Mchakato kugawa mitaa kuanzia kwenye mitaa

Na. Dennis Gondwe, DODOMA

WANANCHI wametaarifiwa kuwa mchakato wa kugawa maeneo ya mitaa ambayo yanaonekana makubwa ili kusogeza huduma karibu na wananchi unaanzia katika ngazi ya mtaa.

Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Joseph Fungo akijibu maswali ya papo kwa papo


Kauli hiyo ilitolewa na Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Joseph Fungo alipokuwa akijibu swali la papo kwa papo la Diwani wa Kata ya Iyumbu, Richard Sutuchi aliyetaka kujua utaratibu wa wa kugawa maeneo ya mitaa ili kusogeza huduma kwa wananchi katika Mkutano wa Baraza la Madiwani uliofanyika katika ukumbi wa mikutano wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma.

Fungo, alisema kuwa utaratibu wa kugawa mitaa unaanzia katika mitaa husika. “Mapendekezo yanatoka katika mitaa husika na utaratibu huo unapelekwa katika kikao cha kamati ya maendeleo ya kata hadi halmashauri. Hivyo, mchakato uanzie kwenye mtaa” alisema Fungo.

MWISHO

Comments

Popular Posts

Wananchi Makutupora wafunguka changamoto ya Maji, Umeme na Shule kwa Mkuu wa Mkoa

Waziri Mchengerwa apongeza usimamizi wa miradi jijini Dodoma

Mkataba ujenzi Uwanja wa Mpira wa Miguu wasainiwa Dodoma