WAFUGAJI KANDA YA KATI WASHAURIWA KULIMA MALISHO YA MIFUGO

Na. Dennis Gondwe, NZUGUNI

WAFUGAJI katika Halmashauri ya Jiji la Dodoma wameshauriwa kufanya ufugaji wa ndani na kulima malisho ya mifugo ili kujihakikishia kipato.

Afisa Mifugo wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Anna Mchomvu


Kauli hiyo ilitolewa na Afisa Mifugo wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Anna Mchomvu alipokuwa akiongea na waandishi wa habari walipotembelea Banda la Mifugo la Halmashauri ya Jiji la Dodoma kwenye maonesho ya Nanenane eneo la Nzuguni jijini Dodoma.

Mchomvu alisema “tunahimiza wafugaji kufanya ufugaji wa ndani. Hivyo, ni muhimu mfugaji alime malisho yake kwa ajili ya kujiongezea kipato na tija ya maziwa na nyama. Wakati mwingine tunawafundisha ambao siyo wafugaji kulima malisho kama zao la biashara. Dodoma upatikanaji wa majani ni mgumu hivyo, mtu anaweza kulima malisho kama zao la biashara akayakata akayaanika na kuyafunga katika mfumo wa bezi na kuwauzia wafugaji. Na soko lipo wazi kabisa kwa wafugaji na bei ni nzuri beli moja tunalipata kwa shilingi 4,000-5,000”.

Alisema kuwa Dodoma ina hali ya ukame ikipata mvua mara moja. “Kutokana na hali hii tunawafundisha wafugaji kulima malisho kwa ajili ya kulisha ng’ombe wao wakiwa nyumbani. Teknolojia hii tumeitoa ‘research’ Mpwapwa na Kongwa na katika vyuo vya mifugo wanatufundisha jinsi ya kulima malisho ya mifugo na kuyahifadhi” alisema Mchomvu.

MWISHO

Comments

Popular Posts

Wananchi Makutupora wafunguka changamoto ya Maji, Umeme na Shule kwa Mkuu wa Mkoa

Waziri Mchengerwa apongeza usimamizi wa miradi jijini Dodoma

Mkataba ujenzi Uwanja wa Mpira wa Miguu wasainiwa Dodoma