Ofisi wazi kuchukua na kurejesha fomu za wagombea nafasi za uongozi wa Serikali za Mitaa

Na. Asteria Frank, DODOMA

 

Vituo 222 vya Ofisi za Mitaa ya Halmashauri ya Jiji la Dodoma zimefunguliwa mapema zaidi leo tarehe 1 Novemba, 2024 kwa lengo la kuweka upana mkubwa kwaajili ya kuchukua na kurejesha fomu za wagombea nafasi ya uongozi Serikali za Mitaa.

 

Msimamizi wa Uchaguzi wa Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Dkt. Frederick Sagamiko 


Kauli hiyo ilitolewa na Msimamizi wa Uchaguzi wa Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Dkt. Frederick Sagamiko asubuhi ya leo katika ofisi yake wakati akizungumza na waandishi wa habari akiuhabarisha umma kuhusu tamati ya zoezi la uchukuaji na urejeshaji wa fomu za kugombea uongozi wa serikali za mitaa katika Jiji la Dodoma.

 

Dkt. Sagamiko alisema “hakuna ofisi yoyote katika Jiji la Dodoma ambayo itafungwa wakati zoezi hilo likiendelea. Naomba nitoe rai kwa viongozi wa vyama vya siasa vyote 19 katika Jiji letu la Dodoma kuhakikisha wanatumia siku hii muhimu ambayo ni siku ya mwisho kuhakikisha wagombea wanaowakilisha vyama vyao wanachukuwa fomu na kurejesha kwanzia muda wa saa 2:00 asubuhi na mwisho itakuwa ni saa 10:00 jioni, ofisi zetu zitakuwa wazi kwa masaa nane”.  

Zoezi la kuchukua na kurudisha fomu za kugombea nafasi za uongozi wa serikali za mitaa lilianza tarehe 26 Oktoba, 2024 na litakamilika leo tarehe 1 Novemba, 2024 saa 10 jioni.




MWISHO

Comments

Popular Posts

Global Affairs Canada yafurahishwa na utekelezaji wa Mradi wa AHADI katika Kata ya Chamwino

JIJI LA DODOMA KUPELEKA MIL 50 ZAHANATI YA KIKUYU

Umeme wa REA chachu ya viwanda vidogo vidogo Kata ya Ipala