Wanasheria waanza mwaka mpya wa Mahakama

Na. Leah Mabalwe, DODOMA

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan alizindua rasmi mwaka mpya wa Mahakama 2024 na kuwatakia wanasheria wote kheri ya mwaka mpya wa mahakama ulioanza Februari 1, 2024.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwa katika picha ya pamoja na majaji wa Mahakama ya Rufaa

Kauli hiyo aliitoa katika kilele cha maadhimisho ya Siku ya Sheria nchini yaliyofanyika katika bustani ya mapumziko Chinangali jijini Dodoma.

“Tunaanza rasmi mwaka wa Mahakama na tunawakumbusha kuwa na mchango katika utendaji kazi kwa wadau wote wa Mahakama nchini, na nawakumbusha kufanya kazi kwa kuzingatia viapo vyenu vya utendaji kazi mlivyo viapa wakati wa kuanza kazi hii” alisema Dkt. Samia Suluhu Hassan.

Aidha, aliongezea kwa kuwapongeza watumishi wote wa Mahakama kwa kufanya kazi nzuri kwa kuendelea kutekeleza majukumu yao. “Nawapongeza sana waheshimiwa Mahakimu, wasajili wa mahakama kuu, majaji wa mahakama za rufaa na watumishi wote wa mahakama kwa namna ambavyo mnavyoendelea kutekeleza majukumu yenu, nawapongeza sana,” alisema Dkt. Samia Suluhu Hassan.

Kwa upande wake Jaji Mkuu wa Tanzania, Prof. Ibrahimu Juma ampongeza Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kuendelea kudumisha mfumo wa utoaji haki jinai. “Jitihada zako za kuijenga Tanzania ya maendeleo na haki kwa jamii inayozingatia misingi ya uhuru, haki na undugu na amani, hata hivyo utashi wako umedhihirika pale ulipounda Tume ya Haki Jinai kuanzisha kwa kampeni ya msaada wa kisheria ni miongoni mwa jitihada zako za utashi wa kiserikali na kuimarisha mfumo wa utoaji haki” alisema Prof. Juma.

Maadhimisho ya Siku ya Sheria nchini hufanyika kila mwaka tarehe 1 Februari na kwa mwaka 2024 maadhimisho yalifanyika jijini Dodoma yakiongozwa na kaulimbiu ‘Umuhimu wa dhana ya haki kwa ustawi wa Taifa, nafasi ya Mahakama na wadau katika kuboresha Mfumo Jumuishi wa Haki Jinai’.

 

MWISHO

Comments

Popular Posts

Mfumo wa Ufuatiliaji na Tathmini ni nyenzo ya utendaji kazi serikalini – Dkt. Biteko

JIJI LA DODOMA KUPELEKA MIL 50 ZAHANATI YA KIKUYU

Waziri Mkuu Mgeni Rasmi NBC Dodoma Marathon 2023