Dodoma Sec yateuliwa ufundishaji mubashara nchini

Na. Dennis Gondwe, DODOMA

BARAZA la Madiwani la Halmashauri ya Jiji la Dodoma limetaarifiwa kuwa Shule ya Sekondari Dodoma imeteuliwa kuwa miongoni mwa shule 10 za majaribio ya ufundishaji mubashara nchini.

Mwenyekiti wa Mkutano wa Baraza la Madiwani, Prof. Davis Mwamfupe akisisitiza jambo


Taarifa hiyo ilitolewa na Mwenyekiti wa Mkutano wa Baraza la Madiwani, Prof. Davis Mwamfupe alipokuwa akitoa taarifa ya Mwenyekiti katika Mkutano wa Baraza la Madiwani uliofanyika katika ukumbi wa mikutano wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma.

Prof. Mwamfupe alisema kuwa Shule ya Sekondari Dodoma imeteuliwa kuwa miongoni mwa shule 10 za majaribio nchini ya ufundishaji mubashara kwa njia ya mtandao. Alisema kuwa ufundishaji huo unamuwezesha mwalimu wa shule moja kufundisha idadi kubwa ya shule kadri inavyowezesha.

“Mwalimu yupo Shule ya Sekondari Kibaha anafundisha wanafunzi wa Shule ya Sekondari Dodoma na wanafunzi wote wanamuona na wanapata fursa ya kuuliza maswali na kujibiwa. Gharama ya mtambo mmoja wa kusimika mfumo huu ni shilingi 67,000,000 kwa shule ya Dodoma sekondari. Hivyo, tutaangalia jinsi ya kuwezesha shule za pembezoni mwa Halmashauri ya Jiji la Dodoma kuweza kuwa na mfumo huo” alisema Prof. Mwamfupe.

MWISHO

Comments

Popular Posts

Wananchi Makutupora wafunguka changamoto ya Maji, Umeme na Shule kwa Mkuu wa Mkoa

Waziri Mchengerwa apongeza usimamizi wa miradi jijini Dodoma

Mkataba ujenzi Uwanja wa Mpira wa Miguu wasainiwa Dodoma