MAANDALIZI UCHAGUZI MDOGO KATA YA NALA YAKAMILIKA

Na. Dennis Gondwe, Dodoma

WANANCHI wa Kata ya Nala wametakiwa kutumia haki yao ya kidemokrasia kujitokeza kwa wingi kumchagua Diwani ili awawakilishe na kutetea maslahi yao.

Kauli hiyo ilitolewa na Msimamizi wa Uchaguzi Jimbo la Dodoma mjini, John Kayombo alipotembelea na kukagua vituo vya kupigia kura katika Kata ya Nala.

Kayombo alisema “maandalizi ya uchaguzi mdogo wa Kata ya Nala yamekamilika. Jumla ya vyama 11 vilichukua na kurejesha fomu na kupata nafasi ya uteuzi wa kugombea nafasi ya udiwani wa Kata ya Nala. Kwa upande wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi ambayo mimi ndiyo Msimamizi wa Uchaguzi wa Jimbo la Dodoma mjini na Kata ya Nala tumejiandaa vizuri na hatuna mapungufu yoyote”.

Alisema kuwa jumla ya wapiga kura wanaopaswa kupiga kura ni 3,741.  “Niwaombe wananchi kujitokeza kwa wingi ili kutumiza haki yao ya msingi kumchagua mwakilishi wao ambae ni Diwani wa Kata ya Nala” alisema Kayombo.

Kata ya Nala inafanya uchaguzi mdogo kufuatilia kifo cha aliyekuwa Diwani wa kata hiyo aliyefariki tarehe 10 Aprili, 2023 ikiwa na vituo 12 vya kupigia kura.

MWISHO 

Comments

Popular Posts

Wananchi Makutupora wafunguka changamoto ya Maji, Umeme na Shule kwa Mkuu wa Mkoa

Waziri Mchengerwa apongeza usimamizi wa miradi jijini Dodoma

Mkataba ujenzi Uwanja wa Mpira wa Miguu wasainiwa Dodoma