Vijana wahamasishwa kujiandikisha Daftari la Kudumu la Wapiga kura


Na. Dennis Gondwe, DODOMA MAKULU

VIJANA wameshauriwa kujitokeza kwa wingi kujiandikisha katika daftari la kudumu la wapiga kura katika Halmashauri ya Jiji la Dodoma ili waweze kushiriki zoezi la Uchaguzi Mkuu wa Rais, Wabunge na Madiwani.


Magdalena Samwel, mkazi wa Mtaa wa Mwangaza Kata ya Dodoma Makulu


Ushauri huo ulitolewa na Magdalena Samwel, mkazi wa Mtaa wa Mwangaza Kata ya Dodoma Makulu, Halmashauri ya Jiji la Dodoma muda mfupi baada ya kujiandikisha katika daftari la kudumu la wapiga kura kwenye kituo kilichopo Shule ya Sekondari Kisasa leo asubuhi.

Samwel alisema “leo nimewahi hapa kituoni kwa ajili ya kujiandikisha kwenye daftari la kudumu la mpiga kura ili niwahi kazini. Nimejiandikisha nikiwa mtu wa pili, ulinitangulia wewe ndugu mwandishi. Nimekuja ili nipate uhalali kwa kushiriki uchanguzi mkuu ujao kama mtanzania”.

Aidha, alitoa wito kwa vijana kujitokeza kwa wingi kujiandikisha katika daftari la kudumu la wapiga kura. “Napenda kuwashauri vijana wajitokeze kwa wingi ili waje kujiandikisha na kuboresha taarifa zao ili wapata kitambulisho kitakachowasaidia katika kushiriki uchanguzi mkuu ujao” alisema Samwel.

Wakati huohuo, Halima Shaban, mkazi wa Mtaa wa Mwangaza, Kata ya Dodoma Makulu baada ya kujiandikisha akiwa mtu wa tatu alisema kuwa zoezi hilo litawawezesha kushiriki katika kuwachagua viongozi ambao ni Rais, Wabunge na Madiwani. “Nimekuja kujiandikisha hapa ili nipate kitambulisho ambacho kitaniwezesha kushiriki uchaguzi na kuchagua Rais, Wabunge na Madiwani. Hivyo, niwashauri vijana wenzangu ambao bado hawajafika katika vituo kufika na kujiandikisha” alisema Shaban.


Halima Shaban, mkazi wa Mtaa wa Mwangaza, Kata ya Dodoma Makulu


Leo ni siku ya tano tangu kuanza kwa zoezi la uboreshaji wa daftari la kudumu la wapiga kura katika Halmashauri ya Jiji la Dodoma ukihusisha usajili wa wapiga kura wapya waliotimiza umri wa miaka 18, kurekebisha, kubadili taarifa au kuhama kituo chini ya kaulimbiu “Kujiandikisha, Kuwa Mpiga Kura ni Msingi wa Uchaguzi Bora”.




MWISHO

Comments

Popular Posts

Wananchi Makutupora wafunguka changamoto ya Maji, Umeme na Shule kwa Mkuu wa Mkoa

Waziri Mchengerwa apongeza usimamizi wa miradi jijini Dodoma

Mkataba ujenzi Uwanja wa Mpira wa Miguu wasainiwa Dodoma