BEST WESTERN DODOMA CITY HOTEL SULUHU MALAZI MAKAO MAKUU
Na. Dennis Gondwe, DODOMA
Ujenzi
wa Hoteli ya Halmashauri ya Jiji la Dodoma umeitikia changamoto ya huduma ya
malazi kwa mabalozi na wageni wengine wanaotembelea makao makuu ya nchi kwa
huduma mbalimbali.
![]() |
Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, Rosemary Senyamule |
Kauli
hiyo ilitolewa na Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, Rosemary Senyamule alipokuwa akitoa
salamu za Mkoa wa Dodoma kwa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali za
Mitaa (LAAC) ilipotembea miradi ya Halmashauri ya Jiji la Dodoma.
Senyamule
alisema kuwa Halmashauri ya Jiji la Dodoma inakabiliwa na changamoto ya sehemu
za malazi kwa mabalozi na wageni mashuhuri. “Kuwepo kwa vitega uchumi hivi Jengo
la Kitega Uchumi Mtumba na Hoteli ya Best Western Dodoma City ni faida kubwa wa
maendeleo ya Dodoma. Mheshimiwa Mwenyekiti mabalozi wengi walikuwa wanakuja
Dodoma na kurudi Dar es Salaam, Balozi anakuja na ndege ya asubuhi anaenda
wizarani akimaliza shughuli zilizompeleka anaondoka. Sasa hivi mabalozi wengi
wanafikia Best Western Dodoma City Hoteli pale mjini, wanaona inaendana na
mahitaji yao” alisema Senyamule.
Alisema
kuwa serikali inatengeneza miundombinu kwa ajili ya sekta binafsi kufanya kazi.
“Tunaona miundombinu ya kiserikali ni mingi ila tunahitaji uwekezaji wa sekta
binafsi na wadau wengine kwa ajili ya vivutio vya kibiashara kwa Jiji la Dodoma”
alisema Senyamule.
Akiwasilisha
taarifa ya mradi wa ujenzi wa Hoteli ya Jiji la Dodoma Mkurugenzi wa
Halmashauri ya Jiji la Dodoma, John Kayombo alisema kuwa gharama ya ujenzi wa
mradi ni shilingi 9,995,881,126. “Mafanikio ya mradi ni kuongeza mapato ya
halmashauri na kutoa fursa za ajira kwa wananchi. Hadi sasa jumla ya wananchi
80 wameajiriwa” alisema Kayombo.
Ikumbukwe
kuwa hoteli ya Halmashauri ya Jiji la Dodoma ilianza kujengwa Mwezi Agosti,
2019 na kukamilika Aprili, 2023 kwa fedha za mapato ya ndani ya jiji.
Best Western Dodoma City Hotel |
MWISHO
Comments
Post a Comment