KATA YA CHAMWINO YATOA ELIMU YA UKATILI WA KIJINSIA

Na. Dennis Gondwe, CHAMWINO

Timu ya wataalam kutoka Kata ya Chamwino yajikita katika utoaji wa elimu ya kupinga vitendo vya ukatili wa kijinsia kwa makundi mbalimbali kwa lengo la kuhakikisha uelewa mpana katika mapambano hayo unaenea kwa jamii.


Akielezea maeneo yaliyopewa kipaumbele na timu hiyo katika kutoa elimu, Afisa Mtendaji kata ya Chamwino, Lucas Nkelege alisema kipaumbele ni kutoa elimu kwa jamii.

Alisema kuwa timu hiyo ilijikita katika kuelezea wajibu wa wazazi na walezi katika makuzi ya watoto na sheria inayomlinda mtoto Namba 21 ya mwaka 2009. Maeneo mengine yaliyopewa msisitizo ni umuhimu wa ulinzi wa watoto wa kiume na madhara kwa watoto hao endapo hawatapewa uangalizi wa karibu na hatua za kufanya pale mtoto amapofanyiwa ukatili.

Aidha, wazazi na walezi walitaarifiwa uwepo wa kituo cha huduma za pamoja na msaada kwa watoto waliofanyiwa ukatili (one stop center).

Nkelege alisema kuwa timu shirikishi ya wataalamu ya Kata ya Chamwino iliongozwa na Afisa Mtendaji kata ya Chamwino, ikiwa na Afisa ushirikishwaji wa Jeshi la Polisi wa Kata ya Chamwino, Afisa Ustawi wa Jamii, Afisa Maendeleo ya Jamii walishiriki kutoa elimu ya kupinga ukatili wa kijinsia kwenye misitiki, na vijiwe vya bodaboda katika Kata ya Chamwino.





MWISHO

 

Comments

Popular Posts

Wananchi Makutupora wafunguka changamoto ya Maji, Umeme na Shule kwa Mkuu wa Mkoa

Waziri Mchengerwa apongeza usimamizi wa miradi jijini Dodoma

Mkataba ujenzi Uwanja wa Mpira wa Miguu wasainiwa Dodoma