Wanasheria watakiwa kufuata misingi ya Uadilifu

Na. Arafa Waziri, DODOMA

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan aliwataka wanasheria nchini kufanya kazi kwa kufuata misingi ya uadilifu na kutenda haki.

 

Dkt. Samia Suluhu Hassan akiongea katika maadhimisho ya Siku ya Sheria nchini

Aliyasema hayo katika kilele cha maadhimisho ya Siku ya Sheria nchini yaliyofanyika jijini Dodoma na kuwataka wanasheria wote nchini kufanya kazi kwa uadilifu mkubwa na kutenda haki kwa wananchi. “Mnalazimika kusimama katika misingi ya dini pamoja na Katiba ya Tanzania. Mna dhima mbinguni na Duniani kwahiyo, mna wajibu wa kutenda haki ili kuweka amanikwa wananchi” alisema Dkt. Hassan

Lakini pia aliwapongeza wanasheria kuendelea kufanya kazi ya kusaidia wananchi kupata haki na kuwasisitiza kuwa na ushirikiano baina yao ili kubaini mapungufu yaliyopo na kuchukua hatua kwa pamoja. “Niwapongeze kwa namna mnavyoendelea kutimiza

majukumu yenu na hii ni ushahidi tosha kwamba mnafanya kazi kubwa na kwamba Mahakama inakwenda na mabadiliko kutoka hatua moja kwenda nyingine” alisema Dkt. Hassan.  

Pia alisema kuwa katika kuendelea kutekeleza Ilani ya Uchaguzi ya Chama Cha Mapinduzi serikali imeeendelea kuweka mazingira mazuri kwa kushirikiana na Mahakama ili kuongeza ufanisi katika kutoa haki kwa wananchi.

“Serikali kwa upande wetu tunaendelea na mkakati wa namna ya kuteleza Ilani ya CCM kwa kuongeza wigo mpana katika kutatua sheria lengo likiwa ni kuongeza ufanisi kwa kuongeza idadi ya watenda kazi wa Mahakama ili kupunguza mrundikano wa kesi” alisema.

Nae Jaji Mkuu wa Tanzania, Prof. Ibrahim Juma alimshukuru Rais, Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuendelea kutoa mchango mkubwa katika Mahakama, huku akiahidi kuwa wataendelea kutoa mchango mkubwa katika kuweka haki na uadilifu. Vilevile, alitoa wito kwa wadau wa sheria kuendelea kuungana kutoa ushirikiano lengo ni kuwa na haki katika jamii. “Maboresho ya miundombinu katika Tehama yamesaidia kupunguza mrundikano wa kesi na tuhaahidi kuwa tutaendelea kufanya kazi kwa ufanisi mkubwa na tunaomba wadau wengine wa sheria waendelee kujitokeza na kutoa ushirikiano ili kuhakikisha utendaji wa Mahakama unakuwa na matokeo kwa jamii” alisema Prof. Juma.

 


Siku ya Sheria nchini ilihitimishwa jijini Dodoma ikiwa na kaulimbiu isemayo ‘Umuhimu wa dhana ya haki kwa ustawi wa taifa, nafasi ya Mahakama na wadaau katika kuboresha Mfumo Jumuishi wa Haki Jinai’

 

                                    MWISHO

 

 

 

Comments

Popular Posts

Jiji la Dodoma lapewa angalizo lishe bora kwa wananchi

RC Dodoma apongeza wafugaji kwa ushiriki wa Paredi ya Mifugo

Vijana waalikwa kushiriki Kongamano S/M Mbwanga