RC Dodoma apongeza wafugaji kwa ushiriki wa Paredi ya Mifugo

Na. Veronica John, DODOMA

Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, Rosemary Senyamule awapongeza wafugaji kwa kujitokeza kwa wingi katika shindano la Paredi ya Mifugo Kitaifa 2025 ambalo hufanyika kila mwaka kuanzia tarehe 1-8 Agosti.



Akizungumza na wafugaji, Senyamule alisema kuwa ameshuhudia mabadiliko na maboresho makubwa katika shughuli za mifugo ambapo hapo awali ilifanyika kikanda na sasa yameenda kimataifa.

Alisema kuwa mashindano hayo kufanyika sehemu nyingi duniani yakiwa na lengo la kutambua mchango na juhudi za wafugaji katika kuchangia maendeleo ya taifa na ya mtu mmoja mmoja. “Maonesho haya huongeza ari kwa wananchi katika kuinua hadhi ya uzalishaji na tija kwa kutumia teknolojia mpya zilizoboreshwa katika shughuli za ufugaji ili kukidhi mahitaji ya soko. Na nimearifiwa kuwa maonesho na mashindano haya yaliasisiwa na Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete, Rais Mstaafu wa Awamu ya Nne wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania mwaka 2010 katika siku ya kilele cha sherehe za maonesho ya Nanenane Dodoma” alisema Senyamule.

Alimalizia kwa kusema kuwa idadi ya mifugo imeongezeka kwa kiwango cha kuridhisha. “Katika juhudi hizo, tumeshuhudia kuongezeka kwa idadi ya mifugo nchini kwa kipindi cha mwaka 2023/2024 mpaka mwaka 2025 idadi ya mifugo imeongezeka. Kwa maana hiyo, wizara imeweka vipaumbele katika kuimarisha upatikanaji wa maji, malisho, vyakula vya mifugo na elimu ya kisasa ya ufugaji.” alimaliza Senyamule.

Nae, Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi, Dkt. Edwin Mhede alikuwa na machache ya kusema kupitia sekta ya ufugaji kwenye mashindano hayo. “Maonesho hayo ya Paredi ya Mifugo ni fursa kwa wafugaji kubadilishana taarifa na teknolojia za ufugaji. Lakini pia kusanyiko hili linawaunganisha wafugaji pamoja na wataalam wetu ambao wanatoa huduma za mafunzo ya ugani kwenye maeneo mbalimbali kote nchini. Yote hii ni katika kueneza ujuzi na namna ya kuendeleza ufugaji katika taifa letu la Tanzania” alisema Dkt. Mhede.

Alimalizia kwa kuwashukuru wafugaji kwa kujitokeza kwa wingi katika paredi hilo. “Nawashukuru sana wafugaji kwa kujitokeza kwa wingi na kuleta mifugo yenu ya aina mbalimbali katika Paredi ya Mifugo hapa ili kuwahamasisha wananchi wengine wanaotarajia kupata elimu pia kuwa wafugaji bora wa baadae. Hatua hii itaongeza tija ya uzalishaji kwa kutumia vizuri teknolojia mpya,” alisema Dkt. Mhende.





Imehaririwa na Nancy Kivuyo

Comments

Popular Posts

Mfumo wa Ufuatiliaji na Tathmini ni nyenzo ya utendaji kazi serikalini – Dkt. Biteko

Waziri Mkuu Mgeni Rasmi NBC Dodoma Marathon 2023

Dodoma Sec kuongeza ufaulu kula mwaka