Na. Nancy Kivuyo, VIWANDANI Watendaji wa Kata 41 za Halmashauri ya Jiji la Dodoma wapokea Kompyuta na Printa kwa ajili ya kurahisisha na kuboresha utendaji kazi wenye ufanisi za kuwahudumia wananchi. Vifaa hivyo, viligawiwa katika hafla ya Ugawaji Kompyuta na Printa kwa Shule za Sekondari za Serikali na Watendaji wa Kata jijini Dodoma, iliyofanyika katika Shule ya Sekondari Viwandani. Akizungumza wakati wa ugawaji kompyuta hizo, Mbunge wa Jimbo la Dodoma Mjini, Anthony Mavunde, alisema kuwa anawapa kompyuta maafisa watendaji wa kata zote 41 kwaajili ya kuwasaidia kufanya kazi zao kidigitali zaidi. “Kompyuta na printa hizi natumaini zitachochea utendaji kazi ulio mzuri. Tuipongeze serikali chini ya uongozi wa Rais, Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa maboresho makubwa ya miundombinu kwenye sekta ya elimu jijini Dodoma ambapo kwa mwaka huu wa fedha zimetengwa shilingi bilioni 16” alisema Mavunde. Nae, Afisa Mtendaji wa Kata ya Hazina, Tunu Mahmoud, alisema kuwa ameguswa na tukio l...
Na. Faraja Mbise, DODOMA Halmashauri ya Jiji la Dodoma imejipanga vema kutoa huduma kwa wananchi wote kwa kuzingatia mgawanyo wa Jimbo la Dodoma Mjini wenye mapendekezo ya kuligawa jimbo hilo kuwa Jimbo la Mtumba lenye jumla ya kata 20 na Jimbo la Dodoma Mjini lenye kata 21. Kauli hiyo ilitolewa na Mkurugenzi wa Jiji la Dodoma, Dkt. Frederick Sagamiko, mara baada ya majadiliano kutoka kwa Madiwani kuhusu taarifa iliyowasilishwa na Afisa Uchaguzi Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Albert Kasoga ya kuwasilisha mapendekezo ya mgawanyo wa Jimbo la Dodoma Mjini, katika Mkutano maalum wa Baraza la Madiwani lililofanyika tarehe 12 Machi, 2025 katika Ukumbi wa Mikutano wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma. Dkt. Sagamiko alisema “mgawanyo huu kwa sasa unalenga mgawanyo wa jimbo kuwa majimbo mawili, bado tutaendelea kuwa na halmashauri moja kwa maana ya utoaji huduma kwa ngazi ya Halmashauri ya Jiji la Dodoma. Jiji litaendelea kuwajibika katika utoaji wa huduma katika majimbo yote mawili”. Akizung...
Na. Aisha Ibrahim, DODOMA Mkuu wa Wilaya ya Dodoma, Alhaj Jabir Shekimweri, amewapongeza wadau na waratibu wa elimu kwa kazi nzuri wanayoifanya ya kuhakikisha ufaulu wa wanafunzi ngazi ya msingi na sekondari unazidi kupanda kila siku katika Jiji la Dodoma. Alitoa pongezi hizo katika kikao cha wadau wa elimu na kuutambulisha mfuko wa lishe shuleni wa mwaka 2025, kilichofanyika ukumbi wa Vijana uliopo Kata ya Kiwanja cha Ndege, jijini Dodoma. Akizungumza katika kikao hicho alisema kuwa, lengo la Rais wa awamu ya sita, Dkt. Samia Suluhu Hassan, kuanzisha mpango wa lishe bora shuleni ni kukuza ufaulu wa wanafunzi na kuenzi kauli za Baba wa Taifa, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere, isemayo “Elimu tunayohitaji siyo tu ya kujua kusoma na kuandika bali ni elimu ya kujenga jamii yetu ya kufanya tuwe na uwezo wa kufanya kazi na kuleta maendeleo kwa wengine”. Aliongeza kuwa, chini ya utawala wa Rais wa awamu ya sita, Dkt. Samia Suluhu Hassan, serikali imejitahidi kuboresha na kutekeleza kw...
Comments
Post a Comment