Maadhimisho ya Siku ya Kichaa cha Mbwa kutoa elimu kudhibiti ugonjwa wa kichaa cha Mbwa

Na. Asteria Frank, DODOMA

 

Maadhimisho ya siku ya kichaa cha mbwa duniani yanalenga kuelimisha jamii juu ya kudhibiti ugonjwa wa kichaa cha mbwa pamoja na kutowa chanjo kwa paka na mbwa ili kuwakinga na ugonjwa huo.



Maadhimisho hayo yamefanyika katika ofisi za kituo za huduma za mifugo kanda ya kati Dodoma mjini ambapo wamefahamisha kuhusu kichaa cha Mbwa Pamoja na kutoa chanjo, dawa ya kuzuia viroboto na dawa za Minyoo kwa Mbwa na Paka.

Kauli hiyo ilitolewa na Afisa Mifugo wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Hussein Nyenye katika maadhimishi ya siku ya kichaa cha mbwa duniani yaliyofanyika katika Kituo cha Huduma za Mifugo Kanda ya Kati, kilichopo jijini Dodoma.

Nyenye alisema kuwa ni muhimu kwa wafugaji wa mbwa na paka kushirikiana na Wizara ya Mifugo na Uvuvi ili kuweza kuwapatia mbwa na paka chanjo kwa wakati sahihi kuzuia magojwa mbalimbali kwa wanyama hao na wafugaji wenyewe.

Alisema kuwa shughuli ya kudhibiti kichaa cha mbwa haiwezakani kufanyika na watu wa mifugo peke yake bali kwa ushiriki wa sekta nyingine kama Sekta ya Maendeleo ya Jamii, Sekta ya Afya na Sekta ya Elimu na ndio maana maafisa wanatoa elimu hii hata shuleni kwa watoto wetu na jamii kwa ujumla ili waweze kujikinga na ugonjwa wa kichaa cha mbwa.

“Lakini wakati huohuo, tunatoa elimu kwa wafugaji juu ya ufugaji bora wa mbwa. Mbwa kwa kawaida anatakiwa afugwe ndani na apewe tiba ikiwa ni pamoja na chanjo ya kichaa cha mbwa, dawa za minyoo na dawa za kuzuia wadudu kama viroboto, kupe na kadhalika ambao wanaleta usumbufu kwa wanyama na sio mbwa kudhurura mitaani” alisema Nyenye.

Nae Kaimu Afisa Mfawidhi, Kituo cha Huduma za Mifugo Kanda ya Kati, Dkt. Dioniz Ibrahim alisema kuwa maadhimisho ya siku ya kichaa cha mbwa yanafanyika tarehe 28 septemba, duniani pamoja na kuongeza uwelewa juu ya udhibiti wa ugojwa wa kichaa cha mbwa.

Dkt. Dioniz Ibrahim ambae pia ni Daktari wa Mifugo Kanda ya Kati alisema kuwa kituo hicho kipo chini ya Wizara ya Mifugo na Uvuvi kikihudumia mikoa miwili ya Dodoma na Singida na majukumu yake makuu ni udhibiti wa magonjwa ya wanayama ikiwemo kichaa cha mbwa.

“Katika maadhimisho haya tunafanya utoaji wa chanjo ya kwa mbwa na paka. Pamoja na kuwa maadhimisho haya yamefanyika hapa Halmashauri ya Jiji la Dodoma na Kalange kwa upande wa Singida, halmashauri zote 15 ambazo ndizo zinatengeneza kanda ya kati zinaendelea na maadhimisho haya na hivi sasa na zinafanya zoezi ya janjo kwa mbwa na paka” alisema Dkt. Ibrahim. 

Katika hatua nyingine Mwenyekiti wa Umoja Wafugaji Mbwa Dodoma, Francisi Macha alisema kuwa zoezi la kuchanja mbwa ni muhimu sana na pia wapo wafugaji wengi sana na changamoto ya kichaa cha mbwa ni changamoto kubwa sana kwa maisha ya binadamu ya kila siku. ”Ni vizuri sana watu kuelewa umuhimu wa kuchanja mbwa wetu kwasababu idadi ya mbwa katika jiji letu imekuwa kubwa. Hivi ninavyoongea kwenye umoja wetu kuna wanachama wasio pungua 218 kwahiyo, unaweza kuona kwamba ni kwa namna gani tutaongeza nguvu kwenye uelewa wa hili zoezi kwa ujumla” alisema Dkt. Ibrahim.

Nae Mfugaji wa mbwa Mtaa wa Chang’ombe, John Katema alisema kuwa nimeenda kuchanja mbwa wake kuwapa dawa ya minyoo pamoja na dawa ya kuzuia wadudu kama viroboto. “Kwasababu cha kwanza, nawajali afya zao na pili, napenda kuwashauri wafugaji wenzangu wa mbwa ambaye hajaweza kufika katika utowaji chanjo aweze kufika kwa maana zoezi hili ni la siku saba. Hivyo, ningependa kuwaambia kwamba ukiwa na mbwa ni lazima umjali na kumpenda kwa faida yake pamoja na wewe mwenyewe unajilinda kutokana na madhara kama endapo ikatokea akakudhuru” alisema Katema.

Ikumbukwe kuwa ugonjwa wa kichaa cha mbwa unakadiriwa kusababisha vifo vya watu 55,000 duniani na watu wapatao 1,500 nchini kila mwaka kutokana na ugonjwa huo wakati dunia ikilenga kuutokomeza ugonjwa huo ifikapo mwaka 2030.

MWISHO

Comments

Popular Posts

Wananchi Makutupora wafunguka changamoto ya Maji, Umeme na Shule kwa Mkuu wa Mkoa

Waziri Mchengerwa apongeza usimamizi wa miradi jijini Dodoma

Mkataba ujenzi Uwanja wa Mpira wa Miguu wasainiwa Dodoma