Wanawake Dodoma watakiwa kujishughulisha

Na. Dennis Gondwe, MSALATO

WANAWAKE wametakiwa kujishughulisha na shughuli za uzalishaji mali ili kuweza kukuza kipato cha familia na taifa kwa ujumla kutokana na fursa za kazi zilizopo katika Mkoa wa Dodoma.

Mwenyekiti wa Umoja wa Wanawake Tanzania wa Chama Cha Mapinduzi (UWT) Mkoa wa Dodoma, Mwl. Neema Majula akiongea na wanawake waliohudhuria Kliniki Zahanati ya Msalato

Kauli hiyo ilitolewa na Mwenyekiti wa Umoja wa Wanawake Tanzania wa Chama Cha Mapinduzi (UWT) Mkoa wa Dodoma, Mwl. Neema Majula alipokuwa akiongea na wanawake katika maadhimisho ya siku ya wanawake Kata ya Msalato yaliyofanyika katika Zahanati ya Msalato katika Kata ya Msalato.

Mwl. Majula alisema kuwa kila mwanamke katika Mkoa wa Dodoma anatakiwa kujishughulisha ili kukuza kipato cha familia na taifa. “Ndugu zangu wakati mwingine ukatili wa kijinsia unatokana na kina mama kutokujishughulisha na uzalishaji mali katika ngazi ya familia. Hivyo, unyanyasaji unakuwepo kwa sababu kila kitu unamtegemea baba alete. Nataka nikwambie ukifanya kazi kwa bidii mfano ukianzisha biashara, ukafuga kuku hata ng’ombe, ukafungua duka au kigege na chenji hazikutoki hata unyanyasaji katika familia hautakuwepo, baba atakuheshimu kwa sababu una pesa” alisema Mwl. Majula.

Uploading: 3021339 of 3021339 bytes uploaded.


Alisema kuwa Mkoa wa Dodoma una fursa nyingi za kujiendeleza kiuchumi kutokana na kuwa na watu wengi waliohamia baada ya kuwa makao makuu. Fursa ya wingi wa watu ndiyo fursa ya kufanya biashara na kufanya kilimo cha mazao mbalimbali, aliongeza.

 

MWISHO

Comments

Popular Posts

Osterbay Dodoma wajitokeza usafi wa mazingira

Usafi wa Mazingira Kipaumbele Kata ya Chamwino

Wananchi wa Kata ya Mtumba wanufaika na Mikopo ya asilimia 10 ya Halmashauri