Wizara yatakiwa kutoa msaada wa kisheria kwa wananchi
Na. Josephina Kayugwa, DODOMA
Wizara ya Katiba na Sheria yatakiwa kutekeleza kikamilifu
msaada wa kisheria kwa wananchi kwa lengo la kutenda haki.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan akiongea na mamia ya wanasheria na wananchi |
Hayo yalisemwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,
Dkt. Samia Suluhu Hassan katika maadhimisho ya Siku ya Sheria nchini
yaliyofanyika katika bustani ya mapumziko ya Chinangali yakiongozwa na kaulimbiu
inayosema ‘Umuhimu wa dhana ya haki kwa ustawi wa Taifa, Nafasi ya Mahakama na
wadau katika kuboresha Mfumo Jumuishi wa Haki Jinai’.
Rais, Dkt. Samia Suluhu Hassan alisema taasisi zote za
kisheria zinatakiwa kushirikiana katika jambo la kutenda haki kwa jamii na
kuimarisha mfumo wa haki hii ni kutokana na kucheleweshwa na mashauri ambayo
yanatakiwa kutekelezwa mapema.
“Muda wa mashauri ya kimahakama unatakiwa kupunguzwa ili
kuwapa nafasi wananchi kwaajili ya kuendelea kutekeleza mambo mengine ya
kimaendeleo na majaji wote mnatakiwa kutokutoa hukumu za dhuluma. Na
niwapongeza kwa kuwa na kuanza mwaka mpya wa Mahakama na kuwa na mfumo sahihi
utakaowezesha kupunguza mashauri ya kesi mahakamani” alisema Rais, Dkt. Samia
Suluhu Hassan.
Kwa upande wake Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Jaji. Dkt. Eliezer
Feleshi alisema viongozi wa serikali wanatakiwa kuzingatia miongozo ya kisheria
iliyotolewa katika kutatua migogogro mbalimbali inayowakumba wananchi.
“Ofisi yangu kama Mwanasheria Mkuu wa Serikali ipo wazi kwa
viongozi na wananchi kwaajili ya kupata masaada wa kisheria pamoja na elimu juu
ya sheria na haki” alisema Jaji. Dkt. Feleshi.
Sambamba na hilo Rais wa Chama cha Wanasheria Tanganyika,
Aloyce Sungusia alimpongeza Rais, Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuweka
kipaumbele katika mfumo wa haki jinai.
Alisema lengo la maadhimisho ya Siku ya Sheria ni kuboresha
mahusiano mazuri kwa wadau wa sheria, kutoa huduma ya msaada wa kisheria kwa
wananchi kutoa elimu ya haki jinai kwa umma.
“Tutaendelea kuhimiza utendaji haki kwa kila mwananchi
ikiwemo kuwapa elimu kuhusu sheria na haki jinai na kuisaidia Serikali, Bunge
na Mahakama” alisema Sungusia.
Maadhimisho ya Siku ya Sheria hufanyika Februari 1 ya kila
mwaka.
MWISHO
Comments
Post a Comment