Msimamizi wa Uchaguzi wa Serikali za Mitaa Jiji la Dodoma atoa hakikisho ofisi kufunguliwa na kufungwa kwa wakati siku ya mwisho kuchukua na kurudisha fomu

Na. Dennis Gondwe, DODOMA

MSIMAMIZI wa Uchaguzi wa Serikali za Mitaa mwaka 2024 Halmashauri ya Jiji la Dodoma Dkt. Frederick Sagamiko amewataka viongozi wa vyama 19 vya siasa kuwahamasisha wananchi kuchukua na kurejesha fomu akiwahakikishia kuwa ofisi zitafunguliwa na kufungwa kwa muda uliopangwa.


Msimamizi wa Uchaguzi wa Serikali za Mitaa mwaka 2024 Halmashauri ya Jiji la Dodoma Dkt. Frederick Sagamiko akiongea na waandishi wa habari ofisini kwake leo asubuhi


Dkt. Sagamiko alitoa kauli hiyo alipokuwa akiongea na waandishi wa habari ofisini kwake leo asubuhi kuwakumbusha wananchi kuwa ni siku ya mwisho ya kuchukua na kurejesha fomu za kugombea nafasi za uongozi wa serikali za mitaa.

“Leo tarehe 1 Novemba, 2024 ni siku ya mwisho ya kuchukua na kurejesha fomu za kugombea nafasi za uongozi wa serikali za mitaa. Ofisi zimefunguliwa mapema zaidi ili saa 2:00 asubuhi kuanza kutoa huduma hadi saa 10:00 jioni. Hakuna ofisi itakayochelewa kufunguliwa wala itakayowahi kufungwa. Hivyo, viongozi wa vyama vyote 19 niwaombe kuwahimiza wanachama wenu kuchukua na kurejesha fomu za kugombea nafasi za uongozi wa serikali za mitaa. Puuzeni taarifa zozote za kuelezea kuwa ofisi zitakuwa zimefungwa” alisema kwa msisitizo Dkt. Sagamiko.

Msimamizi wa Uchaguzi wa Serikali za Mitaa mwaka 2024 Halmashauri ya Jiji la Dodoma Dkt. Frederick Sagamiko


Ikumbukwe kuwa Halmashauri ya Jiji la Dodoma ina vituo 222, wakati zoezi la kuchukua na kurejesha fomu za kugombea nafasi za uongozi lilianza tarehe 26 Oktoba, 2024 na kuendelea hadi leo tarehe 1 Novemba, 2024.

MWISHO

Comments

Popular Posts

Global Affairs Canada yafurahishwa na utekelezaji wa Mradi wa AHADI katika Kata ya Chamwino

Umeme wa REA chachu ya viwanda vidogo vidogo Kata ya Ipala

Kata ya Ipala ipo mstari wa mbele katika Michezo