UMISSETA kuandaa vijana katika sekta ya Michezo Dodoma
Na. Dennis Gondwe, DODOMA
MASHINDANO
ya Umoja wa Michezo wa Shule ya Sekondari Tanzania (UMISSETA) ni takwa la
kikanuni katika mitaala ya sekta ya elimu kwa lengo la kuwaandaa wanafunzi kuwa
mahili katika sekta ya michezo Halmashauri ya Jiji la Dodoma.
Kauli hiyo ilitolewa na Afisa Michezo katika Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Peter Ititi alipokuwa akiongelea maandalizi ya michezo hiyo jijini Dodoma.
UMISSETA
ni michezo muhimu kwa wanafunzi na Halmashauri ya Jiji la Dodoma kwa ujumla.
“Michezo imetajwa kwenye mitaala ya elimu kutokana na umuhimu wake. Michezo
hiyo inalenga kuibua vipaji na kuviendelea kwa maslahi mapana ya taifa. Michezo
pia ni ajira na tumekuwa tukishuhudia vijana wetu wakishiriki katika ligi
mbalimbali” alisema Ititi.
Alisema
kuwa Halmashauri ya Jiji la Dodoma Mwaka 2024 ilitoa wanafunzi 56 kati ya
wanafunzi 120 waliochaguliwa kuunda timu ya UMISSETA ya Mkoa wa Dodoma
iliyoshiriki kitaifa. “Mwaka huu matarajio yetu ni kuchukua makombe yote na
tumejipanga kupeleka vijana wengi zaidi” alisema Ititi.
MWISHO
Comments
Post a Comment