JIJI LA DODOMA LAPELEKA MIL. 20,000,000 KUMALIZIA MAABARA
Na. Dennis Gondwe, KIKUYU KUSINI
HALMASHAURI
ya Jiji la Dodoma imepeleka shilingi 20,000,000 kwa ajili ya ukamilishaji wa jengo
la maabara katika Shule ya Sekondari Wella iliyopo Kata ya Kikuyu Kusini.
![]() |
Mkurugenzi wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma, John Kayombo |
Kauli
hiyo ilitolewa na Mkurugenzi wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma, John Kayombo
katika hafla fupi ya kupokea vifaa vya maabara vilivyotolewa na Mbunge wa Jimbo
la Dodoma mjini.
Kayombo
alisema “Mheshimiwa mbunge hapa tayari unaona ujenzi unaendelea kwenye maabara
yetu kwa maelekezo ya Mheshimiwa Rais, na sisi hatuwezi kukuangusha kwa sababu
tunafanya kazi kwa kushirikiana. Tumeshaleta shilingi 20,000,000 hapa kwa ajili
ya kukamilisha ujenzi wa maabara na inaenda kumaliziwa. Tunataka wanafunzi wetu
waweze kufanya majaribio ya sayansi kwa vitendo. Mheshimiwa mbunge kwa
maelekezo yako ya juzi ulituelekeza tutafute fedha na tumeshapata shilingi 8,000,000
kwa ajili ya kukamilisha matundu saba ya vyoo. Miongoni mwa changamoto ambazo
zimezungumwa na mkuu wa shule nimezipokea na nitakaa na timu yangu ya
menejimenti na madiwani tuone namna bora ya kuzitatua”.
Alishukuru
kwa vifaa vya maabara alivyokabidhi Mbunge wa Jimbo la Dodoma mjini. “Vifaa
hivi ulivyotukabidhi nikushukuru sana. Wewe ni miongoni mwa wabunge wachache
wanaoyapenda majimbo yao. Nikuombe moyo huu uendelee na sisi tupo bega kwa bega
na wewe tutakupa ushirikiano wakutosha na hakuna atakayekuangusha. Endelea
kupiga kazi tupo pamoja na wewe usiku na mchana, muda wowote tutafutie vya
kutosha huko” alisisitiza Kayombo.
Aidha,
alimuombea kwa Mungu ili kukabiliana na changamoto za kazi. “Mheshimiwa mbunge
nikuombe sana kwenye hizi kazi changamoto ni nyingi sisi tutaendelea kukuombea
wala usikate tama, Mwenyezi Mungu atakubariki unafanya mengi mazuri hata Mungu
anaona kwa hiyo, yale maneno ya kukukatisha tamaa achana nayo” alisema Kayombo.
Mbunge
wa Jimbo la Dodoma mjini, Anthony Mavunde alikabidhi vifaa vya maabara za
masomo ya sanyansi vyenye thamani ya shilingi 9,000,000 kwa shule tatu za
sekondari Wella, Makutopora na Mtemi Chiloloma katika Jiji la Dodoma.
MWISHO
Comments
Post a Comment