UMISSETA Jiji la Dodoma yaanza Dodoma Sec

Na. Dennis Gondwe, DODOMA

MASHINDANO ya Umoja wa Michezo wa Shule ya Sekondari Tanzania (UMISSETA) ngazi ya kanda za Halmashauri ya Jiji la Dodoma yameanza katika viwanja vya Shule ya Sekondari Dodoma kwa lengo la uunda timu ya jiji hilo itakayoshiriki katika mashindano ngazi ya halmashauri ili kuunda timu ya Mkoa wa Dodoma.




Kauli hiyo ilitolewa na Afisa Michezo katika Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Peter Ititi alipokuwa akiongelea maandalizi ya michezo hiyo jijini Dodoma.

Ititi alisema kuwa halmashauri iliunda kanda sita zikiwa na shule tofauti tofauti za sekondari kwa lengo la kuzishindanisha. “Kila kanda ilitoa timu moja inayoshiriki michezo yote. Hivyo, baada ya mashindano haya itaundwa timu ya Halmashauri ya Jiji la Dodoma itakayoshindana na timu za halmashauri nyingine ili kuunda timu ya Mkoa wa Dodoma” alisema Ititi.

Michezo inayochezwa katika mashindano ya UMISSETA ni mpira wa miguu kwa wavulana na wasichana, mpira wa mikono wavulana na wasichana, mpira wa wavu wavulana na wasichana, mpira wa kikapu wavulana na wasichana, mpira wa meza wavulana na wasichana, mpira wa pete wasichana. Michezo mingine ni fani za ndani zinazohusisha ngoma, kwaya na muziki wa kizazi kipya pamoja na mashindano ya usafi. 

MWISHO

Comments

Popular Posts

Mfumo wa Ufuatiliaji na Tathmini ni nyenzo ya utendaji kazi serikalini – Dkt. Biteko

JIJI LA DODOMA KUPELEKA MIL 50 ZAHANATI YA KIKUYU

WENZA WA VIONGOZI WASHAURIWA KUANZISHA BUSTANI ZA NYUMBANI