasiriamali. Kauli hiyo ilitolewa na Afisa Maendeleo ya Jamii wa Kata ya Kizota, Theresia Ntui alipokuwa akiongelea mikopo ya vikundi vya wanawake, vijana na watu wenye ulemavu kwa kipindi cha miaka minne ya serikali ya awamu ya sita. Alisema kuwa tangu kuanza kwa utolewaji mikopo ya asilimia 10 katika awamu ya sita ya Rais, Dkt. Samia, Kata ya Kizota imenufaika kwa jumla ya shilingi 410,000,000 zilizotolewa kwa vikundi mbalimbali vya kijamii. Alisema kuwa katika fedha hizo, vikundi 28 vya wanawake vilipokea shilingi milioni 192, vikundi 16 vya vijana vilipewa shilingi milioni 164, na vikundi vitano vya watu wenye ulemavu vilipata shilingi milioni 49. “Mikopo hii ni yenye masharti nafuu, h...
Na. Faraja Mbise, DODOMA Halmashauri ya Jiji la Dodoma imejipanga vema kutoa huduma kwa wananchi wote kwa kuzingatia mgawanyo wa Jimbo la Dodoma Mjini wenye mapendekezo ya kuligawa jimbo hilo kuwa Jimbo la Mtumba lenye jumla ya kata 20 na Jimbo la Dodoma Mjini lenye kata 21. Kauli hiyo ilitolewa na Mkurugenzi wa Jiji la Dodoma, Dkt. Frederick Sagamiko, mara baada ya majadiliano kutoka kwa Madiwani kuhusu taarifa iliyowasilishwa na Afisa Uchaguzi Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Albert Kasoga ya kuwasilisha mapendekezo ya mgawanyo wa Jimbo la Dodoma Mjini, katika Mkutano maalum wa Baraza la Madiwani lililofanyika tarehe 12 Machi, 2025 katika Ukumbi wa Mikutano wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma. Dkt. Sagamiko alisema “mgawanyo huu kwa sasa unalenga mgawanyo wa jimbo kuwa majimbo mawili, bado tutaendelea kuwa na halmashauri moja kwa maana ya utoaji huduma kwa ngazi ya Halmashauri ya Jiji la Dodoma. Jiji litaendelea kuwajibika katika utoaji wa huduma katika majimbo yote mawili”. Akizung...
Comments
Post a Comment