SERIKALI YATOA BIL 1 UJENZI HOSPITALI YA WILAYA DODOMA

Na. Dennis Gondwe, DODOMA

SERIKALI imetoa shilingi bilioni moja kwa ajili ya ujenzi wa Hospitali ya Wilaya ya Dodoma kwa lengo la kuboresha huduma za afya na kuzisogeza huduma hizo karibu zaidi na wananchi.

Mkurugenzi wa Jiji, John Kayombo akiongea na waandishi wa habari


Kauli hiyo ilitolewa na Mkurugenzi wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma, John Kayombo alipokuwa akiongelea mafanikio ya serikali ya awamu ya sita inayoongozwa na Rais, Dkt. Samia Suluhu Hassan wakati wa Uzinduzi wa Mikutano ya Wakuu wa Mikoa na Wakurugenzi wa Mamlaka za Serikali za Mitaa na Waandishi wa Habari katika kampeni ya Tumekusikia Tumekufikia uliofanyika katika ukumbi wa mikutano wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Dodoma.

Kayombo alisema “kwa upande wa afya mheshimiwa rais ameleta fedha nyingi. Ameleta shilingi bilioni moja kwa ajili ya ujenzi wa Hospitali ya Wilaya ya Dodoma inayojengwa eneo la Nala. Kituo cha Afya Makole kimekuwa kikipokea watu wengi sana, mheshimiwa Rais ametuletea shilingi milioni 750 kwa ajili ya kukipanua na kuboresha utoaji wa huduma kwa wananchi. Vilevile, ametuletea fedha shilingi milioni 500 kwa ajili ya ujenzi wa kituo kipya ya Afya Chang’ombe”.

Kwa upande wake Waziri wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Nape Nnauye alisema kuwa program hiyo ni muhimu kuzungumzia maendeleo katika maeneo mbalimbali nchini. “Serikali ya Rais, Dkt. Samia Suluhu Hassan imekusikia imekufikia. Wale kima mama walikuwa na shida ya kujifungua tumekusikia tumekufikia. Wale ambao ilikuwa ni lazima kumsafirisha mgonjwa wake kumpeleka Dar es Salaam kwenda kutibiwa tumekusikia tumekufikia, ni kampeni rahisi na inaeleka” alisema Waziri Nnauye.



MWISHO

Comments

Popular Posts

Wananchi Makutupora wafunguka changamoto ya Maji, Umeme na Shule kwa Mkuu wa Mkoa

Waziri Mchengerwa apongeza usimamizi wa miradi jijini Dodoma

Mkataba ujenzi Uwanja wa Mpira wa Miguu wasainiwa Dodoma