Rushwa Adui wa Haki Uchaguzi wa Serikali za Mitaa

Na. Coletha Charles, DODOMA

Muelimishaji wa Darasa Tembezi Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Chacha Marwa amewataka wananchi kujitokeza kwa wingi kupiga kura ifikapo tarehe 27 Novemba, 2024 katika vituo husika.

 



Marwa alitoa elimu hiyo kwa wananchi waliopanda gari tembezi kutoka Soko la wazi la Machinga hadi Hospitali ya Benjamin Mkapa kwa kuwakumbusha kuwa haki ya kiongozi bora ipo mikononi mwao.

 Alisisitiza kuwa kupiga kura ni msingi wa maendeleo katika mitaa yao kwa kuzingatia haki na kutokupokea rushwa ya aina yoyote kutoka kwa wagombea wa nafasi ya mwenyekiti na wajumbe watano (5) wa serikali za mitaa.

 “Elimu hii ni muhimu kwa wananchi wote hasa mliojiandikisha kwenye orodha ya daftari la wapiga kura, ni muhimu sana kupata haki yako ya msingi, msipoenda kupiga kura mtashindwa kupata viongozi bora wa kuleta maendeleo. Mjitahidi kuchagua viongozi wazalendo wenye busara kwa kusikiliza sera zao. Pia walemavu ambao hawezi kufika katika vituo vya kupiga kura, serikali inashauri wananchi kuwafikisha katika vituo ili waweze kupiga kura kwasababu ni haki yako” alisema Marwa.

 Aidha, Serikali imetenga rasmi tarehe 27 Novemba, 2024 kuwa siku ya mapumziko kwa wafanyakazi na watu wote ambapo zoezi la kupiga kura litaanza saa 02:00 asubuhi hadi saa 10:00 jioni.

 

MWISHO

Comments

Popular Posts

Wananchi Makutupora wafunguka changamoto ya Maji, Umeme na Shule kwa Mkuu wa Mkoa

Waziri Mchengerwa apongeza usimamizi wa miradi jijini Dodoma

Mkataba ujenzi Uwanja wa Mpira wa Miguu wasainiwa Dodoma