JIJI LA Dodoma linajali wanafunzi

Na. Dennis Gondwe, DODOMA

HALMASHAURI ya Jiji la Dodoma inawaonea huruma na kuwajali wanafunzi kwa watengenezea mazingira mazuri ya kujifunzia.

Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Joseph Fungo


Kauli hiyo ilitolewa na Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Joseph Fungo alipokuwa akijibu swali la Diwani wa Hazina, Samwel Mziba aliyetaka kujua ni lini halmashauri itakuwa na huruma kwa wanafunzi wa Shule ya Msingi Uhuru kwa kuifanyia ukarabati mkubwa ili iendane na hadhi ya jiji.

Fungo alisema kuwa halmashauri inawaonea huruma wanafunzi na kuwajali kwa wajengea miundombinu ili waweze kusoma katika mazingira bora na salama. “Mheshimiwa mwenyekiti, tulimpeleka mhandisi kufanya makadirio ya gharama za kufanya ukarabati wa madarasa yaliyochakaa katika shule hiyo na mipaka kwa ajili ya ujenzi wa uzio. Hadi sasa mbao na ‘gypsum board’ zimeshafika shuleni kwa ajili ya kufanya ukarabati wa shule hiyo” alisema Fungo.

Aidha, Mstahiki Meya alisema kuwa kuna utayari wa baadhi ya wananchi waliosoma katika shule ile kuchangia ukarabati huo wanasubiri hatua za awali zianze.


MWISHO

Comments

Popular Posts

Mfumo wa Ufuatiliaji na Tathmini ni nyenzo ya utendaji kazi serikalini – Dkt. Biteko

JIJI LA DODOMA KUPELEKA MIL 50 ZAHANATI YA KIKUYU

WENZA WA VIONGOZI WASHAURIWA KUANZISHA BUSTANI ZA NYUMBANI